Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018 Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji na Mitaji ya Umma kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018

Hon. Charles John Mwijage

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muleba Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018 Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji na Mitaji ya Umma kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018

MHE. CHARLES J. P. MWIJAGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nikushukuru. Awali ya yote ningependa kuwapongeza Wenyeviti waliowasilisha taarifa za Kamati zao, ni Kamati nzuri, ni kioo, kinatuonesha tunafanya nini. Langu ningependa kuanza kuchangia Kamati ya Bajeti, mimi ni Mjumbe wa PIC, nampongeza Comrade Simbachawene na niende taratibu kwa sababu sijawa mzoefu. Nimpeleke ukurasa wa 22 alipozungumzia michezo ya kubahatisha, kwamba mapato ya Serikali kwenye michezo ya kubahatisha



yameongezeka, lakini michezo ya kubahatisha imeleta uzezeta, imeleta uzembe, watu hawafanyi kazi. Sasa hili la kupata mapato kwenye kuangamiza jamii ningependa tuliangalie.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Kamati ya Bajeti nimpeleke ukurasa wa 23 alipozungumzia mafuta ya kula na zile takwimu nzuri za upunguaji wa asilima 90 wakapendekeza zaidi kwamba tubaini endapo uzalishaji wa ndani umeongezeka, ningependa aende zaidi aangalie mchango wa crude palm oil, mchango wa mafuta ya kupikia katika re- export na aangalie mchango wa re-export commodity katika uchumi wa Taifa, aangalie viwanda vimeendeleaje baada ya maamuzi haya, lakini aende zaidi aangalie mafuta haya yalikuwa yanachangiaje kwenye maamuzi ya nje.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia Kamati ya Bajeti nimpongeze kwa pendekezo lao la ukurasa wa 25 alipoitaka Serikali kwamba iwashirikishe kabla haijaenda kwenye CET - Common External Tariff, lakini ningependa aongeze hapo kwamba Serikali inapokwenda kwenye CET wakati inalenga East Africa Community ijue kwamba ina mshirika mwingine anaitwa SADC. Sisi tuko East African Community lakini tuwe waangalifu tusiwekewe magoli na wenzetu wa East Africa katika mchezo ambao sisi tunafaidi kutoka kwenye SADC. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukurasa wa 26 Kamati ya Bajeti imezungumzia suala la udhoofu katika kukusanya mapato ya majengo, kwamba pato katika upande wa majengo ni dhoofu, ningependa kumwuliza au waiulize Serikali kwamba lile pendekezo, ule ushauri Mheshimiwa Rais kwamba watoze kiwango kidogo ili nchi, nyumba zote ziweze kulipa limefikia wapi?



Mheshimiwa Mwenyekiti, niende kwenye Kamati yangu, Msajili wa Hazina au Taasisi, Kamati yetu inasimamia mashirika 270. Mashirika haya 270 yana fursa kubwa kwenye uchumi wa Taifa, lakini linaloonekana wazi na kama tulivyoeleza kuna under capitalization; mashirika haya hayapewi pesa ya kutosha, lakini yakipewa pesa ya kutosha yatazalisha pato kubwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kushauri kama tulivyowashauri, huyu ni ng’ombe wa maziwa, tumpe nyasi, tukubali tumpe mashudu, kwetu wanasema atana gatalonda, poteza kusudi uje upate. Katika eneo hili la mashirika 270 kuna fursa kubwa ya ajira, lakini kuna upungufu wa weledi katika kufanya shughuli, si suala la vyeti suala la weledi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niwapeleke kwenye ukurasa wa tisa wale wanaofuatilia kitabu cha PIC, ukiangalia makampuni yaliyolipa gawio makampuni 11, kuna kampuni inalipa bilioni tisa, naomba nishauri kwamba hawa ndiyo ng’ombe wa maziwa, kampuni kama NMB, lazima itengenezewe mazingira na ituoneshe namna gani italipa zaidi, kampuni kama PUMA Energy lazima itengenezewe mazingira kusudi iweze kulipa zaidi, kuna kampuni kama Cigarette lazima itengenezewe mazingira na kampuni kama Tanzania Planting au TPC. Kwa hiyo, kampuni zinazofanya vizuri, lazima tuzifuatilie kusudi tuweze kupata zaidi katika mapato hayo. (Makofi)


Mheshimiwa Mwenyekiti, wale wanaofuatilia kitabu chetu niwapeleke ukurasa wa 28, nataka nilizungumzie alilozungumza Makamu Mwenyekiti wa Kamati yangu kuhusu mtazamo mpya wa SUMA JKT. SUMA JKT ni zaidi ya JKT tunayoijua, Taifa sasa linao upungufu wa watu wenye weledi, lakini iko fursa kubwa ndani ya JKT kukusanya vijana waliopewa mafunzo, wakapelekwa JKT wakapewa mafunzo mazuri na wakaweza kufanya vizuri. JKT Kigoma wana mradi wa mawese, wanaweza kupelekwa Kigoma, wakalima mawese na kuweza kuzalisha bidhaa za sabuni na zingine.



Nashauri na Kamati yetu imeshauri kwamba tuliangalie suala hilo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine, bandari yetu ya Dar es Salam, Bandari ya Dar es Salam nao ni mgodi na kimsingi sisi bandari ya Dar es Salam hatujaitumia kikamilifu. Kamati yetu iliona Bandari ya Dar es Salam ina matatizo makubwa makubwa matatu. Tatizo la kwanza ni la kisheria na kama mnavyojua Waheshimiwa Wabunge, tuliwahi kutunga Sheria, kwa mfano, ile Sheria ya VAT iliweza kuiathiri Bandari ya Dar es Salam. Pia sasa kuna ile Sheria ya axle weight ambapo mteja wetu namba mbili wa bandari, mteja wa bandari wa nje wa kwanza ni DRC Kongo, wa pili ni Zambia, lakini Zambia sasa inajiandaa kususia Bandari ya Dar es Salam kwa sababu ya Sheria ya axle weight. Kwa hiyo tunapotunga Sheria, kama nilivyosema mwanzoni tuiangalie SADC badala ya kuiangalia Afrika Mashariki tupu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine ni la TEHAMA, ukiangalia ule wepesi wa kufanya shughuli easily of doing business, eneo ambalo Tanzania tunafanya vibaya sana ni cross border business, cross border business inaanzia bandarini na tatizo mojawapo ni kwamba mifumo ya bandari ya kuhamisha bidhaa haisomani, TEHAMA hazisomani, yule anayetoa mzigo bandarini, anayelipisha anayetunza mzigo, hawasomani. Kwa hiyo ninachotaka kuzungumza ni kwamba tu-improve upande huo kusudi bandari yetu tuweze kuifanyia vizuri.


Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na kuwekeza kwenye magati, suala lingine ni kuwekeza rasilimali watu, watu wenye weledi na watu wenye motisha. Tukiweza kuwekeza kwenye weledi wa watu wetu tutaweza kuiwezesha bandari yetu. Bandari ya Dar es Salam, ile geographical location advantage inaondoka; Beila, mtu ambaye alikuwa na disadvantage anatumomonyoa taratibu, lakini watu wengine wana-opt kwenda Durban, lakini fursa za nchi tulizonazo, ukiangalia Tanzania inayokuja hali ni nzuri sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hayo machache, naomba kuunga mkono hoja yangu ya PIC. (Makofi)