Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018 Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji na Mitaji ya Umma kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018

Hon. Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018 Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji na Mitaji ya Umma kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018

WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nashukuru sana kwa kupewa hii nafasi, na kwa sababu ya muda nitakwenda haraka haraka.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la kwanza naomba nichukue nafasi hii kumpongeza sana Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kazi kubwa ambayo ameifanya katika kusimamia uchumi wetu, ambapo viashiria vyote vinaonyesha kwamba uchumi wetu unakuwa na unafanya vizuri. Haijawahi tokea katika historia mfumuko wa bei umeshuka mpaka hadi kufikia asilimia 3.0 kwa kweli ni kazi kubwa sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili, ambalo nataka niliseme kidogo ni kwamba tunayo Benki yetu ya Kilimo ambayo inafanya vizuri na pengine hapa labda nitoe ufafanuzi kidogo benki yoyote, kazi ya benki, ni kutafuta fedha mahali ziliko nyingi na kuzipeleka mahali zinapohitajika na fedha hizo zinaweza zikapatikana kwa wenye mitaji, ama kwenye mikopo ama kwa Wawekezaji kwa hiyo, benki yetu ya kilimo, inazo fedha za kutosha, za kuweza kufanya kazi, na kusaidia kilimo. Na kutokana na hilo basi, ndio maana Serikali tuliamua tukaipa, tukaomba iikopeshe Bodi ya Nafaka na Mazao Mchanganyiko fedha za kununua korosho na kwenda kuuza na imetoa fedha zote. Kwa hiyo, naomba niseme fedha za kununua korosho hatujatumia fedha tulizonunulia, fedha zilipatikana kwenye mkopo kutoka Benki ya Kilimo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba pia nitoe ufafanuzi, kumekuwa na taarifa za upotoshaji juu ya bei ambayo tumenunulia korosho, wengi wanasema tumenunua kwa shilingi 3,300. Nataka niseme hivi, bei tuliyonunulia sio hiyo, kwenye miaka ya nyuma utaratibu uliokuwepo ilikuwa ukinunua kwa shilingi 3,300 ndio unaanza kutoka gharama mbalimbali, gharama za magunia, gharama za maghala na vitu vinginevyo, ndio ilikuwa bei. Kwa sasa hivi, ile 3,300 ni ile anayolipwa mkulima, ni ile anayolipwa mkulima, kwa hiyo basi maana yake bei ya korosho, tuliyonunulia unaongeza magunia shilingi 62.50 kwa kilo, unaongeza usafiri kutoka kwenye AMCOS kwenda kweye maghala makuu. Unaongeza maghala shilingi, 38 unaongeza gharama za uendeshaji wa ushirika AMCOS shilingi 70 union shilingi 50 na gharama zingine, unaongeza cess ya Halmashauri ukizijumlisha bei yake tuliyonunulia ni zaidi ya shilingi 3,600. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tulichokifanya tumelipa vingine na vingine bado, hatujalipa, tutalipa vyote, ukijumlisha na export duty ya shilingi zaidi ni asilimia 15 ya FOB maana yake ni shilingi 560, ukijumlisha utapata ni zaidi ya 4,190,…

MHE. SELEMANI S. BUNGARA: Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa.

WAZIRI WA KILIMO: Kwa hiyo hizi gharama walizokuwa wanasema, naomba niweke hizo rekodi kwa wale wenzangu ambao hesabu zinapigwa hivyo…

(Hapa baadhi ya Wabunge walizungumza bila kufuata utaratibu)

WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, tunayo faida…

Mheshimiwa Mwenyekiti, tukishamaliza sasa kulipa na kuuza, sasa tumeuza hizo tani laki moja tunaendelea kuuza, mwisho baadae tutapata sasa tumeuliza zote kwa shilingi ngapi, gharama yote wadau wanaohusika tumewalipa shilingi ngapi, ndio tutakuja kujua kama tumepata faida shilingi au kiasi gani, sio wakati huu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba pia niweke taarifa vizuri na nihakikishe kwamba Serikali tumefanya vizuri kwa kupitia Bodi yetu ya nafaka na mazao mchanganyiko, mpaka hadi juzi, uhakiki uliofanyika ni wa thamani ya bilioni 442.9 malipo yaliyofanyika hatujakopea hata hizo tulizouza bado, tuliofanya ni shilingi bilioni 424.8; wakulima waliolipwa mpaka sasa hivi, ni 390,466.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Vyama vya Ushirika ambavyo, vimelipa ni 605 kati ya vyama 606…

MWENYEKITI: Ahsante sana Mheshimiwa Hasunga.

WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa nafasi. (Makofi)