Parliament of Tanzania

Supplementary Questions

MHE.DKT. MARY M. MWANJELWA: Mheshimiwa Naibu Spika, ninakushukuru sana kwa kuniona.
Kwa kuwa, tatizo la Tabora linafanana sana na tatizo la Mbeya, mojawapo ya Sera ya Awamu ya Tano ni kufufua na kuimarisha viwanda vya ndani katika kukuza uchumi wa ndani, lakini vilevile kuongeza soko la ajira.
Mheshimiwa Naibu Spika, Mbeya tuna kiwanda cha Mbeya Textile ambacho kimetelekezwa kwa muda mrefu sana, ninaomba Mheshimiwa Waziri atuambie nini mkakati wa kiwanda kile cha Mbeyatex ambacho kimetelekezwa kwa miaka mingi sana? Ahsante sana.


Answer

WAZIRI WA VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, suala la kufufua viwanda hasa viwanda vya nguo, siwezi kutoa jibu moja likawaridhisha Watanzania au Waheshimiwa Wabunge, ni mapana ambayo siwezi kuyakumbatia, kufufua viwanda hivi lazima vifufuke. Ukisoma mkakati wa (C to C) Cotton to Clothing, unaelezea tutakavyofanya, inaanzia kwa wananchi kulima na Serikali kuwawezesha wananchi kulima. Lakini unakwenda zaidi mpaka kwa kudhibiti wananchi wanaoagiza nguo kutoka nje ya nchi ambazo ni dhaifu lakini wengine hawalipi ushuru.
Mheshimiwa Naibu Spika, juzi nimeletewa ripoti, TRA kuanzia mwezi Januari mpaka mwezi wa Mei, walikuwa wameshindwa kuwakamata watu waliopitisha nguo ambazo hazikulipa bilioni 133. Natoka hapa nakwenda kuripoti kwa Waziri wa Fedha, bilioni 133, nguo zilikuwa under-valued, nguo moja nimeoneshwa na wataalam, kilo moja ya nguo ilikuwa imeingizwa nchini kwa kadirio la bei ambayo ni ndogo kuliko pamba, finishing cloth, nguo iliyokwisha tengenezwa kilo moja yake ilikuwa imeingizwa nchini kwa thamani ambayo ni ndogo kuliko bei ya pamba ya Mwanza. Sasa mazingira yote kwa ujumla ndiyo yanafanya ufufuaji wa viwanda hivi iwe vigumu, lakini yote hayo tunayamudu, tutayafanyia kazi, Mbeyatex na yenyewe itafanya kazi.

Hon. Dr. Tulia Ackson

Speaker

Legislative Role

Profile

Ask the Speaker / Comments

Ms. Nenelwa J. Mwihambi

Clerk of the National Assembly

Legislative Role

Profile

Ask the Clerk / Comments

View All MP's