Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018 Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa kuhusu Usimamizi wa Matumizi ya Fedha za Umma katika Serikali za Mitaa kwa Mwaka wa Fedha ulioishia tarehe 30 Juni, 2017

Hon. Omari Mohamed Kigua

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilindi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018 Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa kuhusu Usimamizi wa Matumizi ya Fedha za Umma katika Serikali za Mitaa kwa Mwaka wa Fedha ulioishia tarehe 30 Juni, 2017

MHE. OMARI M. KIGUA: Mheshimiwa Naibu Spika, awali ya yote, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuweza kuzungumza jioni ya leo. Kwa kweli ni jambo la kusikitisha sana kama kila mmoja wetu miongoni mwa sisi Wabunge anaweza kusimama tu na kutoa taarifa ambayo inaweza ikawa ina- distort nchi hii. Nchi hii ina wafadhili, nchi hii ina walipa kodi; unaposema 1.5 trillion imepotea, imetumika vibaya, maana yake unawafanya walipa kodi wasiweze kulipa kodi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ukweli usiopingika ni kwamba Kamati za PAC na LAAC msingi wa kazi zao ni kupitia ripoti ya CAG. CAG ndio jicho la Kamati hizi mbili. Niwakumbushe wazungumzaji waliopita hapa kwamba Ripoti ya CAG inapopita, inapokuja kwenye Kamati zetu, tunapitia lakini pia tunawashirikisha Makatibu Wakuu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, suala la audit query ni suala la kawaida kabisa. Huwezi ukasema kwamba hoja hazitakuwepo. Tukumbuke kwamba suala la mifumo hii ni ya kawaida kabisa. Wamezungumza hapa ndugu zangu, baadhi ya Wajumbe wa Kamati ya PAC, wanasema kwamba Hazina wanatumia excel. Haiingii akilini hata kidogo.

Mheshimiwa Naibu Spika, huwezi ukajumuisha hesabu za Serikali za Mitaa, Serikali Kuu na mashirika kwa kutumia excel. Hii haiingii akilini hata kidogo. Narudia kusema tena kwamba ripoti ya CAG siyo conclusive. Maana yake ni kwamba bado kuna room ya kukaa na kuweka sawa. Ndiyo maana kwenye taarifa hii kuna sehemu kuna neno “reconciliation” na “adjustment.” (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, tafsiri yake ni nini? Maana yake hoja ya CAG walikaa na watu wa Hazina. Sasa wapo Wajumbe hapa ambao hawakupata fursa ya kumsikiliza Accountant General kazungumza nini. Sasa kuna watu hapa wamefundishwa taarifa, ambao nawalaumu sana. Nadhani hili siyo jambo zuri. Mtu kuwa na weledi mkubwa wa mambo ya hesabu, usikubali kuchukua taarifa za mitaani. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, limezungumziwa suala la shilingi bilioni 290, sheria inasema kwamba BoT wanaweza wakatoa 1.2 expenditure kwa Serikali kwa hiyo bado Serikali iliweza kutumia kiasi kidogo sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, suala la Zanzibar, mapato yale yanakusanywa na TRA Zanzibar, lakini ni lazima yaingie kwenye Mfuko Mkuu wa Serikali lakini yanarudi Zanzibar. Ubaya uko wapi hapo? Sasa tukubaliane jambo moja; hebu tuweke utaratibu wa kutoruhusu kila mtu kuzungumza jinsi mtu anavyoona.

Mheshimiwa Naibu Spika, wewe unazungumza taarifa ya CAG ambayo haijawa-verified, sisi tumemwona CAG hapa, amesema mwenyewe kwamba hakuna matumizi mabaya wala hakuna wizi. Suala la CAG yeye hagundui theft na fraud, anatoa opinion. Hawa wenzetu suala la wizi wamelitoa wapi? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kuna Mjumbe hapa kasema kwamba siyo 1.5 trillion, imekwenda mpaka trilioni mbili, atuambie ana ripoti nyingine ya CAG nyingine? Hilo naomba athibitishe, kwa sababu sisi tume-rely on Taarifa ya CAG, yeye taarifa ya shilingi trilioni mbili kaipata wapi? Huwezi uka-distort profession yako kwa sababu ya mambo ya kisiasa. Umeapa, lazima uwe mkweli. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nadhani Wajumbe badala ya kuipitia taarifa vizuri na kuangalia maoni ya Kamati yetu, tumezungumza mambo mazuri sana. Serikali hii mambo yote ambayo hayako sawa yamezungumzwa kwenye taarifa hii, kwa nini wanang’ang’ania eneo ambalo tayari CAG ameshali-clear? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, labda nitoe ushauri mmoja, kama kuna Mjumbe ambaye bado ana wasiwasi, anaweza bado akamwomba CAG na utaratibu unaruhusu, lakini suala la 1.5 trillion tayari limeshafungwa page na halipo tena. Naomba msiwaaminishe Watanzania kuwa kuna wizi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nashangaa sana, wakati tunaandika ripoti hii tulikuwa pamoja na wenzetu. Walikuwa na nafasi ya kumwuliza CAG. Vile vile PST kwa maana ya Paymaster General, alikuja, kwa nini hawakumwuliza maswali hayo? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nataka nikuthibitishie jambo moja; watumishi waliopo Wizara ya Fedha pale ni watu ambao ni very professional. Mhasibu Mkuu wa Serikali, Mhasibu Mkuu Msaidizi wa Serikali, wote ni CPA holders. Hiyo ni sambamba na watu wa CAG. (Makofi)

MHE. SALOME W. MAKAMBA: Mheshimiwa Naibu Spika, Kuhusu Utaratibu.

MHE. OMARI M. KIGUA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, kuanza kuhoji competence yao, nadhani siyo sahihi. Tukubaliane kabisa kwamba suala la kurekebisha mifumo ni sawasawa…

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Kigua subiri. Mheshimiwa Salome, kanuni inayovunjwa.

KUHUSU UTARATIBU

MHE. OMARI M. KIGUA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Pengine labda niendelee kwa kusema maneno yafuatayo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, mahusiano kati ya Ofisi ya Bunge na CAG ni mazuri sana na Kamati za LAAC na PAC zimeweza kufanya kazi nzuri sana kwa kupitia Ofisi ya CAG. Tukubaliane kwamba hata katika utaratibu wetu wa Kamati hizi, pia watumishi wa CAG wakija pale huwa tunawapa challenge, umekagua hili; hili siyo sawa na hili siyo sawa. Huo ndiyo utaratibu wetu wa kazi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ninapozungumzia suala la kutumia excel, nazungumza professionally kwamba haiwezekani kutumia excel kuweza ku-consolidate hesabu za Serikali nzima, haiwezekani. Pia na-refer majibu ya Accountant General kwamba hilo halijafanyika. Sasa haya ni mambo tu ya kawaida. Hizi zinaitwa hoja za ukaguzi na hoja za ukaguzi zipo kila siku. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kueleza eneo hilo, sasa nirudi kwenye suala la mikataba hasi ya NDC. Hapa tulijikita zaidi, tuliona ni eneo ambalo haliko vizuri, nadhani katika taarifa yetu ya Kamati hapa tumeelezea vizuri sana. Ushauri wangu kwa Serikali, kupitia kwa Attorney General pamoja na Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda, wapitie waangalie mikataba ya TANCOAL, haijakaa vizuri hata kidogo. Kwa sababu tunaiona dhamira ya Mheshimiwa Rais ya kuhakikisha kwamba tunapata mapato, sasa inawezekana vipi kama una mikataba hasi? Maana yake gawio lile haliwezi kupatikana. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, nashauri sana, maeneo yote ambayo tumeainisha yahakikishwe kwamba yanafanyiwa kazi. Naamini kabisa kwamba taarifa hii, kwa sababu tumewashirikisha wenzetu wa upande wa pili, italeta mafanikio makubwa sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kusema hayo machache, nashukuru sana. Ahsante. (Makofi)