Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018 Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji na Mitaji ya Umma kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018

Hon. Hasna Sudi Katunda Mwilima

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kigoma Kusini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018 Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji na Mitaji ya Umma kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018

MHE. HASNA S. K. MWILIMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru na mimi kwa kupata nafasi ya kuchangia kamati hizi mbili, hasa Kamati yangu ya Bajeti kwa sababu mimi ni Mjumbe kwenye hiyo kamati.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kabla sijaanza kuchangia, leo asubuhi nilimsikia mdogo wangu Mheshimiwa Ester Bulaya anasema tuongee kama Taifa tusiongee kama Wabunge wa vyama tofauti, lakini Mchungaji Msigwa hapa ametuambia kama tunawatukana donors tutapataje ile asilimia 40 kuiingiza kwenye bajeti yetu ya Serikali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa mimi napata mashaka kidogo. Juzi tukiwa kwenye kamati Mheshimiwa Waziri wa Fedha alituambia kwamba Serikali ya Ubelgiji imesema haiwezi kutupa misaada kwa ajili hatuungi mkono masuala ya ushoga.

Sasa najiuliza maswali kama tunazungumza kama Taifa, yeye leo ameambiwa na Mheshimiwa Jacqueline hapa kuhusiana na suruali, ameomba Mwongozo, ina maana hapendezwi na hayo masuala. Tunawezaje kukubaliana na donors ambao wanataka vizazi vyetu ambavyo tumevizaa huko baadaye vije kuwa ni vizazi vya asilimia 80 vya ushoga, haiwezekani. (Makofi)

T A A R I F A

MHE. HASNA S. K. MWILIMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, pilipili usiyoila inakuwashaje?

KUHUSU UTARATIBU

MHE. HASNA S. K. MWILIMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Lema ni mdogo wangu, lakini kama pilipili usiyoila huwezi kujua muwasho wake ukoje. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niseme hivi, kwamba sisi kama Serikali ya Chama cha Mapinduzi tunatekeleza miradi mbalimbali kwa pesa zetu za ndani. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, na hii imejionesha. Leo kuna mtu alisema kwamba, huwezi kuweka tozo kwamba ni sehemu ya revenue, lakini kwenye taarifa ya REA, kwenye taarifa ya maji, waliyoleta Waheshimiwa Naibu Mawaziri wameonesha ni jinsi gani Wizara ya Fedha imepeleka tozo zote zilizotolewa na miradi imetekelezwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, na hiyo bilioni 67 point something iliyopelekwa kwenye miradi ya maji imetokana na nini? Imetokana na revenue ya tozo ya lita ya mafuta shilingi 50, petroli na dizeli. Kwa hiyo, pesa zetu za ndani zinatusukuma na miradi, lakini wale wafadhili ambao wanaona hawataki kutuletea masharti yasiyokuwa na msingi na taifa letu wanaendelea kuisaidia Serikali yetu ya Chama cha Mapinduzi. Kwa hiyo tuache upotoshaji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba sasa nijikite kwenye taarifa yetu ya bajeti.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunajua kwamba tuna ile miradi ya mkakati, naomba unilindie muda wangu maana Mheshimiwa Lema aliniharibia muda.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunajua tuna ule mkakati wa miradi ya kimkakati kama vile SGR pamoja na mradi wa Mchuchuma na Liganga. Niishauri Serikali, hebu iangalie hii miradi kwa sababu, deni letu la Taifa ni himilivu tuone ni jinsi gani tunaweza tukakopa tukaangalia miradi mikubwa miwili kama SGR, Liganga na Mchuchuma, ili tuwe na uhakika wa kuongeza kipato katika makusanyo yetu ya Taifa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninasema hivi kwa sababu Mradi wa SGR tumeuanza kwa pesa zetu za ndani, lakini tuangalie matawi ambayo yana umuhimu zaidi kiuchumi kuliko kuangalia tawi linalokwenda Isaka mpaka Mwanza huku tunaacha kutoka Tabora kwenda Kigoma kama alivyosema mdogo wangu Mheshimiwa Bashe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sambamba na hilo tuangalie vilevile njia ya kutoka Isaka kuelekea Kigali, ili tuweze kupata mapato zaidi na hatimaye Taifa letu litekeleze miradi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niwe mkweli, mnyonge mnyongeni haki yake mpeni. Mheshimiwa Rais ana miaka mitatu, leo ameingiza ndege sita, tunakosa kumpongeza! Hizi ndege, tunayo Dreamliner moja, Airbus mbili, tukitoa direct flight, Dar es Salaam to Guangzhou, Dar es Salaam to New Delhi, hatuwezi kuingiza mapato? Watalii watakuja direct kwa kutumia ATCL. Sasa tusikashifu hapa as if kwamba hizi ndege zilizonunuliwa hazina thamani yoyote ndani ya nchi yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba sana tuache upotoshaji, Serikali inafanya kazi. Mheshimiwa Rais ameshasema, hata wewe nyumbani kwako ukitaka ukiwa na maisha mazuri, lazima ujibane. Tutaendelea kujibana ili Taifa lisonge mbele.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema haya, naunga mkono hoja Kamati yetu ya Bajeti pamoja na hiyo Kamati nyingine.