Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018 Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji na Mitaji ya Umma kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018

Hon. Ester Amos Bulaya

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018 Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji na Mitaji ya Umma kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018

MHE. ESTER A. BULAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi, kwanza kabla sijaanza kuchangia, lazima nisisitize mambo ya msingi na kama Bunge lazima tuvae viatu vyetu katika kuisimamia Serikali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imekuwa na tabia ya kutofanyia kazi Maazimio ya Bunge na Kamati yetu tumesema, na changamoto inayotokana na kutofanyia kazi maazimio ya Bunge lako tukufu ni kusuasua kwa uwekezaji na utendaji wa mashirika yetu, hilo ni jambo baya sana na inaonesha Serikali hii inalidharau Bunge na tumesema kwenye Kamati yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti na Wabunge wenzangu, kuna suala la Kikanuni hapa kama ambavyo Kamati ya PAC na Kamati ya LAAC inavyofanyia kazi taarifa ya CAG sisi tunafanya kazi na Msajili wa Hazina. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hivi tunavyoongea hatujawahi kupewa ripoti na Msajili wa Hazina, hili ni jambo la kikanuni na tulipohoji tukaambiwa taarifa inakwama Wizara ya Fedha, aibu, mnatufanya sisi tushindwe kufanya kazi yetu vizuri kwa niaba ya Bunge kwa kusimamia mashirika na kuja kuishauri Serikali. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze na shirika letu pendwa la ndege, ni jambo jema kufufua Shirika la Ndege na hakuna mtu anayepinga. Lakini tujiulize tunafufua wakati gani, tuna mipango gani, kwa malengo gani ya ushindani wa kibiashara. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Shirika letu la Ndege kwa miaka mitatu mfufulizo wametengeneza hasara ya bilioni 316, mnajua ni kwa sababu gani! Shirika halina mpango wa kibiashara. Kwa nini tusibebe kitimoto, tusibebe mbuzi, tusibebe samaki kwenye ndege ya abiria? Haya mambo hayatutendei haki kama Taifa, kwa mfano, tumewekeza. Kwa mfano trilioni moja kununua ndege, lakini hivi karibuni tumeambiwa shirika letu limeingiza bilioni nne halafu limeenda kufanyia ukarabati ndege mbili kwa bilioni 13. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kama haitoshi tuna upungufu wa marubani, Mwenyekiti wa Bodi alikuja kutuambia kwenye Kamati na ma-engineer yaani hivi ninavyowaambia marubani wa bombadier ndio wanaorusha dreamliner. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, yaani ni kama dereva wa Noah mkabidhi basi la Shabiby abebe abiria, ndio mambo hayo! (Makofi/Kicheko)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunataka Shirika letu la Ndege lakini lazima mambo kama haya yafanyiwe kazi ili Shirika letu liwe na ufanisi, lijiendeshe kibiashara, lakini tuwe na usalama wa abiria wetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali yetu imewekeza takribani shilingi trilioni 54 kwenye Mashirika ambayo yana hisa kuanzia asilimia 50 mpaka 100, lakini imepata faida asilimia moja tu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tumewekeza trilioni 54 faida kwa mwaka 2017 ilipata bilioni 800 sasa hivi, kwa hesabu za Juni, 2018 faida iliyopatikana bilioni 600 pungufu ya bilioni zaidi ya 200. Hizo bilioni 200 mngenipa bilioni tano ningemaliza mradi wangu wa maji Bunda. Hizo bilioni 200 hapa kila Mbunge ana matatizo lukuki au basi at least mngeenda kupunguza ahadi yenu ya shilingi milioni 50 kila kijiji ambayo hamjaitekeza, tangu muingie madarakani. (Makofi)

NAIBU WAZIRI WA KILIMO (MHE. INNOCENT L. BASHUNGWA): Mheshimiwa Mwenyekiti taarifa.

MWENYEKITI: Taarifa Mheshimiwa.

T A A R I F A

MWENYEKITI: Ahsante sana, Mheshimiwa Bashungwa, Mheshimiwa Esther taarifa.

MHE. ESTER A. BULAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, niu-junior unamsumbua sio type yangu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine nililotaka kulisema hapa, tumesema Serikali haitoa mitaji kwenye mashirika mbalimbali. Nitoe mfano, tumeanzisha Benki ya Kilimo, Benki yetu ya Kilimo, lengo kubwa la kuanzisha ni kusaidia wakulima wetu, Benki yetu ili isimame ilikuwa inahitaji Mtaji wa bilioni 800, lakini sasa hivi ina bilioni 60 tu. (Makofi)

Waheshimiwa Wabunge mnakumbuka Kilimo ndio kinaajiri asilimia zaidi ya 70 ya Watanzania na kuna habari chini ya carpet kwamba benki hii, ambayo ina mtaji, wa bilioni 60 ndio alikuwa amepewa kazi ya kwenda kununua korosho za bilioni 900 wapi na wapi? Aibu haiwezekani na ni kwa sababu Serikali haifatilii mashirika yake haifuatilii vyombo vyake. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti na hili pia sijui mnabisha?

MHE. RICHARD P. MBOGO: Taarifa.

MHE. ESTER A. BULAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, haya.

MWENYEKITI: Taarifa Mheshimiwa Mbogo.

T A A R I F A

MWENYEKITI: Mheshimiwa Ester Bulaya taarifa hiyo.

MHE. ESTER A. BULAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, siipokei angesema hiyo pesa, hiyo pesa anayoisema ni mkopo kutoka TIB yaani Benki yenye mtaji wa bilioni 60 unaenda kukopa kuipa bilioni mia mbili naa; na hapa kwenye taarifa yetu tumesema kuna hatari ya benki kufilisika kwa sababu itashindwa kulipa deni. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini jambo lingine ambalo nataka kusema hapa ni Serikali hii ya Chama cha Mapinduzi kukopa bila kulipa madeni kwa taasisi zake na kusababisha utendaji mbovu wa mashirika TANESCO inadai zaidi ya bilioni mia mbili naa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukienda kwenye ripoti yetu utaona JWTZ inadaiwa Bilioni 8…

MHE. GOODLUCK A. MLINGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa.

MWENYEKITI: Taarifa muda wako umemalizika Mheshimiwa Ester.

MHE. ESTER A. BULAYA: Ya kwanza eehe.

MWENYEKITI: Ya kwanza eeh, haya Taarifa Mheshimiwa.

MHE. ESTER A. BULAYA: Na ulinde muda wangu.

T A A R I F A

MHE. ESTER A. BULAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa yake siipokei kwa sababu SUMA JKT, viongozi wa Chama cha Mapinduzi wamekopa matrekta na hamjalipa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, JWTZ inadaiwa bilioni nane, Wizara ya Maji - DAWASA inadaiwa bilioni sita, Wizara ya Afya
- Muhimbili inadaiwa bilioni 2 na maeneo mengine. Lakini tunajua mbali ya madeni, ambayo...

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Taarifa.

MHE. ESTER A. BULAYA:…TANESCO inaidai Serikali, Shirika hili linashindwa kujiendesha, kwa sababu inashindwa kulipa madeni, na hela nyingi zipo kwa Serikali. Serikali inaua Mashirika yake…

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa.

MWENYEKITI: Mheshimiwa Waziri, Mheshimiwa Ester taarifa tafadhali, Mheshimiwa Waziri.

T A A R I F A

MWENYEKITI: Mheshimiwa Ester Bulaya.

MHE. ESTER A. BULAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, hapa ndio nimesema moja ya maazimio ambayo hayajafanyiwa kazi kwenye taarifa yetu ya mwaka jana ni pamoja na Serikali kutolipa madeni, hapo sijazungumza madeni ya Mifuko ya Hifadhi ya Jamii, takribani…

MBUNGE FULANI: Taarifa Mwenyekiti.

MHE. ESTER A. BULAYA: mmefilisi nyie.

(Hapa baadhi ya Wabunge walizungumza bila kufuata utaratibu)

MHE. ESTER A. BULAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, haya lazima tuyaseme kwa sababu wazalendo wanasema kwa lengo la kujenga, sisi wengine tusipokufa na ajali, tuna maisha marefu sana, tunahitaji Serikali itimize wajibu wake ili wananchi wapate huduma bora na mashirika yetu yafanye kazi, kwa ufanisi, lipeni madeni, acheni blah blah!

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana. (Makofi)