Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018 Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji na Mitaji ya Umma kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018

Hon. Dr. Advocate Damas Daniel Ndumbaro

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Songea Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018 Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji na Mitaji ya Umma kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA AFRIKA MASHARIKI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi hii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hapa tulikuwa tunajadili taarifa hizi mbili za Kamati za Bunge. Nikianza na taarifa ya Kamati ya Bajeti, katika ukurasa wa 10, kipengele 2.2.3 kimeongelea diplomasia ya uchumi. Nichukue fursa hii kuishukuru Kamati kwa kuipongeza Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa kazi nzuri inayofanya kwenye diplomasia ya uchumi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, badala ya kujadili ripoti hii na mambo ambayo yameandikwa katika ukurasa wa 10 na 11 yanayohusu Wizara ya Mambo ya Nje, baadhi ya wachangiaji wamejikita kujadili mambo ya ushoga.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sisi Waheshimiwa Wabunge tunatumwa na wananchi kuja kuipa Serikali maagizo. Kwa ruhusa yako, naomba uniruhusu niwaulize Waheshimiwa Wabunge kama kuna Mbunge yeyote ametumwa na wananchi wake kuja kutetea ushoga humu Bungeni. Kama yupo anyooshe mkono juu au ajifanye kama anajikuna. (Makofi/Kicheko)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama huyo Mbunge hayupo ambaye ametumwa na wananchi wake, basi anyamaze milele kuanzia sasa. Ili nchi hii iweze kuendelea tunahitaji kujituma na kuchapa kazi sisi wenyewe. Tunahitaji kulipa kodi kwa mujibu wa sheria za nchi. Hakuna mwekezaji wa nje atakayekuja kuikomboa nchi hii. Wawekezaji watakuja kuchuma na ili wachume vizuri wanatuvuruga kwa kutupa masharti hayo mbalimbali kama vile ya kutaka tukubali mambo ya ushoga.

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kuongelea sovereignty of the country. Watu wengi wanadhani sovereignty ni kitu chepesi sana. Suala la
sovereignty lilianza kukubalika mwaka 1648 kupitia Westphalia Treaty. Baada ya vita ya miaka 30 umwagaji mkubwa wa damu na majadiliano ya miaka minne ukapatikana mkataba wa Westphalia ambao ndiyo umeleta suala zima la sovereignty. Leo tunalichukulia suala hili kiwepesi wepesi sana. Tunataka uhuru wetu huu wa kujiamulia mambo tuukabidhi kwa watu wengine, hilo halitawezekana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tumesemwa sana kwamba hatuna uhuru wa vyombo vya habari. Mimi naomba kusema kwamba Tanzania tuna redio 158, TV 34, magazeti 216 na tuna mitandao ya kijamii 224. Hii yote imeonyesha kitakwimu tuna uhuru wa vyombo vya habari. Pia tuko huko kuongea, kuikosoa Serikali na kutoa maoni pasipo bugudha yoyote. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo, naomba kuunga mkono taarifa hizi za Kamati zote mbili. (Makofi)