Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018 Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa kuhusu Usimamizi wa Matumizi ya Fedha za Umma katika Serikali za Mitaa kwa Mwaka wa Fedha ulioishia tarehe 30 Juni, 2017

Hon. Felister Aloyce Bura

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018 Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa kuhusu Usimamizi wa Matumizi ya Fedha za Umma katika Serikali za Mitaa kwa Mwaka wa Fedha ulioishia tarehe 30 Juni, 2017

MHE. FELISTER A. BURA: Mheshimiwa Naibu Spika, nianze kwa kumshukuru Mungu kwa neema yake iliyonipa nafasi ya kusimama mbele ya Bunge lako tukufu.

(Hapa baadhi ya Wabunge walizungumza bila kufuata utaratibu)

MHE. FELISTER A. BURA: Mheshimiwa Naibu Spika, nichukue nafasi hii kumpongeza Athuman Kihamia, nachukua nafasi hii kumpongeza Athuman Kihamia aliyekuwa Mkurugenzi wa Kaliua, alipofika Kaliua yeye ndiye aliyetoa taarifa Serikali juu ya ubadhirifu mtu kama huyu anastahili kupongezwa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ninashangaa mtu aliyesema juu ya ubadhirifu analaumiwa leo, sasa je, angenyamaza taarifa hizi zingepatikana wapi? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ni Mjumbe wa PAC na nitasema kweli yale ambayo tuliyazungumza Kamati ya PAC, Vote 20 haikujadiliwa PAC na hatukuwahi kuijadili na mtu anaposimama na kusema kwamba vote 20 ni kichaka anamkosea yule anayetumia vote 20. Huwezi kusema kwamba vote 20 ni kichaka, wakati vote 20 haikuwahi kujadiliwa na PAC na mimi nakwambia mimi ni Mjumbe…(Makofi)

MHE. CATHERINE N. RUGE: Mheshimiwa Naibu Spika, taarifa.

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Felister Bura kuna taarifa, Mheshimiwa Catherine Ruge.

T A A R I F A

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Felister Bura unaipokea taarifa hiyo?

MHE. FELISTER A. BURA: Mheshimiwa Naibu Spika, wala siwezi kupokea taarifa ya mtu ambaye sio Mjumbe wa Kamati, siwezi kupokea taarifa ya mtu ambaye sio Mjumbe wa Kamati.

WABUNGE FULANI: Buuuuu!

MHE. FELISTER A. BURA: Mheshimiwa Naibu Spika naendelea, Kamati yetu, Kamati ya PAC, upande wa pili sijui wamepatwa ugonjwa gani wa kelele!

(Hapa baadhi ya Wabunge walizungumza bila kufuata utaratibu)

MHE. FELISTER A. BURA: Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu shilingi trilioni 1.5, tumezungumza sana, vizuri sana Kamati yetu imezungumza vizuri sana na taarifa tumeandika kuanzia ukurasa wa 15 hadi ukurasa wa 31 na tumefafanua kila jambo, kila kipengele hata yule ambaye hajui mahesabu anaweza akasoma na akaelewa kwamba tumeeleza nini kuhusu pesa trilioni 1.5 na naomba nisome ukurasa wa 35 inasema hivi na taarifa hii amesoma Mwenyekiti wa PAC; “Mheshimiwa Spika, katika kuhitimisha suala la tofauti ya shilingi trilioni 1.5 kati ya mapato ya Serikali na makusanyo kwa mwaka wa fedha 2016/2017 naomba kuweka kumbukumbu sahihi katika Bunge lako tukufu kuwa tofauti hiyo haikuwepo baada ya marekebisho ya hesabu kufanyika.” (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, wakati tunajadili taarifa hii tulikuwa Wabunge mchanganyiko chama cha CCM Wajumbe walikuwepo, vyama vya upinzani Wajumbe wake walikuwepo, na waliuliza maswali na walisikia jinsi CAG alivyoeleza na walisikia TRA walikuwepo, BOT walikuwepo, Wizara ya Fedha walikuwepo walisema waziwazi wala hawakuficha jambo lolote, leo mtu anakuja anauliza trilioni
1.5 iko wapi?

MBUNGE FULANI: Wazushi hao

MHE. FELISTER A. BURA: Mheshimiwa Naibu Spika, sema humu, utapata taarifa zote.

MBUNGE FULANI: Wazushi hao

MHE. FELISTER A. BURA: Mheshimiwa Naibu Spika, soma taarifa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, waliodhani kwamba Tanzania bado itakuwa shamba la bibi, watapata taabu sana.

MHE. JOHN W. HECHE: Mheshimiwa Naibu Spika, taarifa.

MHE. FELISTER A. BURA: Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Rais wetu yuko makini na anafanya kazi kwa umakini.

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Felister Bura, Mheshimiwa John Heche.

MBUNGE FULANI: Sikiliza.

T A A R I F A

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Felister Bura unaipokea taarifa hiyo?

MHE. FELISTER A. BURA: Mheshimiwa Naibu Spika, sipokei taarifa hiyo, unajua naomba unajua kupe aking’ang’ania kwenye ngozi hata kama anachomwa moto, ile ngozi inachomwa moto hawezi kujua, kwa hiyo, ameng’ang’ania jambo moja ambalo limefafanuliwa mbele kwenye taarifa hataki kusoma, asome taarifa yetu mpaka ukurasa wa 37 ataona maelezo, sasa aking’ang’ania ukurasa wa 15; atang’ang’ania na sisi tunasonga mbele. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali ya Awamu ya Tano, inapiga vita ufisadi na wale watendaji waliodhani kwamba…

MHE. JAMES K. MILLYA: Taarifa.

MHE. FELISTER A. BURA: …ukifanya ufisadi, ndio namna ya kufanya kazi...

MHE. JAMES K. MILLYA: Taarifa.

MHE. FELISTER A. BURA: Mheshimiwa Naibu Spika hawatafika mbali.

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Felister Bura kuna taarifa nyingine, Mheshimiwa James Millya.

T A A R I F A

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Felister Bura unaipokea taarifa hiyo?

MHE. FELISTER A. BURA: Mheshimiwa Naibu Spika, naipokea kwa mikono miwili. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niendelee, na niseme kwamba…

MHE. CECIL D. MWAMBE: Mheshimiwa Naibu Spika, taarifa.

MHE. FELISTER A. BURA:… kwa sasa Serikali ya Awamu ya Tano, haina muda kabisa na wale wabadhirifu wa mali ya umma.

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Felister Bura, kuna taarifa. Mheshimiwa Mwambe.

T A A R I F A

MHE: FELISTER A. BURA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kuwa macho na kuwarudisha Waheshimiwa Wabunge kwenye mstari.

Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyosema mwanzo Serikali ya Awamu ya Tano, haina mchezo, na wabadhirifu wa mali ya umma, haina mchezo na Mheshimiwa Rais Dkt. Magufuli alipoingia madarakani aliona mambo yaliyofanywa na baadhi ya mashirika ya umma na akawatoa wale, haraka ilivyowezekana. Nitoe mfano, kuna uwekezaji usio tija ambao Serikali iliona na baadhi ya watendaji kwa mfano NSSF Wakurugenzi wote, walifukuzwa kazi, kwa miradi isiyokuwa na tija. (Makofi)

Sasa niombe Serikali yangu…

MHE. CECIL D. MWAMBE: Mheshimiwa Naibu Spika, taarifa.

(Hapa baadhi ya Wabunge walizungumza bila kufuata utaratibu)

MHE. FELISTER A. BURA: Mheshimiwa Naibu Spika, ya Awamu ya Tano, kusimamia miradi yote…

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Felister Bura kuna taarifa.

T A A R I F A

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Felister Bura, unaipokea taarifa hiyo?

MHE. FELISTER A. BURA: Mheshimiwa Naibu Spika, sipokei taarifa kwa sababu Mheshimiwa Mbunge hataki kusoma taarifa yote, hataki kusoma kuanzia ukurasa wa 15 hadi ukurasa wa 37, asome apate mantiki yote ya maelezo ya CAG, Ofisi ya Hazina, BOT na Mamlaka ya Mapato Tanzania, kwa hiyo taarifa yake sipokei.

Mheshimiwa Naibu Spika, nimesema kwamba nchi yetu, Serikali ya Awamu ya Tano, ambaye anafanya kazi…

MHE. JAMES K. MILLYA: Taarifa! Taarifa!

MBUNGE FULANI: Endelea, hiyo hiyo.

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa James Millya.

T A A R I F A

MHE. JAMES K. MILLYA: Mheshimiwa Naibu Spika, nampa taarifa ndugu yangu kwenye ukurasa wa 37 kwamba ripoti ya PAC pale mwisho inasema hivi naomba ninukuu; “Kwa hiyo kitu tulichokuwa tunashughulikia nacho hapa, je, tofauti hii, imeletwa na nini? Tutapata maelezo ya kutosha kuhusu tofauti hii na ukiisoma ripoti yetu, utaona ile table, inaonesha kwamba tumepata reconciliation.” (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, huyu ni CAG, kwa hiyo hilo linajibu hilo swali, naomba kuwasilisha. (Makofi)

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Felister Bura, unaipokea taarifa hiyo?

MHE. FELISTER A. BURA: Mheshimiwa Naibu Spika, namshukuru sana Mheshimiwa Millya kwa kunisaidia na kuwasaidia wengine wasiotaka kusoma, wasome hii taarifa, kwa nini hawataki kuisoma!

MHE. PASCAL Y. HAONGA: Mheshimiwa Naibu Spika, taarifa.

MHE. FELISTER A. BURA: Mheshimiwa Naibu Spika, nimesema, tunaiomba Serikali yetu, sasa isimamie miradi…

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Haonga, kwa Mheshimiwa Felister Bura hiyo itakuwa ni taarifa ya mwisho, Mheshimiwa Haonga.

T A A R I F A

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Felister Bura, unaipokea taarifa hiyo?

MHE. FELISTER A. BURA: Mheshimiwa Naibu Spika, hiyo taarifa sipokei, kwa sababu wamefukuzwa kazi, Wakurugenzi wote waliokuwa NSSF kwa ajili ya ubadhirifu, Wakurugenzi kumi wamefukuzwa kazi. Kwa hiyo, hiyo taarifa siwezi kupokea.

Mheshimiwa Naibu Spika, niiombe sasa Serikali yangu, kwamba sasa, tuelekeze muda wetu, tuelekeze nguvu zetu katika kusimamia miradi yenye tija, maeneo yale, ambayo kwa mfano NSSF walikuwa wajenge Ofisi kule Nairobi, Wizara ya Mambo ya Nje wapo, kwa hiyo wawasiliane na NSSF huu mradi uendelee. Kuna mradi wa kuzalisha umeme Mkuranga, mradi huu uendelee kwa sababu Halmashauri ya Mkuranga ipo, NSSF wapo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kuna madeni ya SUMA JKT, Taasisi zilikopa watu binafsi walikopa, tuiombe Serikali wale waliokopa hawajaresha madeni, wachukuliwe hatua.

Mheshimiwa Naibu Spika, sijui ni kengele ya kwanza…

(Hapa kengele ililia kuashiria kuisha kwa muda wa mzungumzaji)