Parliament of Tanzania

Questions By: Hon. Dr. Elly Marko Macha

Supplementary Questions
MHE. DKT. ELLY M. MACHA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Napenda kumuuliza Mheshimiwa Waziri swali moja dogo la nyongeza, je, Waziri anaweza kulihakikishia Bunge hili kwamba katika hii bajeti ya 2016/2017, kutatengwa bajeti kwa ajili ya kuliwezesha Baraza la Ushauri kwa Watu Wenye Ulemavu kuanza kazi na programu zake kuwafikia watu wenye ulemavu? (Makofi)
MHE. DKT. ELLY M. MACHA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Sikuridhika sana na jibu lililotolewa na Mheshimiwa Naibu Waziri hasa katika kipengele (a). Kwa ajili hiyo basi, naomba kumuuliza maswali mawili madogo ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza, ni lini basi mchakato wa mabadiliko ya sheria utafanyika ili kuhakikisha kwamba sheria inawapigania watu wenye ulemavu kwa kuwaongezea umri wa kustaafu kwa kuwa umri wao wa kuanza shule unakua umechelewa ili waweze kupata nafasi ya kufanya kazi zaidi?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, ni mechanism gani ambayo Serikali imeweka katika kuhakikisha kwamba taasisi zake pamoja na sekta binafsi zinatenga asilimia tatu katika kila waajiriwa 20? Ahsante.
MHE. DKT. ELLY M. MACHA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Napenda kusema tu kwamba sikuridhika kabisa na nina hakika watu wenye ulemavu hawakuridhika kabisa na majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri ambayo ameyatoa. Ina maana kwamba kwa kutokuwa na miundombinu au kutokuwa na watumishi ni sababu ya kutosha ya kusababisha vyuo vifungwe kwa miaka mingi? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la kwanza. Naomba Mheshimiwa Naibu Waziri atupe concrete sababu kwa nini vyuo vimefungwa na vitafunguliwa lini, atupatie time frame.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, hawa watumishi ambao anasema wanatayarishwa, tunahitaji muda gani kuwatayarisha hawa watumishi kwa sababu watu wenye ulemavu wamekuwepo na vyuo vimekuwepo miaka mingi lakini vimefungwa kwa miaka mingi na inaonekana kama ni business as usual but it is not business as usual. Ahsante.

Hon. Dr. Tulia Ackson

Speaker

Legislative Role

Profile

Ask the Speaker / Comments

Ms. Nenelwa J. Mwihambi

Clerk of the National Assembly

Legislative Role

Profile

Ask the Clerk / Comments

View All MP's