Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018 Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa kuhusu Usimamizi wa Matumizi ya Fedha za Umma katika Serikali za Mitaa kwa Mwaka wa Fedha ulioishia tarehe 30 Juni, 2017

Hon. Allan Joseph Kiula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Mashariki

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018 Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa kuhusu Usimamizi wa Matumizi ya Fedha za Umma katika Serikali za Mitaa kwa Mwaka wa Fedha ulioishia tarehe 30 Juni, 2017

MHE. ALLAN J. KIULA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana kwa kupata nafasi ya kuchangia hotuba ya Kamati yetu. Mimi natoka Kamati ya PAC, kwa hiyo, hiyo hotuba ni ya wana-PAC wote. Nilivyoona makofi mengi yanatoka upande wa Upinzani nikawa najiuliza maswali mengi sana lakini kumbe hoja hii ilitakiwa isijadiliwe.

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo lingine ambalo napenda kuweka kwenye record ni kwamba watu wanaotaka ile verification report iletwe, maana ule haukuwa Ukaguzi Maalum ilikuwa ni verification, hili jambo nalo lifahamike. Mheshimiwa Halima Mdee alikuwepo, Mheshimiwa Ester Bulaya alikuwepo na Mheshimiwa Zitto Kabwe tulikuwa naye. Hata dakika ya mwisho Mheshimiwa Zitto Kabwe alivyokuwa anatoka alituachia maswali ya kuuliza kwa ziada kwa maana tulijua ni Mbunge mwenzetu na tuliuliza yale maswali kupata ufafanuzi kwa sababu kila mtu alitaka ajue ufafanuzi wa shilingi 1.5 trilioni imekwenda wapi.

Nataka kuonesha tu kwamba kama alivyosema mwenzangu kwamba wapotoshaji wako humu humu badala ya kuchukua taarifa wanakuja ili waweze kupotosha. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na hayo tunaliomba Bunge liweze kuzingatia Maazimio manne yale ambayo hayajatekelezwa kwenye ripoti iliyopita yaweze kufanyiwa kazi. Vilevile, tunaomba Maazimio ya Kamati..

T A A R I F A

MHE. CECIL D. MWAMBE: Mheshimiwa Naibu Spika, taarifa.

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Allan Kiula kuna taarifa kutoka kwa Mheshimiwa Mwambe.

MHE. ALLAN J. KIULA: Mheshimiwa Naibu Spika, hiyo taarifa siipokei. Namheshimu sana Mheshimiwa Mwambe, lakini nafikiri kwamba anatulisha matango mwitu hapa. Hapa subiri tutoe taarifa na ambazo nyingine tumezinukuu ziko humu, tumefanya quotation, maana yake Kamati haiwezi kuleta quotation za uongo, quotation zilizoko humu ni quotation sahihi na kama unafikiri unaweza kunitoa kwenye reli huwezi. Ni mti mkavu usiochimbwa dawa. (Makofi/Kicheko)

Mheshimiwa Naibu Spika, tukiendelea na uchangiaji wetu kuhusu trilioni 1.5 CAG kwenye verification report yake ameonesha hesabu zake zime-balance, hesabu zake zimewiana mapato na matumizi. Tumeona kwamba, zilipatikana trilioni 26 ukiangalia kwenye ukurasa wa 24 na matumizi kulikuwa na over release ya shilingi bilioni 290 na over release aliyoieleza inasababu yake, BOT walitoa kibali cha over release ya 1.2 trillion Serikali ikatumia bilioni 290 tu. Kwa maana nyingine kungekuwa na jambo ambalo si sahihi wangeweza kutumia pesa zaidi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini si hivyo tu, Serikali imeonesha transparency ya hali ya juu kuruhusu Mfuko Mkuu wa Serikali kuweza kukaguliwa na CAG na kueleza mambo yote yaliyoko mle ni jambo kubwa sana. Si hivyo tu, watu wote tunafahamu kwamba ukaguzi unapofanyika wanaangalia checks and balance na wanatoa hoja kwa hiyo, hoja ni kitu cha kawaida na baada ya ripoti hii kutolewa Machi ndipo ilipokwenda kufanyika verification report. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, walikuwepo na ndio maana nasema wapotoshaji walikuwepo, maelezo yaliyotolewa na CAG…

MBUNGE FULANI: Wapeeee!

MHE. ALLAN J. KIULA:...na mtu anayehojiwa alisema kwamba wakati ripoti inatolewa ziko transaction ambazo zilikuwa hazijawa recorded. Moja ya transaction ni pesa ambazo zinakwenda direct to project, unapopeleka pesa direct to project wakati gani una-recognize? Na watu wengine, wafadhili wetu (development partner), wanapeleka vifaa na nini kwenye project moja kwa moja.

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Kiula kuna Taarifa nyingine. Mheshimiwa Profesa Ndalichako.

T A A R I F A

MHE. ALLAN J. KIULA: Mheshimiwa Naibu Spika, naipokea taarifa hiyo na kwa taarifa za ziada ndio maana niliamua niende kipengele kwa kipengele. Kwa sababu watu wamesoma humu uhasibu, wamesoma kodi, sasa tunataka tuoneshane hapa tumekwenda hatua kwa hatua na twende sambamba. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, na ndio maana tumezungumza suala la pesa ambazo zilikuwa zimekuwa over spent na pesa nyingine za Zanzibar zilikusanywa Zanzibar na zilibaki Zanzibar, kwa hiyo, ile verification report ilikwenda kufanya usuluhishi wa takwimu zote hizo kwa undani wake na CAG mwenyewe akakiri na kwenye Hansard inaonesha na kitabu hiki kinafanya nini, kinaonesha kwamba usuluhisho ulifanyika. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na hayo yapo mambo yalijitokeza na mambo hayo yaliyojitokeza ambayo Kamati ilihoji na tukapata kinachoendelea kule Hazina, tunaipongeza Hazina kwa ku-adapt hii Integrated Financial Management System inafanyika. Lakini pili, pia kuna single treasury account. Hayo mambo yote yalitakiwa yafanyiwe kazi na yakifanyiwa kazi kwa wenzetu wanaojua kuangalia haya mambo utaona kwamba zile hesabu zitakwenda sawa, sasa na taarifa, system zitaongea pamoja na taarifa zitaweza kupatikana. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, suala la kwamba kwa nini kulikuwa na hoja, data zimekwenda kuwa marched hizo data. Kwa hiyo, suala la 1.5 trillion ni suala ambalo limekuwa closed, limeshahitimishwa na CAG alisema suala hilo limehitimishwa, alisema suala hilo limekwisha hitimishwa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na hayo iko hoja ya TIB Development, kuna madeni kule kama tulivyoeleza kwenye taarifa yetu. Tunaomba Serikali suala hilo ilifuatilie na ilifuatilie kwa sababu madeni hayo ukiangalia huku ndani takwimu kwenye ukurasa wa 61 na 62, naomba kunukuu kwa kusoma inasema; “Katika jedwali 24 hapo juu inavyofafanua ni dhahiri kuwa kundi la mikopo inayohesabika kama hasara (loss loans) inachukua karibu asilimia 69. Kwa hiyo, TIB pia ina- operate chini ya required capital. Hasa hilo ni jambo muhimu sana ambalo Bunge tuazimie kwa sababu kwenye maazimio yetu yapo na Serikali iweze kulifuatilia kwa karibu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo lingine ambalo tulilizungumza na tumelipitia tena ni suala la mikopo ya matrekta. Tunaamini kabisa kwamba haijafanyika juhudi kubwa ya kuweza kukusanya madeni hayo kwa sababu, tunaamini madeni hayo yanakusanyika na kama wenzetu wakichukua hatua za makusudi kuweza kufuatilia tunaweza ku-recover hizo pesa ambazo ni pesa za Serikali.

Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana na mchango wangu ndio huo na suala la 1.5 trilion ni chapter closed. Nashukuru sana, asanteni. (Makofi)