Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo ya Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

Hon. Desderius John Mipata

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkasi Kusini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo ya Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

MHE. DESDERIUS J. MIPATA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kwa kupata nafasi, na nimshukuru vilevile Mwenyezi Mungu kwa kunijalia uzima, kama nitapata nafasi nitaweza kuchangia maeneo matatu, eneo la kilimo, afya na elimu na kama nafasi itaruhusu na mambo yanayohusu barabara.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niungane na wenzangu wanaotoa pongezi nyingi sana kwa hotuba nzuri ya Mheshimiwa Mpango na utendaji mzuri sana wa Serikali ya Awamu ya Tano na hapana mashaka juu ya utendaji huu, umejidhihirisha juu ya mambo mengi ambayo ushahidi wake nitauelezea baadae.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niende moja kwa moja kwenye kilimo. Nakubaliana sana na taarifa ya Mwenyekiti wa Kamati ya Bajeti juu ya mapendekezo anayotoa juu ya kuboresha kililimo katika kitabu chake ukurasa wa 18. Kwamba ili tuweze kwenda lazima Serikali itenge fedha za kutosha katika kuhudumia kilimo na hasa ukiona mwelekeo wetu ni mwelekeo wa viwanda, sasa huwezi kukwepa na historia inatuambia nchi zote duniani zilizofanya vizuri kwenye viwanda zilianza kuboresha kilimo, kwa hiyo hatukwepi hapo. Na kwa mtazamo wangu naona ni kama tunaenda hatujazingatia sana suala la kuimarisha kilimo. Katika kuimarisha kilimo ni lazima upatikanaji wa pembejeo uwe wa uhakika na kwa wakati na kwa bei nafuu zinazokuwa affordable kwa wakulima, zinazowezekana kununulika na uchumi ulipo sasa kwa wakulima.

Lakini pia kuendeleza vituo vya utafiti ili viweze kuleta matokeo bora kwa mbegu na mazao tunayofanya. Lakini vile vile kuhakikisha kwamba upatikanaji wa nyenzo za uvuvi zinapatikana bora na kwa bei nafuu na kuimarisha masoko ya kilimo na ufugaji. Mambo haya kama yatazingatiwa, kilimo kitakwenda. Lakini ninavyoona ni kama kilimo kwetu hapa Tanzania tunaacha sekta binafsi ikiongoze, ukiwaachia sekta binafsi kwa mawazo yangu mimi, nashauri Serikali si sawa ni hatari kwa usalama wa chakula lakini pia kwa usalama wan chi yetu kwa sababu kilimo kinaajiri Watanzania wengi, na ukiachwa kiendeshwe kwa matumaini ya kusema sekta binafsi ndio itakuwa inawawezesha pembejeo na masoko unafanya makosa makubwa. Tuje na mkakati utakaowezesha kubuni mbinu za kuwezesha upatikanaji wa haya niliyoyasema kwa wakulima, kwa uhakika na kwa wakati, lakini vilevile masoko yao. Na Bodi ya Nafaka na Mazao Mchanganyiko ni chombo ambacho kikitumiwa vizuri na kikiwezeshwa, kinaweza kikaleta neema ya wakulima. Kikatafuta masoko ya ndani ya nchi nan je ya nchi nab ado mambo yakaenda vizuri kwenye kilimo. Kwa hiyo ndugu zangu naomba Mheshimiwa Waziri, uhakikishe kwamba suala la kilimo inakuwa kipaumbele cha kwanza. (Makofi)

La pili, katika kilimo kuna uvuvi. Suala la uvuvi linavyoendeshwa na wavuvi wanaonekana kama ni balaa sasa hivi, Ziwa Tanganyika sasa hivi kuna taharuki kubwa na wananchi hawavui wamekaa na maisha ya kule nature yao wanategemea ziwa. Ukishaweka utaratibu ambao huwawezeshi kuingia Ziwani maana yake wanakufa kabisa. Naomba kwa kutumia hotuba hii, Waziri anaehusika ajaribu kuangalia vijana wake aliowatuma kule, wanachokifanya sio hicho. Kwa sababu mtu anapokiuka utaratibu lazima watu wapige kelele wanajua haki zao, kwa hiyo nawaomba Serikali itupie macho kule. (Makofi)

Sasa hivi wavuvi wanahamia ng’ambo ya DRC na kwa maana hiyo Halmashauri yetu ya Wilaya ya Nkasi leo hazina mapato sasa kwa mwezi huu wa Oktoba na wananchi wana taharuki kubwa na wananchi wa maeneo hayo hawapati hata kitoweo cha samaki. Kwa hiyo, itakuwa shida kubwa, naomba Serikali iliangalie hili na ifuatilie kwa haraka sana hali ni mbaya sasa hivi. (Makofi)

Suala lingine ni suala la Afya, ndugu zangu suala la afya nchi nzima tumeona juhudi kubwa sana itanayofanywa na Serikali yetu hasa kwenye vituo vya afya na mimi kwenye Jimbo langu nimeweza kupata Kituo cha Pembe na sehemu zote. Lakini niseme tu juhudi hii ni upendo wa Serikali kuonesha kwamba ikiwa kipaumble ni afya maana yake watu watakuwa na afya na wataweza kuendeleza shughuli zingine. Niombe haya maboma yote ambayo yapo kupitia mpango huu ukajibu ukaweza kuyaezeka na kukamilisha, nchi nzima kuna zahanati nyingi sana zimejengwa, kuna vituo vya afya vingi tu, sasa kupitia mpango huu tuone kama vinaendelezwa na kujengwa. Kwenye Jimbo langu tu peke yake kuna zahanati zaidi ya 12 zilizojengwa na wananchi ziko katika hatua mbalimbali, wananchi hawaja anza kupata huduma. Kwa hiyo na tumewahamasisha na wakahamasika, sasa itakuwa tunapoenda kwenye uchaguzi kipindi kijacho itakuwa kazi kubwa sana kuelezea haya. Lakini vilevile vituo vya afya viko. Vingi tu nchi nzima kwenye Jimbo langu tu viko zaidi ya vinne Kasu, Kate, Namansi kule, Mbinde, Wampembe, Kala bado vinatakiwa visaidiwe na wananchi wa Kala wana shida kubwa zaidi.