Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

Hon. Richard Phillip Mbogo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nsimbo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

MHE. RICHARD P. MBOGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa nafasi, napenda niipongeze Serikali na Waziri pamoja na timu yake nzima kwa namna wameweza kuandaa mpango huu na niseme tu katika changamoto ambazo amezieleza kutokana na utekelezeji wa mpango amekwa wazi na sisi kama Wabunge tunahitaji kumsaidia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ili uweze kutekeleza mpango au bajeti tunaangalia mapato na matumizi, na katika upande wa mapato ili kuweza kuongeza mapato maana yake utaongeza bei au rate, utaongeza ushalishaji au utaongeza vyanzo vipya vya mapato.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa naomba nianze na masuala ya kodi, kwanza niombe Serikali au Wizara husika ule muda wa makampuni au taasisi mbalimbali kupitia malimbikizo ya madeni ya riba kwenye kodi badala ya tarehe 30 Novemba muuongeze na watembelee makampuni mbalimbali ili watu waitikie na walipe malimbikizo ya kodi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tuna suala la kuongeza bei kwenye maeneo mbalimbali mara nyingi mwezi Juni kwenye Finance Bill ndio tunaletewa maeneo ya mapendekezo. Lakini ningependeza kipindi hiki cha mpango hebu Waziri awe anatupa maeneo anayotarajia kuongeza ili tuwe na nafasi nzuri ya kuweza kushauri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ningeomba kwa namna ya pekee kabisa tuumie Watanzania lakini tupate huduma, naomba tuongezee shilingi 50 kwenye kila lita ya mafuta ili iende kwenye maji. Kwa sababu gani napendekeza, miradi ya maji ikishatengenezwa maintenance inaachiwa kwenye jumuiya ya watumia maji watabaki wana-maintain wenyewe, tofauti na Road Fund kila mwaka zinatoka fedha za ukarabati lakini mradi wa maji ikisha tengenezwa COWOSO ndio inakuwa na wajibu wa ku-maintain kwa hiyo kama Serikali tukiruhusu hii shilingi 50 tukaongeza ikaenda kwenye maji itasaidia kwenye miradi ya maji ambayo ndio changamoto kubwa ya wananchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tulifanya mabadiliko sheria ya fedha produce cess tukashusha kutoka asilimia tano kwenda asilimia tatu, lakini kimsingi kwenye mazao ya biashara kama tumbaku hatujamnufaisha mkulima kwa hiyo hii tumenufaisha mnunuzi. Kwa hiyo niombe Serikali muone namna gani vya ku-review hii punguzo kutoka asilimia tano kwenda asilimia tatu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine ni kuhusu sevice levy. Halmashauri nyingi hazipati service levy kutoka kwa wa wakandarasi wanaotengeneza barabara ambao wapo chni TARURA na chini ya TANROADS kwa hiyo mapato kwenye halmashuri hayakuwa hayafikii malengo vilevile kampuni za simu ambazo zimeweka minara sehemu mbalimbali nchini bado Halmshauri zetu hazipati mapato upande ya service levy. Kwa hiyo tunaomba kama Serikali muweze kuangalia maeneo hayo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, awamu hii ya tano tunapongeza sana kwamba tutakuwa na uchumi upande wa viwanda, lakini kuna viwanda hapa Tanzania kuna viwanda vinalishwa kwa 90%; 75% kutoka nje ya nchi. sasa kama Serikali nini mkakati kwa mfano kwenye ngano Bakhresa 95% anaingiza toka nje, sasa tuna mkakati upi wa kuweza kuwezesha akapata malighafi hizi toka Tanzania ambapo tutatengeneza ajira humu ndani tutakusanya mapato ya kodi mbalimbali, sasa nini kifanyike tutaomba Serikali ingalie na upande hata wa mafuta 75% tunaingiza kutoka nje. Kwa hiyo, dola ambazo tunalipa kwenda nje ni nyingi kuliko tunazoziingiza kutokana na export, kwa hiyo balance payment inakuwa ni negative, kwa hiyo hii inatuathiri uchumi wetu.

Kwa hiyo, tunaomba pia kwenye upande wa kilimo wananchi wengi wanatumia jembe la mkono. Sasa ni lini tutawatoa hii benki yetu ambayo tumeanzisha kwa ajili ya kuendeleza kilimo inaenda kusaidia namna gani maeneo hayo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niende kwenye upande wa Balozi zetu, nchi nyingi duniani tuna Balozi nyingi lakini ni jinsi gani kama kama Serikali tunazitumia hizi Balozi kwenye kupata wawekezaji na kuangalia fursa zilizopo kwenye nchi mbalimbali duniani. Tumeona Balozi nyingi hatujapata taarifa yake kamili lakini hatuzitumii vizuri na hata Balozi zingine zinahitaji taarifa toka huku nchi hazibiwi kwa wakati miezi miwili/miezi mitatu kwa hiyo tutumie vizuri hizi Balozi tuweze kukuza uchumi wetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti,kuna suala la sekta binafsi na sekta isiyo rasmi, mwaka juzi ilipitishwa na mwaka jana wakati wa bajeti ilitoa taarifa kwamba watapewa vitambulisho watambulike na waingie kwenye kuchangia kwa maana kwamba walipe kodi, sasa changamoto Waziri ameileza kwenye kitabu chake kwamba imekuwa ni ngumu, sidhani kama sisi wanadamu au Serikali ikiamua jambo linaweza likashindikana.

Kwa hiyo, tukiweka vitambulisho na maeneo husika na hata wale wanaotembea kama vitambulisho wataweza pia kuhusishwa vyema nakuweza kulipa kodi na staiki zingine zote za Serikali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna masuala ya mashirika ya Serikali ambapo yana zaidi ya 50% na mengine chini 50%. Kuna kampuni kama TTCL inahitaji udhama wa concession loan, inahitaji Serikali iweze kusaidia kuwekeza. Mchango karibuni na Serikali dora 231,000 sasa ni lini Serikali itaoa fedha kwa Kampuni ya TTCL ili ingie kwenye ushindani, ipate faida na Serikali ipate gawio kama ambalo ndilo kusudio. Na ATCL tunashukuru shirika limefufuliwa vizuri lakini ATCL inahitaji jicho zaidi, ipate discount kwenye government bill kwa mfano land fees, mambo ya navigation wapunguziwe kama nation flag ili waweze kukua zaidi na zaidi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna suala la utalii kama ni Tanzania tuna vivutio vingi je, ni lini mchango wa utalii utaongezeka kwa kiasi kikubwa katika kukuza pato la Taifa. Tunaona nchi za wenzetu wanapata mapato mengi kwenye utalii lakini vivutio ni chache sana. Sasa tuombe Wizara ya Maliasili ya na Utalii kwa kushirikiana kwa ujumla kama kuna msaada wa Wabunge, msaada wa maeneo mbalimbali watuoneshe mkakati utalii utaenda kuongeza mapato kwa kiasi kikubwa na nchi ambazo watalii wengi wanapatikana tufanye mawasiliano...

(Hapa kengele ililia kuashiria kuisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MHE. RICHARD P. MBOGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.