Parliament of Tanzania

Questions By: Hon. Livingstone Joseph Lusinde

Supplementary Questions
NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa wa Maji na Umwagiliaji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Livingstone Joseph Lusinde, lenye sehemu (a) na (b) kwa pamoja, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, katika kutekeleza Miradi ya Maji ya Vijiji Kumi kwa kila Halmashauri, Halmashauri ya Chamwino inatekeleza miradi kwenye vijiji saba ambapo miradi katika Vijiji vitano vya Mvumi Makulu, Itiso, Mvumi Mission, Chamuhumba na Membe imekamilika na wananchi wapatao 49,000 wanapata huduma ya maji. Mradi wa Wilunze unaendelea kutekelezwa na upo asilimia 60.
Mheshimiwa Naibu Spika, utekelezaji wa mradi wa maji katika Kijiji cha Manzase umefikia asilimia 40. Kazi zilizofanyika hadi sasa ni ujenzi wa vituo 11 vya kuchotea maji, ujenzi wa nyumba ya mashine na ujenzi wa tanki lenye ujazo wa lita 80,000. Gharama ya ujenzi wa mradi ni shilingi milioni 355, ambapo hadi sasa kiasi cha shilingi milioni 71 kimeshapelekwa kwenye Halmashauri hiyo kwa ajili ya utekelezaji wa mradi huu. Serikali itaendelea kupeleka fedha ili kukamilisha mradi huo.
Mheshimiwa Naibu Spika, Mradi wa Maji katika Kijiji cha Chinoje ni kati ya miradi iliyokosa chanzo cha maji wakati wa utekelezaji wa awamu ya kwanza ya Program ya Maendeleo ya Maji. Utafiti wa chanzo kingine cha maji unafanyika na ujenzi wa mradi utafanyika katika mwaka wa fedha 2016/2017.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimshukuru Naibu Waziri kwa majibu mazuri, lakini niulize maswali mawili madogo ya nyongeza. Swali la kwanza, kwa kuwa wananchi wa Manzase wanakabiliwa na kero kubwa ya maji na Mkandarasi hayupo kwenye eneo la Site, je, Naibu Waziri yuko tayari kuongozana na mimi kufika Manzase kwenda kuonana na wananchi na kuwahakikishia mwenyewe kwamba kweli mradi ule utakamilika?
Swali la pili, kwa kuwa Mradi wa World Bank, maeneo mengi maji yalipochimbwa vijijini hayakupatikana na wananchi wanaendelea kukabiliwa na shida kubwa ya maji. Serikali ina mpango gani wa kukamilisha miradi ya maji au Je, wananchi waendelee kusuburi tena, hawana mpango wowote Serikali mpaka Benki ya Dunia itusaidie tena? Ahsante.
MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri ya Naibu Waziri, nina maswali mawili madogo ya nyongeza. Swali la kwanza; kwa kuwa wananchi wamezoea kabla ya barabara ya lami kujengwa huanza na upembuzi yakinifu: Mpaka sasa hivi hakuna hata dalili hizo: Je, Mheshimiwa Naibu Waziri anatuhakikishiaje wananchi wa Jimbo la Mtera kwamba upembuzi yakinifu utakaopelekea ujenzi wa lami ya barabara ile utaanza kufanyika?
Swali la pili, Naibu Waziri amejibu kwamba Serikali itaendelea kuitengeneza barabara ile kwa kiwango cha changarawe; barabara ile haijawahi kutengenezwa kwa kiwango hicho kwa muda mrefu. Je, kwa majibu hayo, Naibu Waziri anataka kutuhakikishia kwamba kwa maneno yake tu ya leo barabara ile imepandishwa hadhi na kuwa barabara ya Mkoa? Ahsante.
MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE: Mheshimiwa Spika, kwanza nimshukuru Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu, hata hivyo naomba niulize maswali madogo mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Spika, kwa kuwa Mkoa mzima wa Dodoma hakuna sehemu ambayo tuna mto unaotiririsha maji mwaka mzima, na kwa kuwa mradi ule haukuzingatia uchimbaji wa bwawa kwa maana ya kuyahifadhi maji ili baadaye wananchi waweze kuyatumia kwa kumwagilia.
Je, Mheshimiwa Waziri anatuambia nini juu ya uchimbwaji wa bwawa ili tuweze kuvuna maji na baadae tuweze kuyatumia na ili ule mradi uweze kuleta ufanisi?
Swali la pili, kwa kuwa kwenye majibu ya Serikali kuna baadhi ya vitu vingi vimeachwa, Naibu Waziri yuko tayari kuongozana na mimi kwenda kujionea kwa macho hali ilivyo kwenye mradi huo? Ahsante (Makofi)
MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nimshukuru sana Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu yake. Hata hivyo napenda niulize maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, punde wakati akijibu maswali leo asubuhi, amesema barabara ili ijengwe kwa kiwango cha lami inapitia upembuzi yakinifu na usanifu wa kina; na kwa muda aliouonyesha ni kama vile kila kitendo kinachukua zaidi ya miaka miwili.
Je, kwa miaka iliyobaki kabla hata ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina haujaanza kufanyika, Waziri anawahakikishiaje wananchi wa Jimbo la Mtera kwamba barabara hiyo itakamilika mwaka 2020?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, Mheshimiwa Naibu Waziri amesema barabara hiyo itaendelea kujengwa kwa kiwango cha changarawe na sasa hivi barabara hiyo bahati nzuri inajengwa. Je, Naibu Waziri yuko tayari kuongozana na mimi ili akaone hicho kiwango cha changarawe anachokisema kwamba kinajengwa badala ya kiwango cha changarawe naona wanajenga kwa kiwango cha tope, yuko tayari twende tukaone site? Ahsante
MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE: Mheshimiwa Naibu Spika, nikushukuru sana kwa kupata fursa hii. Kama alivyouliza Mheshimiwa Mgumba, majimbo ya vijijini yana matatizo makubwa sana ya umeme hasa katika center za Kata ya Mpwayungu, Kata ya N’ninyi, Manzase na Makao Makuu ya Kata ya Muungano ambako hakuna umeme kabisa. Sasa je, ni lini Serikali itapeleka umeme katika maeneo haya hususan katika Kata ya Muungano? Ahsante. (Makofi)
MHE. LIVINGSONE J. LUSINDE: Mheshimiwa Naibu Spika, namshukuru Naibu Waziri kwa majibu, hata hivyo napenda kuuliza maswali mawili madogo ya nyongeza kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza; urefu wa barabara alizotaja na milioni 350 kweli hapo kuna matengenezo ya barabara kwa kiwango cha changarawe au ni kwa kiwango cha tope?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; kwa kuwa mvua za mwaka huu Mungu ametupa neema zimekuwa nyingi na zimetusaidia sana kwa upande wa kilimo, vilevile zimeleta uharibifu mkubwa sana wa barabara na madaraja, Mheshimiwa Waziri anatuambiaje juu ya matengenezo mazuri na yenye maana kwa ajili ya wananchi kuweza kupitisha mazao yao ambayo wanategemea kuyavuna ili waweze kujiletea maendeleo? Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana.
MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri, napenda kuuliza maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kufuatia kuuwawa kwa Ndugu Emmanuel Ernest wa Ilolo na Stefano Ndalu wa Nhinyi na Amani Joseph Sita wa Mvumi Mission kujeruhiwa vibaya na kupata malipo kidogo sana, je, ni lini sasa Serikali itaruhusu vijiji viweze kumiliki silaha kwa ajili ya kujilinda na wanyama hao wakali?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la pili, pesa aliyoitaja Mheshimiwa Naibu Waziri kuwa imelipwa kwa watu 27 ukiigawanya ni sawasawa na shilingi 278,518. Sasa Mheshimiwa Naibu Waziri anaweza kuwatangazia Watanzania kwamba katika nchi yetu tembo wana thamani kubwa kuliko uhai wa watu? Ahsante. (Makofi)
MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE: Mheshimiwa Naibu Spika, nikushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili madogo ya nyongeza. Kwanza nawapongeza sana Mheshimiwa Naibu Waziri pamoja na Waziri wake kwa namna ambavyo wanafanya kazi kwenye Wizara hii. Hongereni sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza, kwa kuwa eneo lile na Tarafa nzima ya Mkwayungu limegundulika kuwa na madini mengi sana ya gypsum na dhahabu kwa upande


wa Mafulungu na ninyi Serikali mlikuwa mmeona kabisa watu wanachimba na wanapata fedha na nyie mnapata kodi lakini baadaye mlisimamisha uchimbaji wa madini ya gypsum. Je, ni lini Serikali itawafungulia wale wachimbaji wengine ili waendelee kuchimba na nyie muendelee kupata mapato na wananchi waendelee kufanya kazi zao?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, Mheshimiwa Naibu Waziri yuko tayari kuongozana nami ili twende tukajionee hali halisi ya watu wanaochimba dhahabu Mafulungu na wale wanaopata tabu ya kuchimba madini ya gypsum pale Manda ili tukaone na tukatatue matatizo yao kwa macho huku akishuhudia? Ahsante. (Makofi)
MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE: Mheshimiwa Spika, nikushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili madogo ya nyongeza.

Swali la kwanza Mheshimiwa Naibu Waziri katika jibu lake amesema ujenzi umeshaanza. Je, yuko tayari kuongozana na mimi kesho ili akaone ujenzi kama umeanza au watu wake wamemdanganya?

Mheshimiwa Spika, swali la pili, kutokana na kunyesha kwa mvua barabara nyingi siyo tu zimeharibika bali zimeoza na hii imepelekea wazazi kupata shida kufika hospitali hasa kwa barabara ya Huzi kuja Manda ambapo ukitoka Manda kuja Huzi kuja kwenye Kituo cha Afya cha Mpwayungu, lakini Mvumi Mission hakuingiliki pande zote, madaraja yamezingirwa na maji na yamevunjika.

Mheshimiwa Naibu Waziri anatuambiaje kuhusu kutengeneza kwa haraka ili kunusuru maisha ya akinamama na watoto na wagonjwa akinababa ili waweze kufika hospitali? Ahsante sana.
MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE: Mheshimiwa Spika, nikushukuru tena kunipa nafasi ili niweze kuuliza maswali madogo mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, Jimbo la Mtera lina kata 22, na lina vijiji zaidi ya 60 na kitu, Mheshimiwa Naibu Waziri kwenye jibu lake la msingi anasema wana mpango wa kujenga vituo kila kata, haelezi mpango huo unaanza lini? Lakini Jimbo la Mtera lina Tarafa tatu.

Swali langu la kwanza dogo la nyongeza linasema, kama kwenye Tarafa tu hawajajenga Kituo hata kimoja, je hiyo kwenye kata itawezekana? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali langu la pili, barabara kubwa ya Iringa - Dodoma inayopita kwenye Jimbo la Mtera, Kibakwe, Isimani Waheshimiwa Wabunge wengi na Mawaziri wanapita njia ile lakini haina Kituo cha Polisi hata kimoja chenye gari. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, matokeo yake ajali zote kubwa zinazotokea njia ile, polisi inawachukua muda mrefu sana kufika, kwa mfano wiki mbili zilizopita ilitokea ajali mbaya sana mama mmoja mzazi alipoteza maisha, nesi alipoteza maisha, pamoja na wasindikizaji, polisi walikuwa wanakuja wengine na lori, fuso iliwachukua muda sana kwenda kumaliza tatizo pale.

Je, Serikali ni basi itakipatia Kituo cha Mvumi Misheni gari, walau liweze kusaidia kufanya mzunguko katika barabara hiyo kubwa? Ahsante sana. (Makofi)
MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE: Mheshimiwa Spika, ninakushukuru kwa kunipa nafasi hii ya kuuliza swali moja la nyongeza lakini nami niwapongeze Yanga kwa kupata Ubingwa baada ya kusota kwa miaka minne ndiyo leo wanapumua hapa unawasikia, ubingwa ulikuwa mikononi mwa Simba. Baada ya kuwapongeza naomba niulize swali moja la nyongeza:-

Mheshimiwa Naibu Waziri, utakubali kuongozana nami kufika Mvumi kujionea hali ilivyo kwa askari wa pale Mvumi Misheni ili tuweze kujenga kituo pamoja? (Makofi)
MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE: Mheshimiwa Spika, ninakushukuru kwa kunipa nafasi hii ya kuuliza swali moja la nyongeza lakini nami niwapongeze Yanga kwa kupata Ubingwa baada ya kusota kwa miaka minne ndiyo leo wanapumua hapa unawasikia, ubingwa ulikuwa mikononi mwa Simba. Baada ya kuwapongeza naomba niulize swali moja la nyongeza:-

Mheshimiwa Naibu Waziri, utakubali kuongozana nami kufika Mvumi kujionea hali ilivyo kwa askari wa pale Mvumi Misheni ili tuweze kujenga kituo pamoja? (Makofi)

Hon. Dr. Tulia Ackson

Speaker

Legislative Role

Profile

Ask the Speaker / Comments

Ms. Nenelwa J. Mwihambi

Clerk of the National Assembly

Legislative Role

Profile

Ask the Clerk / Comments

View All MP's