Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018 Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji na Mitaji ya Umma kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018

Hon. Hamidu Hassan Bobali

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Mchinga

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018 Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji na Mitaji ya Umma kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018

MHE. HAMIDU H. BOBALI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa fursa hii kuchangia. Niseme kwamba nimezipitia hizi taarifa za Kamati zote mbili; Kamati ya Bajeti na Kamati ya PIC. Niseme wazi kabisa kwamba ninawapongeza sana Wajumbe wa PIC kwa kazi kubwa waliyoifanya na wameleta taarifa ambayo iko very heavy, nawashukuru sana na nawapongeza. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninataka kuchangia jambo moja tu kwenye mjadala huu leo na jambo lenyewe si lingine ni korosho. Mimi nilitegemea Mheshimiwa Mwenyekiti wa Kamati ya Bajeti angetueleza kwamba hizi fedha ambazo Serikali wanatumia kununua korosho zimetoka kwenye kifungu gani, angeanzia hapo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini la pili, wakulima wamecheleweshewa fedha zao sana, hiyo haitoshi tumesikia juzi Serikali imeuza korosho tani laki moja. Binafsi nilimfuata Waziri nikaenda kumpongeza kwamba sasa najua wakulima watapata fedha zao. Cha ajabu korosho tani laki moja imeuzwa kwa mujibu wa maelezo ya Waziri wa Katiba, nilikuwa namuangalia, Serikali imeingiza shilingi bilioni 418 kwa tani laki moja. Kwa mahesabu ya kawaida itakuwa Serikali imeuza korosho kwa shilingi 4,180.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa kama Serikali imeuza shilingi 4,180 Serikali ije itueleze mnaendelea kulipa grade one shilingi 3,300 kwa faida hii kubwa mliyoipata, hilo moja. La pili…

MHE. PASCAL Y. HAONGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa.

MWENYEKITI: Taarifa ya kwanza hiyo.

T A A R I F A

MHE. HAMIDU H. BOBALI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru, nimeikubali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, cha ajabu zaidi mimi nilimfuatilia Mheshimiwa Rais wakati anatangaza uamuzi wa kwenda kununua korosho alisema atanunua korosho za Watanzania wote kwa shilingi 3,300 hakuna kauli nyingine iliyotolewa na kiongozi yeyote mwingine kubatilisha bei hii.

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa.

MWENYEKITI: Taarifa.

T A A R I F A

MWENYEKITI: Ahsante sana Mheshimiwa Kuchauka, Mheshimiwa Bobali.

MHE. HAMIDU H. BOBALI: Mheshimiwa Mwenyekiti, sikubaliani nayo taarifa aliyonipa Mheshimiwa Kuchauka kwa sababu moja, Serikali ilikwenda kwenye Kamati ya Kilimo ikakiri kwamba korosho gharama yake ilivyo sasa ukijumlisha hizo zote ni shilingi 3,800; Serikali tena kwa taarifa yake yenyewe kabisa iliyo rasmi imekiri gharama ya korosho ni shilingi 3,800 ukijumlisha gharama hizo zote ambazo Mheshimiwa Kuchauka amezisema. Sasa kama mmeuza shilingi 4,180 tunataka kauli mtuambie hii iliyoongezeka mtawarudishia wakulima? Hilo moja. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili, sasa hivi ninapozungumza wakulima wanalipwa shilingi 2,640 hawalipwi tena shilingi 3,300…(Makofi)

MHE. HAMIDU H. BOBALI: Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Rais alisema korosho itakuwa…

NAIBU WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA: Mheshimiwa Mwenyekiti, Kuhusu Utararibu.

MWENYEKITI: Haya Kuhusu Utaratibu.

KUHUSU UTARATIBU

MHE. HAMIDU H. BOBALI: Mheshimiwa Mwenyekiti, wakulima sasa hivi wanalipwa shilingi 2,640; kama kuna Waziri ama Mbunge anasema nasema uongo akathibitisha kwamba mimi nasema uongo, nipo radhi kujiuzuru Ubunge kama unaweza kuthibitisha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama mimi ninayoyasema kwamba wakulima hawalipwi shilingi 2,640 na anaweza kunithibitishia, nitajiuzuru Ubunge. Wakulima wanalipwa shilingi 2,640 Rais alisema wakulima wote watalipwa shilingi 3,300 kwa kuingiziwa moja kwa moja. Ni tamko gani la Serikali limetolewa na kiongozi yeyote wa Serikali likabadilisha bei hii? (Makofi)