Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018 Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji na Mitaji ya Umma kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018

Hon. Dr. Ashatu Kachwamba Kijaji

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kondoa

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018 Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji na Mitaji ya Umma kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nikushukuru sana, kwa kunipa nafasi hii, naomba nichangie Taarifa ya Kamati ya PIC kwa machache yaliyosemwa. Lakini naomba nianze hapa alikoishia Mheshimiwa Hasunga, ndugu zangu Katiba, Sheria wala Kanuni yoyote ndani ya Taifa hili, haipo iliyozuia Taifa hili kufanya biashara ndio maana PIC Mwenyekiti wake anatueleza Serikali kwamba tuendelee kusimamia mashirika yetu ili yaendelee kufanya vizuri. Sasa hiki mnachokisema kwamba Serikali ilinunua korosho elfu tatu na mia ngapi, imeuza bei hii halafu yote ipelekwe kwa mwananchi that is not a business analysis. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo hilo, nilitaka nianze kulisema hivyo, naomba tu tulie ili tuweze kusikilizana na na tuelewe nini Serikali inafanya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze na jambo moja muhimu ndani ya Kamati yetu ya PIC na niishukuru sana Kamati ya PIC kwa kuendelea kutoa ushirikiano/kutoa ushauri na hata nilipopitia kitabu chenu, maazimio yote, mmeshauri Serikali iwe iendelee kufanya improvement katika maeneo mbalimbali, nakushukuru sana kwa hili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika tangu nimeingia ndani ya Bunge hili, na ndani ya Wizara ya Fedha, jambo kubwa ambalo Kamati hii ilikuwa inaongelea ilikuwa ni kuimarisha na kuboresha ofisi ya Msajili wa Hazina. Kama Serikali tulilipokea kwa mikono miwili, tukafanyia kazi Maazimio haya ya Bunge na leo hii napenda kumpongeza Msajili wa Hazina na watu wake, wanafanya kazi nzuri sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nayasema hayo wanafanya kazi nzuri kwa sababu gawio lililotolewa na Taasisi haijawahi kutokea katika historia ya Taifa hili, tuliona wenyewe Taasisi zimetoa gawio kwa sababu ya uimara wa Ofisi ya Msajili wa Hazina.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hili la TEHAMA ambalo Kamati imesema napenda kusema kwamba tayari tumeanza na sasa hivi mfumo, wa TEHAMA wa Ofisi ya Msajili wa Hazina upo katika kufanyiwa majaribio na kati ya taasisi za Serikali, taasisi 27 tayari zimeshafanyiwa majaribio na tayari zimeshazipata mafunzo ya jinsi ya kutumia mfumo huo, mfumo wenyewe unaitwa Financial Analysis Reporting System ambayo ndiyo kazi kubwa ya Ofisi ya Msajili wa Hazina. Kwa hiyo, kama ambavyo Waheshimiwa Wabunge wamependekeza, kama ambavyo Kamati imependekeza tumesikia kama Serikali na sasa tunaifanyia kazi hii sasa itatupa nafasi popote pale alipo Msajili wa Hazina popote pale alipo Katibu Mkuu wa Hazina ataweza kuona Taasisi zote za Serikali zinafanyaje kazi. Hili ni azimio lilikuwa la Bunge na sisi kama Serikali tunaanza kufanyika kazi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika utendaji wa Ofisi ya Msajili wa Hazina na hii ndiyo maana siku zote tunapenda kusema, lazima tuwe na hofu ya Mungu, tunapoongea ndani ya Bunge hili lazima tuwe na hofu ya Mungu. Ndugu yangu, rafiki yangu Mheshimiwa Ester Bulaya uliposema kwamba Ofisi ya Msajili wa Hazina haijawahi kuwasilisha taarifa kwenye Kamati hii, hakuna aliyekataa, ni maoni ya Kamati lakini wewe, kipo ulichokiongezea kwamba taarifa hii Wizara ya Fedha na Mipango ndio inaishikilia taarifa ya Msajili wa Hazina na kuizuia kwamba isiletwe katika Bunge hili Tukufu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niseme hapana, Maazimio ya Kamati ambayo yaliletwa na sasa, tunayafanyia kazi ilikuwa ni kuhakikisha Ofisi ya Msajili wa Hazina inaongezewa Bajeti na ndicho ambacho Wizara ya Fedha na Serikali imefanya na sasa hivi ndicho walichokisema Msajili wa Hazina kwenye Kamati, wameongea na Ofisi ya Bunge kuona utaratibu na ni lini wawasilishe taarifa yao kwenye Bunge letu tukufu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, na kwa ratiba waliyopewa kufika Aprili, 29 taarifa ya Msajili wa Hazina, itakuwa imewasilishwa katika Bunge lako tukufu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa nafasi hii na naunga mkono hoja za Kamati zote mbili, ahsante sana.