Parliament of Tanzania

Questions By: Hon. Saul Henry Amon

Supplementary Questions
MHE. SAUL H. AMON: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi hii ya kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Wilaya ya Rungwe ni moja kati ya Wilaya ambazo zimebarikiwa sana kuwa na vyanzo vingi vya maji. Hata hivyo, kuna baadhi ya maeneo maji yamefungwa yasiendelee kutiririka kwa sababu ya uhaba wa maji, hakuna matenki, miundombinu ni ya kizamani mno na watu wameongezeka.
Je, Serikali ina mpango gani na Wilaya ya Rungwe ili kuisambazia maji ambayo hayana taabu ni maji ya kutega? (Makofi)
MHE. SAUL H. AMON: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa majibu mazuri ya Naibu Waziri. Naomba kama Naibu Waziri ana nafasi aone hali ilivyo mbaya, kile kipande cha kata nne hata kwenda kuwasalimia tunaogopa kwa sababu tunatoa ahadi lakini haitimizwi. Je, yuko tayari kuongozana na mimi akaangalie hali ilivyo mbaya ya hicho kipande cha kutoka Njiapanda mpaka Mpakani? (Makofi)
Mheshimiwa Spika, swali la pili, vilevile barabara hii iko sawa kabisa na barabara ya Igogwe – Mchangani - Mbeye One. Mazao ni mengi lakini wananchi wa eneo hilo wanauza mazao kwa bei ya chini sana kwa sababu hakuna usafiri. Naomba Waziri atakapokuja Rungwe aangalie vipande hivyo viwili na aone ukweli na hali halisi ilivyo kwa wananchi wa Rungwe. (Makofi)
MHE. SAUL H. AMON: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi hii.

Kwanza nishukuru Serikali kwa kuboresha Vituo vya Afya vya Masukulu na Ikuti, hapo nashukuru sana, kwani sasa hivi vinaonekana kama hospitali, lakini wananchi wa Kata ya Mpuguso na Kata ya Isongole kwa nguvu zao wamejenga vituo vya afya kufikia hatua ya maboma, wengine mpaka kumalizia kwenye ceiling board.

Je, Serikali ina mpango gani wa kumalizia hivi vituo vya afya kwa hao watu wanaotoka mbali sana ili viweze kwisha kwa haraka na waweze kuvitumia?

Hon. Dr. Tulia Ackson

Speaker

Legislative Role

Profile

Ask the Speaker / Comments

Ms. Nenelwa J. Mwihambi

Clerk of the National Assembly

Legislative Role

Profile

Ask the Clerk / Comments

View All MP's