Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Azimio la Bunge la Kuridhia Ubadilishaji Hadhi Mapori ya Akiba ya Biharamulo, Burigi, Kimisi, Ibanda na Rumanyika – Orugundu kuwa Hifadhi za Taifa

Hon. Dr. Christine Gabriel Ishengoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Azimio la Bunge la Kuridhia Ubadilishaji Hadhi Mapori ya Akiba ya Biharamulo, Burigi, Kimisi, Ibanda na Rumanyika – Orugundu kuwa Hifadhi za Taifa

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipatia nafasi. Kwanza kabisa naunga mkono hoja ya azimio iliyopo ya kupandisha hadhi Mapori ya Akiba ya Biharamulo, Burigi, Kimisi, Ibanda na Rumanyika Urugundu.

Mheshimiwa Spika, naunga mkono kwa sababu mapori haya yalikuwa yanaleta matatizo ya wananchi hasa waliozunguka mapori haya. Wakati wanaposafiri lilikuwa ni tatizo kubwa kutokana na ujangili, kutokana na watu wanaobeba silaha yaani ilikuwa ni tatizo kweli. Kwa hiyo naamini kuwa hata vijiji vyote vilivyozunguka mapori haya watakuwa wamefurahi sana, watakuwa na amani, watakuwa kwa kweli wanaona vizuri sana.

Mheshimiwa Spika, kupandisha haya mapori kuwa Hifadhi ya Taifa kutasaidia kuimarisha na kupandisha utalii kwenye nchi yetu kutokana na mapori haya, kutaimarisha na kupandisha kipato cha nchi pamoja na vijiji vinavyozunguka mapori haya na kutaleta amani kwa wananchi wanaozunguka mapori haya. Kwa kweli ni jambo zuri sana na pia kwa kutumia na kuwepo kiwanja cha Ndege cha Chato kitasaidia sana kuwapeleka Watalii wataokuwa wanakwenda kwenye mapori ya hifadhi hizi kwa sababu hizi Hifadhi za Biharamulo, Burigi, Rumanyika, Ibanda zote zinazunguka Kiwanja cha Ndege cha Chato. Pia kuwepo kwa maziwa ya Victoria, Burigi na Mto Ngono kutasaidia sana watalii na kukuza utalii wa nchi yetu.

Mheshimiwa Spika, nafurahi na sina mengi na naamini kuwa Wabunge wote wataunga mkono na wananchio wote kwa kukuza utalii wa Magharibi na yenyewe itakuwa nzuri sana kwa wananchi wetu.

Mheshimiwa Spika, ahsante na naunga mkono azimio hili. (Makofi)