Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018 Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018

Hon. Upendo Furaha Peneza

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018 Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018

MHE. UPENDO F. PENEZA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Ukiangalia katika ripoti ya Kamati, Kamati katika vitu ambavyo vimependekezwa, katika ripoti yake ukurasa wa 22 kwamba maeneo ambayo wachimbaji wadogo wadogo wamekuwa wakipata shida na wao kutorosha madini kupeleka nje ya nchi. Kamati imetaja matatizo ni kodi ambazo ziliwekwa na kodi hizi ni kodi ya ya ongezeko la thamani (VAT 18%), kodi ya zuio (ithholding tax 5%), tozo ya ushuru (service levy 0.3%), tozo ya ukaguzi kwa maana ya (inspection free ya 1%) na mrabaha wa madini katika maeneo mbalimbali ambao wachimbaji hao wadogo wanatozwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, utakubaliana nami kwamba, pamoja na kwamba Mheshimiwa Rais Magufuli alifanya kikao na wachimbaji wadogo na kukubaliana kwamba Serikali itafanya utaratibu wa kuondoa kodi hizi zinazowakabili wachimbaji wadogo, lakini ndani ya Bunge hili kuanzia mwaka 2017, tulipokuwa tukijadili Finance Bill ndani ya Bunge hili tatizo la withholding tax lilijadiliwa ndani ya Bunge hili na Mheshimiwa Mbunge wa Kahama pamoja na Mheshimiwa Mbunge wa Nzega ambao na wenyewe ni Wabunge wa Chama cha Mapinduzi na kuonyesha kwamba hili ni tatizo na Serikali isikubali kupitisha kodi hizi ambazo zinaenda kuwakaba hawa wachimbaji wadogo wadogo. Hata hivyo, hatukuweza kusikiliza, leo miaka miwili baada ya kupitisha hiyo Finance Bill, tunarudi tunakaa na wachimbaji wadogo ili kuweza kuzifuata kodi hizo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, utakubaliana nami kwamba nchi hii sasa tumekuwa na matatizo mengi, kwa sababu hatusikilizi ushauri au hatuongei na wadau kabla ya kufanya maamuzi. Tulipokuwa tunaanza Bunge hili tulipata shida kwa Serikali kuweka kodi katika huduma za bandari. Serikali imepoteza fedha nyingi sana kwa watu kuhama kusafirisha mizigo kupitia bandari yetu, Bunge hili hili lilipitisha vilevile kwa Serikali kung’ang’ania wakati Wabunge wanashauri, Bunge likapitisha tena kwa maana ya watalii kutozwa VAT katika huduma ambazo wanazozitoa. Kila mwaka, mwaka unapita, ndipo tunapokuja kufanya mabadiliko, huku watu na kodi zimeshapotea.

MHE. JACQUELINE N. MSONGOZI: Taarifa.

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Upendo Peneza, kuna taarifa. Mheshimiwa Jacqueline Ngonyani.

T A A R I F A

MHE. UPENDO PENDEZA: Mheshimiwa Naibu Spika, suala la bandari mwaka mmoja baadaye tukafanya marekebisho, suala la Utalii mwaka mmoja baadaye tukafanya marekebisho, mapato tumeshapoteza na leo kwenye suala la wachimbaji wadogo miaka miwili baadaye. Watu wa Geita ni kati ya watu ambao wamewekwa ndani kwa sababu utoroshaji wa madini. Ni kwa sababu wakipiga mahesabu, wakifanya shughuli zao za uchimbaji mpaka wakauze, faida hawaioni. Kwa hiyo, naongea kwa sababu sehemu ya wananchi waliopo Geita ndio waliokamatwa kutokana na kadhia hii. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, suala ambalo nchi inabidi ifanye ni suala la kuzingatia ushauri kwa muda, ni suala la muda, kwa sababu katika utawala hakuna kujaribu, ndio maana nadhani hata Urais mwenye sifa anayegombea miaka 40, la sivyo wangeruhusu vijana wenye miaka 18 au 25, hata Tume ya Jaji Warioba walikataa kwa sababu tunategemea watu wanaotuongoza ni watu wenye experience, ni watu ambao wapo tayari kusikiliza ushauri wa watu, watu walioko tayari kuangalia impact kabla ya kufanya maamuzi ambayo tunaendelea kuyafanya ndani ya Taifa hili. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Geita watu wengine wanaopata leseni ni watu wanaopata leseni za uchenjuaji ambayo kwa Kiingereza wanasema processing and smelting, ni watu ambao wanachukua mchanga ambao umeshafanyiwa kazi na mtu mwingine, anauchukua anauozesha kwenye sumu aina cyanide na mercury kwa ajili ya kupata dhahabu tena. Watu hawa wanaofanya shughuli za uchenjuaji wana tozo nyingi sana zinazowakabili. (Makofi)