Parliament of Tanzania

Questions By: Hon. Suleiman Masoud Nchambi

Supplementary Questions
MHE. SULEIMAN M. NCHAMBI: Mheshimiwa Naibu Spika, wabheja sana. Kwa kuwa Jimbo la Kishapu halikupata mgao wa magari mapya ya polisi katika awamu hii na Jimbo hili lenye watu sharp na askari wanaofanya kazi zao kwa u-sharp, lina magari mawili mabovu yenye umri wa zaidi ya miaka mitano.
Je, Mheshimiwa Naibu Waziri, nilipata ahadi kuwa mwezi wa pili tutapata magari mapya ya polisi, uko tayari kunihakikishia Jimbo sharp litapata magari mapya ili Wananchi waweze kupata huduma hasa za kiusalama wanapohitaji kuliko hivi sasa polisi wangu wa Kishapu wanavyohangaika? Wabheja
MHE. SULEIMAN M. NCHAMBI: Mheshimiwa Naibu Spika, wabheja sana. kwa niaba ya wananchi sharp wa Jimbo Sharp, namwomba Mheshimiwa Naibu Waziri, Jimbo la Kishapu limekamilisha ujenzi wa hospitali ya kisasa kabisa ya Wilaya, tena ni hospitali ya mfano na kujivunia ambayo Serikali ya Chama cha Mapinduzi, imeijenga kwa kushirikiana na wananchi wa Jimbo la Kishapu pamoja na Wawekezaji.
Kwa kuwa, hospitali hiyo ina upungufu mchache, imekamilika takribani kwa asilima 78 na upungufu huo katika swali la nyongeza hauwezi kunoga kuueleza, nimwombe Naibu Waziri, yuko tayari kufuatana na Mbunge sharp, kwenda kwa wananchi sharp, kuiona hospitali sharp, inayotoa huduma sharp sharp, ili mambo yaendelee kuwa sharp wakati wowote atakapotamka kwamba yuko tayari? Wabheja Sana.
MHE. SULEIMAN M. NCHAMBI: Namuomba sasa Mheshimiwa Mwiguli na Naibu wake Mawaziri hawa shapu wanaofanya mambo kwa ushapu watumie neema hiyo kwa kutengeneza mabwawa kwa ajili ya umwagiliaji wa mazao ambayo yatawakomboa wana Kishapu.
MHE. SULEIMAN M. NCHAMBI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana. Kwa kuwa tatizo hili la pembejeo hasa mbegu bora ni tatizo ambalo kwa kweli linatakiwa sasa lishughulikiwe kwa kina na kwa kuwa Mungu ameijalia Wizara hii ya Kilimo kupata Waziri na Naibu Waziri ambao ni wachapa kazi na ni mahodari, je, kutokana na uhaba wa mvua, Mheshimiwa Waziri, Naibu Waziri na Wizara wapo tayari kuharakisha tafiti za mbegu ambazo zitaendana na mazingira ya sasa
MHE. SULEIMAN M. NCHAMBI: Mheshimiwa Mwenyekiti, wabeja sana. Kwa niaba ya wananchi Shapu wa Jimbo la Kishapu, kwanza naomba nitoe shukrani za dhati kwa Wizara kwa kutekeleza mradi kabambe wa maji ya ziwa victori katika Jimbo la Kishapu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pili, naomba nije na scenario tofauti baada ya mradi huo kufika katika Mji Mdogo wa Muhunze, Mbunge wa Kishapu kushirikiana na viongozi wa Kishapu tumeshafanya mkakati kabambe wa kutafuta mkandarasi ambaye anaweza kutupatia fedha kwa vigezo vile ambavyo Serikali inaweza ikaridhia. Je, Mheshimiwa Waziri je, yuko tayari kukaa na uongozi wa Kishapu ukiongozwa na Mbunge wa Kishapu ili tumweleze kuwa tumeshapata fedha ambazo zinaweza zikayasambaza maji katika Jimbo lote la Kishapu katika vitongoji vyote vya Kishapu iwapo utaridhia tena kwa masharti yale ambayo Serikali inaya…(Makofi)
MHE. SULEIMAN M. NCHAMBI: Mheshimiwa Naibu Spika, wabheja sana.
Kwa kuwa Jimbo la Kishapu lenye watu shapu na Mbunge shapu, ni moja ya Majimbo ama Jimbo lililotekeleza kwa kiwango cha juu sana mpango wa huduma za afya. Tunayo hospitali ya kisasa kabisa katika Wilaya yetu ya Kishapu, tuna vituo vinne vya afya vya kisasa kabisa ambavyo vimekamilika na vinatoa huduma bora katika Jimbo la Kishapu, lakini katika vijiji 118, takribani asilimia 50 mpango wa zahanati katika Jimbo la Kishapu unaendelea vizuri na miongoni mwa vituo hivyo vya zahanati vinatoa huduma bora.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu je, ndugu yangu, wajina Mheshimiwa Suleiman Jafo na dada yangu Mheshimiwa Ummy, kutokana na malumbano ama tatizo kubwa la mpango wa afya ambalo ni dhahiri limeelezeka na wewe umekiri kuwa watu wengi wanahitaji kuuliza maswali katika jambo hili la afya na kwa kuwa Kishapu tumekwishajitahidi tumepiga hatua…
Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana.
Kwa kuwa Kishapu tumepiga hatua kubwa, je, Wizara ya Afya na Ofisi ya TAMISEMI kwa maana ya Wizara hawaoni sasa watoe kipaumbele kwa Jimbo la Kishapu ili kuiweka kuwa ni ajenda maalum na kipaumbele cha kumaliza tatizo hili ili Kishapu iwe mfano katika Wilaya zote nchini kwa kumaliza kabisa tatizo hili kwa kutuongezea michango?
MHE. SULEIMAN S. MURAD: Mheshimiwa Mwenyekiti, na yeye apewe maelekezo afike kwenye kaya zote. Na Mheshimiwa Naibu Waziri nakukaribisha Mvomero karibu sana. (Makofi)
MHE. SULEIMAN M. NCHAMBI: Mheshimiwa Mwenyekiti, wabheja sana. Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa Jimbo la Kishapu lina zahanati 45 zilizokamilika na zinafanya kazi, vituo vya afya vinne vimekamilika vinafanya kazi na viwili tayari tunasubiri vianze kufanya kazi hivi karibuni na tuna hospitali kubwa ya kisasa ambayo inafanya kazi vizuri. Kwa kuwa tumekwishaleta maombi ya upungufu wa baadhi ya madaktari, wauguzi na watumishi wa kada ya afya, je, Mheshimiwa Naibu Waziri, uko tayari kukaa na mimi hata leo tupitie maombi hayo uone namna ambavyo utasaidia jitihada za watu wa Kishapu? Mheshimiwa Mwenyekiti, wabheja sana. (Makofi)
MHE. SULEIMAN M. NCHAMBI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya wananchi shapu wa Jimbo la Kishapu, naomba nitoe pongezi kwa Wizara kwa kazi nzuri manayoifanya, lakini nina swali la nyongeza kwakuwa bararaba ya Kolandoto kwenda Kishapu ni muhimu kwa kuwekwa lami kwa sababu za kiuchumi na mambo mengine. Je ni lini Serikali itaanza kujenga barabara hiyo ya lami kutoka angalau Kolandoto kwenda Kishapu?

Hon. Dr. Tulia Ackson

Speaker

Legislative Role

Profile

Ask the Speaker / Comments

Ms. Nenelwa J. Mwihambi

Clerk of the National Assembly

Legislative Role

Profile

Ask the Clerk / Comments

View All MP's