Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018 Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa kuhusu Usimamizi wa Matumizi ya Fedha za Umma katika Serikali za Mitaa kwa Mwaka wa Fedha ulioishia tarehe 30 Juni, 2017

Hon. Ali Salim Khamis

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Mwanakwerekwe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018 Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa kuhusu Usimamizi wa Matumizi ya Fedha za Umma katika Serikali za Mitaa kwa Mwaka wa Fedha ulioishia tarehe 30 Juni, 2017

MHE. ALI SALIM KHAMIS: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, awali ya yote nimshukuru Mwenyezi Mungu siku hii ya leo kuweza kutujalia hapa tukiwa wazima na nikushukuru wewe kunipatia hii fursa kwa ajili ya na mimi kutoa maoni yangu.

Mheshimiwa Naibu Spika, ripoti imeeleza wazi na query zote ambazo zilitokea ni kwa sababu ya Hazina. Hazina ndio ambao wamesababisha query hizi na Mkaguzi ikabidi atoe hoja zake na ninafikiri sote tunakubaliana kwamba na mwisho yametolewa mapendekezo huku kwamba, mfumo wa mahesabu wa Hazina ni shida, kwamba ikiwa leo Halmashauri zinatumia mfumo wa hesabu wa EPICOR lakini Hazina inatumia mfumo wa excel. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli taarifa zimeletwa kutoka Serikalini, lakini bado Mkaguzi aliweka hoja kwa sababu hazikupita katika mfumo rasmi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, na kibaya ni kwamba fedha ambazo zimetoka kwenye Hazina, tuchukue mfano leo Serikali, Serikali ndio inapanga bajeti, wanakaa wanapanga bajeti yao wanakutana na CAG, CAG anafanya approval akishafanya approval inaletwa Bungeni hapa sisi tunapitisha. Sasa ikishapitishwa hapa na Sheria ya Matumizi ikishapitishwa matokeo yake Hazina wanakwenda kubadilisha matumizi ya bajeti ambayo imepitishwa na Bunge pasipo na kumtaarifu CAG. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, kuna exchequer chungu mzima hapa zimeonesha kwamba, kuna fedha zimefanyiwa matumizi ambayo hayakupitishwa na Bunge na wala hakutaarifiwa CAG, jambo ambalo lilikuwa rahisi tu. Serikali walikuwa na uwezo wa kwenda kwa CAG kutokana na bajeti tunayoipeleka hapa kumetokea dharura hii tufanyie marekebisho hapa tupate approval halafu baadaye inaletwa Bungeni kuja kupitishwa pia hili limeshindikana, lakini Hazina wanafanya halafu baadae ndio Mkaguzi anakuja kuona. (Makofi)

MHE. MARIAM N. KISANGI: Taarifa.

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Ali kuna Taarifa. Mheshimiwa Mariam Kisangi.

T A A R I F A

MHE. ALI SALIM KHAMIS: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Mimi kwanza sina shida na adjustment, adjustment ni mambo ya ndani ya utawala, sina shida nayo na wala sijazungumzia habari ya adjustment, mimi nimezungumzia reallocation. Kuna reallocation mbalimbali ambazo zimefanyika na ndiyo maana CAG ali-raise query kwa sababu hazikufata utaratibu kwa mfano... (Makofi)

MHE. KHADIJA NASSIR ALI : Mheshimiwa Naibu Spika, taarifa.

T A A R I F A

MHE. ALI SALIM KHAMIS: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba unitunzie muda wangu kwa hisani yako.

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Ali Salim unaipokea taarifa hiyo?

MHE. ALI SALIM KHAMIS: Mheshimiwa Naibu Soika, siipokei kwa sababu siyo utaratibu huo. Kama ikitokea hivyo Serikali inayo mamlaka ya kufanya reallocation, hilo halina mjadala, lakini kwa sababu bajeti hii ilishapitishwa Bungeni na Serikali inafanya reallocation imtaarifu CAG approve hiyo reallocation yao. Hilo ndilo tatizo, si kwa sababu…

NAIBU WAZIRI WA FEDHA: Mheshimiwa Naibu Spika, taarifa.

T A A R I F A

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Ali Salim unaipokea taarifa hiyo?

MHE. ALI SALIM KHAMIS: Mheshimiwa Naibu Spika, siipokei hiyo taarifa kwa sababu kwanza mimi nataka nimfahamishe Mheshimiwa Naibu Waziri. Yeye alileta taarifa hapa Bungeni, na taarifa hii amesema kwamba bilioni 203 zilikuwa transfered to Zanzibar, lakini Mheshimiwa Kiula amesema fedha zile zilikusanywa Zanzibar na hazikuondoshwa Zanzibar zilitumika pale pale Zanzibar, sasa hapa dakika kumi zilizopita hapa taarifa zinatofautiana. Ndiyo maana nasema kuna shida ya mfumo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa ninaposema tusikilizane tunasema haya kwa maslahi ya nchi yetu, mimi nimezungumzia kuhusu mfumo…

MHE. KABWE Z. R. ZITTO: Mheshimiwa Naibu Spika, taarifa.

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Ali Salim kuna taarifa nyingine.

T A A R I F A

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Ali Salim unaipokea taarifa hiyo?

MHE. ALI SALIM KHAMIS: Mheshimiwa Naibu Spika, taarifa hiyo naipokea na kwa kuongezea tu baada ya query hii ya CAG ya shilingi bilioni 976 Hazina ilipeleka document za clear dola bilioni 1.25 lakini bilioni 975.1 hazijapatiwa majibu mpaka sasa. (Makofi)