Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018 Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018

Hon. Cosato David Chumi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafinga Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018 Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018

MHE. COSATO D. CHUMI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi, nitatumia vizuri dakika tano. Awali ya yote, kwa niaba ya wananchi wa Mafinga, niseme napenda kumshukuru sana Mheshimiwa Rais, niliposimama hapa 2017 kutetea suala la vinyungu kuna baadhi ya watu hawakunielewa lakini kwa watu wa Mafinga, Mufindi, Iringa, Kilolo, Njombe na maeneo yanayofanana kwetu vinyungu ni maisha na maisha ni vinyungu kwa sababu ndiyo uchumi wa watu wetu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, baada ya kusema hayo, nijielekeze kwenye jambo ambalo nimekuwa nikilisema na sitaacha kulisema, suala la Serikali kufikiria na kuona umuhimu wa kuruhusu kusafirisha mazao ya misitu saa 24. Hapa ninapozungumza saa 11.00 hii umepakia mbao zako pale Mafinga huwezi kuondoka mpaka kesho saa 12.00 asubuhi, hii tunachelewesha uchumi. Naomba Serikali na hasa Wizara ya Maliasili na Utalii waliangalie jambo hili na bahati nzuri nime-peruse naamini sijakosea nimegundua ni kanuni siyo sheria. Kwa hiyo, bado Mheshimiwa Waziri anaweza akakaa na wadau akalifanyia kazi tukaruhusu malori yasafiri saa 24 kusafirisha mazao ya misitu ili tu first track uchumi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, hapa nina hesabu ndogo tu, ukichukua mzigo kutoka Mafinga mpaka Mwanza unatumia mafuta takribani lita 880. Kwa maana kwenda kwa sababu una mzigo utatumia 530 kurudi kwa sababu huna mzigo utatumia 350 na katika kila lita moja Serikali inapata fuel levy 313. Kwa wiki moja gari inaenda mara moja lakini the same, lori kwa wiki moja ingeweza kwenda mara tatu na ikienda mara moja Serikali inapata fuel levy Sh.274,400 ikienda mara tatu kwa wiki Serikali itapata fuel levy Sh.826,200. Maana yake ni kwamba kwa wiki moja kama Serikali itapata fedha hiyo basi kwa mwezi itapata Sh.3,304,800 na fedha hizi zinaenda kwenye Road Fund. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, maana yake ni kwamba yaani sisi wenyewe kwa kutoruhusu magari yasafiri usiku tumejipunja kama Serikali. Maana yake ni nini, gari moja Serikali badala ya kupata shilingi milioni tatu point something kutokana na fuel levy inaishia kupata milioni moja inapata loss ya shilingi milioni mbili. Wote tunalia na umeme wa REA, Sh.100 kwa kila lita inaenda kwenye REA. Kwa hiyo, gari zikisafiri kwa haraka na usiku maana yake Serikali nayo itapata mapato na wale wananchi uchumi wao utakuwa umezunguka. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kutoka Mafinga mpaka Dar es Salaam tuna checkpoint siyo chini ya 10 at the same time tuna magari ya patrol, hii sheria yenyewe ukii-trace ni ya 1959 wakati Serikali ya wakoloni haina vitendea kazi vya kutosha ndiko uliko originate. Kwa hiyo, naomba kama Serikali ina wawasi na mbao pori sisi ambao miti yetu tunapanda wenyewe ituruhusu tusafirishe saa 24. Haiwezekani mchana ukutane na roli, basi na gari za Wabunge, malori hata Ulaya traditionally yanasafiri usiku. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, baada ya hilo nizungumzie suala la utalii ambao unachangia fedha nyingi za kigeni. Ukienda katika utalii kuna tozo na kodi 33 yaani kama unataka kufanya kazi kwenye industry hii inabidi ujipange na tozo 33 na hizo 33 zenyewe leo unaenda kushoto, kesho kulia, kesho kutwa nyuma, siku nyingine mbele. Hii ni sekta inayochangia sana mapato kuwa na One Stop Center ili kurahisisha facilitation kuhakikisha kwamba utalii na hizi ndege tulizoleta unaendelea kuchangia pato la Taifa kutoka asilimia 17 kwenda zaidi ya hiyo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha, ahsante sana. (Makofi)