Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo ya Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

Hon. Athumani Almas Maige

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo ya Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

MHE. ALMAS A. MAIGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, na mimi nakushukuru sana kuniruhusu na mimi nichangie hotuba hii ya ndugu yangu Mheshimiwa Dkt. Mpango kuhusu Mapendekezo wa Taifa na Mwongozo wa Maandalizi wa Bajeti.
Mheshimiwa Mwenyekiti, siwezi kuanza kutoa maoni yangu kabla ya kusema ukweli wa utendaji wa Serikali ya Awamu ya Tano chini ya Mheshimiwa Rais Magufuli, mimi naamini sasa masia nyumbani haaminiki, upande wa pili kule wanasema maneno mabaya ambayo hatuelewi kuhusu utendaji mzuri wa Serikali ya Awamu ya Tano. Sisi huku tunapongeza mambo mazuri yaliyofanywa na Serikali ya Awamu ya Tano lakini sio sisi tu, hata nchi za nje wanapa taabu kujua lugha gani watumie neno gani watumie wamesema magufulification na sisi tunasema kazi tu maana yake kazi nzuri imefanyika. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nami naomba nitaje mafanikio yaliyotajwa hapa kweye kitabu cha Mheshimiwa Mpango pamoja na kukusifia wewe na taaluma yako wewe na dada yangu Kijaji, Naibu Waziri lakini pia watendaji wa kazi ya Wizara yako ambao wameleta mpango mzuri sana katika mapendekezo yenu ya maendeleo ya huu mwaka moja na mpango wa bajeti.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nianze na ukuwaji wa uchumi. Uchumi wa Tanzania hakuwi wenyewe unakuzwa ina maana kuna watu wanafanya kazi ili uchumi wetu ukuwe, lakini mapato ya kodi za pamoja na mapato yasiyokuwa ya kodi yamekuwa sana kulinganisha miaka mitatu iliyopita, lakini vilevile ulipaji wa madeni na mimi naomba niseme hapa ni declaire interest, Wizara hii imenilipa madeni kama mkandarasi, wakandarasi walipolipwa na mimi naipongeza Wizara hiyo kwa sababu nilikuwa mtu ambaye niliyolipwa madeni hayo ya wakandarasi, lakini pia barabara pia mimi ni moja watu walio benefit na barabara inayojengwa kutoka hapa kwenda Tabora imebakia karibu kilometa 65 tu ili barabara yote iliyojengwa pale ikamilike tuwe tunatoka hapa kwenda tabora kwa muda masaa mawili/matatu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna reli ya standard gauge sitaki kuisema sana imetajwa mpaka imekuwa tunu ya Tanzania, lakini pia kuboresha shirika la ndege, mimi niseme nini. Kila mtu mwenye macho ahambiwi tanzama ndege zote zile tangu lini sisi tungeweza kupanda dream line ndani hapa hapa ndani lakini kila mtu ana panda dream line kwa faida kubwa tunaipata, lakini viwanja vya ndege pamoja na kiwanja cha Tabora kimekarabatiwa vizuri, lakini bandari imejengwa vizuri, imefungwa mitambo ya kuona vitu vya kuona mitambo ya kuona vitu vinavyopita kwenye makontena yale na kazi kubwa imefanyika ya kukamata watu wanaojaribu kuiba nyara zetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kilimo mimi sisemi, kazi kubwa ya kilimo imefanyika lakini hapa nitakuwa na mapendekezo yangu baadae, lakini huduma ya afya katika Jimbo langu pamoja na zile vituo vya afya 295 vimetolewa mimi nimepata kituo kimoja ambacho kimejengwa na kila kitu sasa kipo ndani kazi ndogo iliyobakia tunaomba gari la wagonjwa ili tuweze kuwakimbiza wale wangonjwa wanaozidiwa kwenda Hospitali ya Rufaa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu nishati tumesikia miradi mipya ya Kinyerezi, miradi mpya ya umeme na umeme wa REA ambao sasa utaleta maendeleo vijijini. Lakini huduma ya maji sisi upande wa Tabora tumepata mpaka maji kutoka Ziwa Victoria mradi mkubwa na mabomba yamekaribia kabisa jimboni kwangu na kwenda Tabora Mjini, lakini pia kuamasisha makao makuu kutoka Dar es Salaam kuja hapa lilikuwa jambo lisilowezekana mbona hamshangili? Mbona hamuoneni ukweli huo kwamba tupo hapa Dodoma pamoja na kila mtu isipokuwa Mheshimiwa Rais, Makamu wa Rais yupo hapa, Waziri Mkuu yupo hapa, Mawaziri wote wako hapa. Jambo limekaa miaka 43 karibu hawashangai upande wa pili na hili pia hamlioni wakati mnajua tupo hapa? Lakini pia mambo ya madini mwaka huu tumepata bilioni 301 faida au mapato kutokana na madini, ilikuwaje miaka iliyopita hayakupatikana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nina maoni yangu kuhusu elimu lakini tunasoma elimu ya msingi bure jambo hili haliwezekani na halikuwezekana miaka iliyopita tunatumia zaidi ya bilioni 20 kwa mwezi kulipia watoto wetu waende shule, lakini pia usafiri wa majini, meli zimejengwa pamoja na ajali iliyotokea tunaomba Mungu awarehemu marehemu waliofariki.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya hapo sasa ni change mimi mambo gani ingefaa Wizara yako Mheshimiwa Mpango ifikirie mambo haya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali itafute mahusiano kati ya sekta binafsi na Serikali; kuiwezesha sekta binafsi Mheshimiwa Dkt. Mpango itazalisha na kuuza uchumi wa nchi hii, duniani kote Tanzania tu ndio tunasema kwamba labda Serikali peke yake itafanya, lakini sekta binafsi ina mchango mkubwa sana katika kukuza uchumi.

Kwa hiyo, mimi napendekeza Serikali itafute jinsi ya ku-engage private sector tuweze kuitumia ikuze uchumi na kuongeza ajira. Lakini pia Serikali itoe kipaumbele kwa katika kurasimisha baadhi ya kazi, shughuli nyingi hapa Tanzania za wananchi hazijawa rasmi na hiyo sekta na hiyo isiyo rasmi hailipi kodi, lakini inapata mgao mkubwa wa maendeleo wa fedha za maendeleo lakini kama ingerasimishwa basi tungeweza kupata mapato makubwa kuongeza kwenye kapu la mapato ya Serikali pamoja na kuwatengea vijana na akinamama katika Halmashauri zetu lakini hela hizo haziendi, kwa mfano katika Halmashauri ya Uyui hela zote zaidi ya milioni 400; milioni 500 zilizogaiwa hazifiki milioni 46 kwa mwaka mzima. Hili ni tatizo. Kwa hiyo, Serikali itafute njia ya kuweza kurasimisha upatikanaji wa hela za wale akina mama na vijana huko vijiji ili waweze kuleta maendeleo na kujibudu huko.

Mheshimiwa Mwenyeikiti, lakini pia Serikali ifanye kazi ya kurejesha elimu ya ufundi hapa nchini na hili ni jambo la muhimu kabisa, viwanda haviwezi kwenda bila mafundi sadifu na mafundi mchundo, ninamaanisha artisans na full technician certificate people, bila hiyo viwanda haviwezi kwenda hali hii ilikuwepo miaka iliyopita ikatokea bahati mbaya sana elimu ya ufundi imedhalilishwa, imeteremshwa mimi nafikiri ni muhimu sasa kila shule za kata ipewe somo moja la ufundi labda umeme, labda ujenzi wa mabomba na kadhalika ili tuwe na mafundi kule vijijini. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyetiki, mwisho jambo muhimu sana ni kuweza kutumia kukuza uchumi wetu ni kutumia taasisi za majeshi, katika nchi zingine kwa mfano Vietnam na sio Vietnam peke yake kwa sehemu kubwa ya maendeleo katika nchi imetumika majeshini aidha katika kufanya research au kuzalisha mali ambao ilikuza uchumi, sisi tuna mashirika matatu hapa makubwa sana. Shirika la Mzinga pale Morogoro lingeweza kufanya kazi kubwa sana ya kukuza uchumi wakiwezeshwa, lakini pale Kibaha kuna Shirika la Nyumbu ambapo wanayo Research and Development Unit (R&D) wangeweza kufanya kazi kubwa sana za kiuchumi na kuwa chanzo cha kukuza uchumi na kuongeza ajira. Lakini mashirika yale mawili yametelekezwa na yanahangaika peke yake na yanatumia bajeti ya Ngome ambayo hakuna hela, Serikali ichukue jukumu muhimu la kuwezesha maeneo haya mawili tunaweza kukuza uchumi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Dkt. Mpango lakini lipo Shirika la SUMA JKT ambayo pia unaweza kuwa uzalishaji mkubwa sana na jua chakula kina-stabilize mfumo wa bei, Magereza wakiwezeshwa wanaweza kulima chakula cha kutosha kula watu wote lakini pia wanaweza kuleta chakula cha kutosha kuziba nafasi ya mfumuko wa bei.

Mheshimiwa Mwenyekit, mimi nafikiri nilitaka kusema hayo, lakini la mwisho kabisa niongelee kuhusu lugha ya kufindishia. Elimu ni ufunguo wa kila kitu, hakuna maendeleo bila elimu, lakini elimu yetu inawapa watoto mzigo kweli kweli. Watoto wanasoma darasa la kwanza mpaka la saba kwa kiswahili na mwaka huu watoto wamefeli sana kiingereza halafu wakifika darasa la saba wakienda form one wana switch frequency, wanasoma kiingereza kwanza wanapata tabu yakuelewa kiingeraza, lakini wanapata tabu ya kuelewa masoma kuna tatizo gani hapa la watu wasisome kiswahili, kwanini watoto wetu wasome kiswahili zipo nchi nyingi wanasoma lugha za kwao na hata nikizitaja Ufaransa, Uingereza, Marekani, Ujerumani Urusi, China kote wanasoma lugha zao na watoto wanaelewa, mimi nilikuwa kwenye mahafali mbili kwenye shule za sekondari jimboni kwangu.

Mheshimiwa Mwenyekiti naomba kuunga hoja mkono hii asante sana.