Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

Hon. Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

MHE. HUSSEIN M. BASHE: Mheshimiwa Mwenyekiti, kama hatutaanzisha Price Stabilisation Fund, hatuwezi kupiga hatua kama Taifa. Kwa sababu wakulima ambao ndiyo asilimia 70 tunatarajia auze mahindi yake Nzega akanunue bati. Leo mahindi ni Sh.18,000, Sh.20,000, bati bandari moja imeongezeka kwa kipindi cha miaka mitatu almost mara mbili. Kwa taarifa mazao ya kilimo yanashuka bei kwa zaidi ya 20%; ni taarifa za NBS na za Wizara ya Fedha. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nitolee mfano zao la korosho, hatuna uwezo wa ku-control bei ya soko dunia sisi, lakini sisi tuna uwezo wa ku-control volumes. Ili tu-control volumes ni lazima tuwape incentives wakulima. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo mfuko wa mahindi wa kilo mbili ni Sh.12,000, nataka niwape hizi takwimu. Mkulima ninayemuongelea ni huyu anayetumia mbegu ya hybrid ambayo kwenye heka moja atapata magunia 20 ambayo yatampatia kilo 2,000. Sasa ili alime heka moja atatumia tractor kwa Sh.45,000, tuandike, atafanya harrow kwa Sh.40,000, atatumia mbolea ya kupandia kwa Sh.65,000, atapalilia kwa Sh.25,000 mara mbili Sh.50,000, atatumia mbolea ya kukuzia kwa Sh.70,000, atanunua mbegu ya hybrid kilo moja Sh.6,000 kwenye heka moja atatumia mifuko nane ambayo ni Sh.48,000. Mkulima huyu ataweka ulinzi, atavuna, atapakia, ataweka dawa, ukichukua gharama yake ni karibu Sh.650,000. Gawa kwa huyo amepata at the optimal, best production, tani mbili ni Sh.325, bei leo kilo moja Sh.150. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa heshima, tuchukulie zao la korosho, tumbaku sisi imeanguka leo ni mwaka wa pili wa tatu. Nataka nitoe ushauri na ni ushauri tu, it is pure administrative. Leo Mheshimiwa Rais kachukua hatua kasema korosho inunuliwe kwa Sh.3,000, ushauri wangu kwa heshima Mheshimiwa Dkt. Mpango wafanyabisahara wamesema watanunua kwa Sh.2,700 waagizeni nunueni kwa Sh.3,000 sisi kama Serikali tuta-subsidise hiyo Sh.300 mnayopata hasara ili mkulima asipate hasara. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hatuwezi kutoka, this is the practise all over the world. Lazima tutengeneze a buffer plan kwa wakulima wetu. Tusipofanya namna hii madhara wanayoyapata wakulima kitakachotokea demand na purchasing power ya wakulima itashuka, ndio asilimia 60.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wewe unatoka Dodoma. Zao la zabibu, mimi nitampa Kaka yangu Mheshimiwa Dkt. Mpango World Economic Forum wamefanya Competitive Index Report ya dunia wametu-rank sisi 100. Hii siyo World Bank Report ambayo imetu-rank 140 ambayo tumeporomoka kwa digit 4. Hawa watu wa World Economic Forum wamefanya survey kwa ma-CEO wa Kitanzania. Ma-CEO wa Kitanzania na wafanyabiashara wa Kitanzania wametaja mambo matano ambayo ni matatizo katika nchi yetu kwa ajili ya kufanya biashara. La kwanza wamesema access to financing, la pili right to own properties, la tatu tax rate, la nne tax regulation.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi nachoshangaa ni jambo moja, Serikali imechukua hatua nzuri ya kutengeneza document ya blue print, nachojiuliza kwa nini wasilete sheria na kwenye document ya mpango kungekuwa na chapter inayoongelea tax reforms tutakazozifanya kutokana na document ya blue print. Nilitarajia nione hili kwamba tutafanya mabadiliko ya kodi na regulations katika mwaka huu wa 2019/2020 katika maeneo haya baada ya kuandaa document ya blue print, hakuna. Kinachotokea ni nini? Nashindwa kuelewa kwa nini tunaandaa kwa haraka Muswada wa Vyama vya Siasa? Kwa nini tusilete Sheria za Kodi ambazo ni bottleneck to the economy, kwa nini? What is our priority? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi namuonea huruma sana Mheshimiwa Waziri wa Fedha na nataka niwaambie Waheshimiwa Wabunge, mimi naona kuna tatizo sana Serikalini Mheshimiwa Waziri Mkuu. It is either Mawaziri na wataalam wameamua kutokufikiri ama wameamua kutegeana, hakuna kitu kingine. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninachojiuliza tumbaku inaporomoka, the biggest market ya tumbaku sasa hivi ingekuwa Middle East, what are we doing as a country? Far East, what are we doing as a country? Yaani husikii, tunaambiwa tu tupunguze production, tumbaku imekuwa shida. Leo korosho tunaenda kwenye crisis. Nataka nishauri, sisi hatuna control na bei za dunia, tuna control na volumes za ndani na ili tuweze ku-expand volume lazima tujenge incentives. (Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa mzungumzaji)

Mheshimiwa Mwenyekiti, namalizia tu. Naomba Wizara ya Fedha njooni na chapter kwenye mpango wa Februari wa namna gani mnaokoa kilimo katika nchi hii kwa kuanzisha price stabilisation, namna gani mnafanya tax reforms ili biashara ziweze kufanyika katika nchi yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.