Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

Hon. Anatropia Lwehikila Theonest

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

MHE. ANATROPIA L. THEONEST: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushuru, kuna wachumi wa IMF waliwahi kusema, waliandika paper yao moja wakijibu walikuwa wanaulizwa maswali ni fedha kiasi gani nchi inahitaji kukopa; anasema how much a debt is sustainable? Maana tumekuwa na maeneo mengi kuwa deni letu ni himilifu ni toshelevu sasa katika hiyo paper yao ambayo waliandika walijibu kwamba kwa kiswahili wakisema; they don’t know kwamba hawajui ni hela kiasi gani au ni debt kiasi gani ya Taifa ambayo ni sustainable na wakenda mbali zaidi wasema market signals don’t work as should; kwamba zile sign za soko some time hazipo predictable nadhani na hiyo nimwambie Mheshimiwa Dkt. Mpango sometimes market signal haziko predictable.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunaweza kuwa tunajiamini kwamba deni letu ni himilivu, deni la Taifa linalipika hana anayebisha kwa sababu tunaona uchumi unakua kwa mujibu wa takwimu zetu kwa maana ya GDP bado ina tolerate mkopo tuliao nao, lakini swali tunajiuliza kwa nini hii mikopo inakuwa kwa haraka. Sikatai kwamba tunakopa fedha nyingi kwa ajili ya kenudesha miradi yetu mikubwa inayoendelea lakini ushauri wangu nitakao utoa sasa tuangalie hizo fedha tunazozikopa katika miradi tunayoweka, je, itaweza kutupa fedha kwa wakati mfupi? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunakopa kwa ajili ya kuwekeza kwenye miradi ambayo ni ya muda mrefu hatuna uhakika kama tunaweza kufuna haraka haraka hiyo hiyo naleta kwenye mradi mkubwa tunaouendesha kwenye SGR. Huo mradi mkubwa tunaoendesha ambao sisi humu Bungeni tumekuwa tukipiga kelele kwa ajili ya kufufua mradi mkubwa wa chuma wa Liganga na Mchuchuma nimepitia kwenye kitabu chako mmesema mnakamilisha taarifa za awali, nanihajui kwamba kukamilika kwa mradi mkubwa chuma ndio ungesaidia pakubwa katika mradi mkubwa wa SGR, nani anabisha katika hilo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, fedha tunazozidi kukopa kwa wahisani au wafadhili tukaiwekeza kwenye kujenga SGR tungeweza kuwekeza kidogo kama tungekuwa tunazalisha sisi chuma hapa nchini. Lakini kama haitoshi tungeweza kupata faida zaidi hata fedha kigeni kwa kuuza chuma lakini badala yake mradi ambao umekuwa kipaumbele 2015/2016 leo inapewa that half a page ndio inazungumziwa na dhani Waziri atupe status leo kuna mwekezaji alijitokeza nadhani anaitwa Szechuan Onda akija na terms zake atuambie amefikia wapi as far as concern kuwekeza katika huu mradi ambao kimsingi ndio mradi wenye kielelezo na unapaswa kuwa kipaumbe kwa nchi yetu kwa nchi yetu kama tunamaanisha tunakata uchumi ukue.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninarudia tena kusema tusijamini sana kusema kama deni letu ni himilivu kama tunaenda kuwekeza katika vitu ambavyo havitaweza kupandisha GDP yetu haraka sana ikiwa ni pamoja na mazao ambayo tutazalisha au uchumi tutakaoweza kuu-nature ukaweza ku-support export ndio itasaidia deni letu lizidi kuwa himilivu. Hao Wakenya leo ambao wanakaribia ku-default na wao walikuwa najinasibu kama tunavyoongea leo kwamba deni lao lilikuwa himilivu na kama haitoshi GDP ya Kenya iko juu kuliko ya kwetu, lakini nini kinatokea ni lazima tujiangalie wanasema ukitaka kuruka ni lazima uagane na nyonga, kwa hiyo sasa tungalie vipaumbele vyetu vya kiuchumi in relation to deni la Taifa hiyo ni ya kwanza, lakini ya pili, nina muda mchache, Serikali...

(Hapa kengele ililia kuashiria kuisha kwa muda wa Mzungumzmji)