Parliament of Tanzania

Questions By: Hon. Salum Mwinyi Rehani

Supplementary Questions
MHE. SALUM MWINYI REHANI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri kuhusiana na bei ya umeme bado Shirika la Umeme la Zanzibar (ZECO) halijapunguza bei ya umeme kitu ambacho kinawanyima fursa wananchi wa Zanzibar kuweza kutumia nishati hii au rasilimali hii kwa ukubwa zaidi kuliko hali inavyokuweko sasa hivi. Kwa sababu wengine wanashindwa kuunga umeme kutokana na hali ya bei. Je, Serikali ina mpango gani wa kuweza kukaa na ZECO ili kuona na kwamba na wao viwango vile vinaweza kupungua na kuwanufaisha wananchi wote kwa bei ya chini zaidi kama ilivyokuwa huku Tanzania Bara.
MHE. SALUM MWINYI REHANI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, pamoja na majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri, naomba nimuulize swali moja la nyongeza.
Kwa Zanzibar suala hili limekuwa na manung‟uniko sana na hasa kwa kutokuweko watendaji katika hizi taasisi na hili limetokana kwamba wanafunzi wengi wanaopata huduma kupitia TCU, NACTE na NECTA wamekuwa wanahisi hakuna uwiano na hakuna haki inayotendeka kwa vile hakuna watu ambao wanaohusiana wanaotoka upande ule kule. Je, Waziri au Wizara ina mpango gani wa kuweza kupata angalau maana yake watu wawili, watatu kuweza kuingia katika taasisi hizi ili kuepusha manung‟uniko ya kila siku hasa yanayohusiana na masuala ya vyeti na mengineyo ambao wanataka kujiunga katika vyuo mbalimbali vya huku Tanzania Bara?
MHE. SALUM MWINYI REHANI: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi. Nataka kumwuliza Mheshimiwa Waziri; kwa vile utalii ni moja kati ya tegemeo kubwa la uchumi wa nchi yetu. Je, Serikali ina mpango gani wa kuwajengea uwezo Mabalozi hasa walioko nchi mbalimbali za Latin America na America kuwa na uwezo wa kuweza kufanya ushawishi na kuweza kuunganisha Mashirika ya Kitalii yaliyoko katika nchi hasa za Ujerumani na Ufaransa kuweza kuja katika nchi zetu hizi na kuwa na mfano wa nchi ambazo wameweza kufanikiwa sana tukilinganisha nchi za Mauritius na nchi nyinginezo za Mashariki ya mbali ambazo zimefanikiwa sana katika suala hili la utalii?
MHE. SALUM MWINYI REHANI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri, lakini tulikuwa tunataka kujua mkakati gani Wizara inayo wa kuwafanya Wachina hawa kuhamisha teknolojia na viwanda ambavyo vinazalisha bidhaa mbalimbali kutoka kwao kule kuanzishwa katika nchi yetu?
MHE. SALUM MWINYI REHANI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru, naomba niulize swali moja la nyongeza, kama ifuatavyo:-
Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, lakini bado wamiliki wa vyombo hivi hawajawapa mikataba waendesha bajaji na bodaboda, matokeo yake wanakubaliana kwa maneno kwamba baada ya mwaka mmoja chombo hiki kitakuwa chako kwa kiasi fulani cha fedha lakini ikifika miezi saba au nane anamnyang’anya kile chombo na kumpa mtu mwingine.
Je, Serikali iko tayari kusimamia zoezi la kukabidhiwa mikataba waendesha pikipiki na wakamatwe waendesha pikipiki waulizwe mkataba aliokupa mwajiri wako uko wapi ili kuwashinikiza wamiliki hawa kutekeleza hii sheria?
MHE. SALUM MWINYI REHANI: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri ningependa kumuuliza swali moja la nyongeza.
Kwanza, tunataka tupate ripoti na siyo cheti kwa sababu cheti kinakuwa ni uthibitisho tu, lakini ripoti ndiyo kitu ambacho tunaweza kuona athari iliyopo au hakuna athari.
Pili, nilitaka kuelewa kwamba bwawa lile liko maeneo ya upande wa Morogoro, lakini wananchi wa pale wanategemea sana kuzalisha pamoja na mazao ya miwa na mpunga lakini na mazao mengine mbalimbali ambayo yako katika eneo lile.
Je, wasiwasi wangu uliokuweko maporomoko ya maji na mwelekeo wa maji ambayo yanashuka katika lile bwawa hayatoweza kuathiri mmomonyoko na uharibu wa lile bwawa pengine labda ikasaidia kuingia na kufanya contamination ya maji ambayo yatakuwa yanaingia katika maeneo yale.
Je, Serikali iko tayari kuweka utaratibu mzuri wa kilimo ambacho kitakuwa hakitumii kemikali ili kuepukana na athari za kikemikali katika maji yale ambayo wanatumia binadamu na kilimo?
MHE. SALUM MWINYI REHANI: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru. Kwa kuwa moja ya vitu ambavyo nchi hii inatakiwa kuwa navyo ni iwe inaelewa mambo mengi yanayohusiana na hali ya hewa kwa sababu tuna vifaa ambavyo vimeunganishwa na satellite duniani lakini kinachosikitisha ni kwamba mara nyingi matukio mengi ambayo yanatakiwa yatolewe kwa tahadhari, kwa mfano tuna tishio la nzige sasa hivi, lakini tuna tishio la kweleakwelea na viwavi jeshi, kwa hali ya hewa inavyoonesha na hali ya hewa ya mvua hicho kitu time yoyote kinaweza kutokea katika maeneo yetu. Sasa matatizo haya huwa yanatokea katika maeneo mengi na hakuna taarifa zinazotolewa. Je, ni lini Serikali itakuwa ina utaratibu wa kuweza kutujulisha kama nchi, yale matukio ya hatari kama haya yanavyoweza kutokea na kuweza kujilinda na kuwa tayari kuweza kukabiliana nayo?
MHE. SALUM MWINYI REHANI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, nauliza maswali mawili ya nyongeza; Je, Serikali ina mkakati gani wa ndani ambao utahakikisha kwamba viuatilifu vyote vinaagizwa kwa mfumo wa bulk procurement ambao sasa hivi haujaanza. Mfumo huu ndiyo ule ambao unasaidia kulifanya zao la korosho ku-stand kwenye uzalishaji mkubwa zaidi kama ulivyofanyika mwaka juzi?

Mheshimiwa Mwenyekiti, mpango wa udhibiti wa wafanyabiashara wasio waaminifu pamoja na kutumia watafiti ambao wengine wanashirikiana katika kutengeneza baadhi ya viuatilifu ambavyo wanavichanganya na dawa kama za salfa, dawa kama za pecoxystrobin na proquinazid ambazo zinachangia sana kuweza kusaidia kuongeza uwezo wa kemikali na kuua wadudu lakini vinaharibu mazingira katika maeneo yetu. Je, mkakati gani upo ambao utaweza kuwadhibiti kupitia TPRA hawa wafanya biashara ambao si waaminifu?

Hon. Dr. Tulia Ackson

Speaker

Legislative Role

Profile

Ask the Speaker / Comments

Ms. Nenelwa J. Mwihambi

Clerk of the National Assembly

Legislative Role

Profile

Ask the Clerk / Comments

View All MP's