Parliament of Tanzania

Questions By: Hon. Flatei Gregory Massay

Supplementary Questions
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi niulize maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza, kwa kuwa miradi hii haijakamilika na wananchi sasa hivi wanapata adha ya kutopata maji hasa katika miji niliyoisema na vijiji vyake, je, Serikali itahakikisha vipi leo hii itapeleka pesa kule ili wananchi wapate maji?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kutokana na adha ya maji katika maeneo yetu, yuko mwananchi mmoja amechimba maji na kuyapata katika Mji wa Hydom. Je, kwa nini Serikali isiweze kupata maji katika maeneo yale na kuweka hela nyingi namna hii? Waziri yuko tayari kufuatana na mimi akaone jinsi ambavyo wananchi wanapata adha katika mji wa Hydom na maeneo mengine ya Mbulu Vijini? (Makofi)
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Spika, ahsante sana, ninaomba kumuuliza Mheshimiwa Waziri maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa sasa uhalifu umeongezeka katika bonde la Yayeda Chini, hasa ubakaji na mengineyo mengi; gari lililosemwa hapo kwanza ni bovu au chakavu katika eneo hilo la polisi au kituo cha polisi, Hydom. Lakini hiyo haitoshi hapo, mvua ikinyesha kidogo bonde la Yayeda Chini halipitiki kutoka Haidom kwa gari lolote.
Je, Serikali haioni kwamba bado wananchi wa Yayeda Chini wana haki ya kulindwa wao na mali zao?

Mheshimiwa Spika, swali la pili. Kwa kuwa wananchi wa Yayeda Chini wanahitaji kulindwa: Je, tukiwahamasisha, Serikali iko tayari ku- chip in ili kujenga kituo hicho pamoja na wananchi?
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Kwanza, kwa kuwa Mbulu walishapewa ahadi ya kujengewa uwanja na Olympic na sasa wale wameondoka na eneo hilo lipo mpaka sasa na wananchi wa Mbulu wamekubali kutoa eneo hilo. Je, Serikali haioni ndiyo sasa wakati wa kuja kuwekeza au kujenga kituo hicho Mbulu?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kwa kuwa wanariadha wazuri ambao wamevunja rekodi ya dunia mpaka leo na haijawahi kuvunjwa mfano Philbert Bai ambao wamekuwa msaada mkubwa kwa Tanzania, je, Serikali haioni sasa ndiyo muda muafaka wa kujenga kituo hicho Mbulu kwa sababu uwezo wa Mbulu na uoto wa asili na hali ya hewa inawaruhusu wanariadha kuweza kufanya mazoezi na kushinda Olympic?
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali ya nyongeza.
Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri je, ni lini sasa Serikali itaanza kutoa mikopo hiyo?
Swali la pili, kwa kuwa wananchi wa Mkoa wa Manyara hasa Mbulu Vijijini wako tayari kabisa kwa elimu hiyo ya ujasiriamali, je, Mheshimiwa Waziri anaweza kusema anaweza kuanza na Mkoa huo kwa kuwa uko tayari?
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Naibu Spika, asante sana.
Kwa kuwa, ni makosa ya uchapaji nashukuru amekiri kuwa Kata hii ya Qurus ipo na kwamba Kijiji hiki cha Gongali ndiko ofisi ya TANESCO ilipo. Sasa
kuna Vijiji ambavyo amevitaja hapa katika swali la msingi ambavyo vinaitwa Gendaa na Bashay;
Je, ni lini vitapata umeme?
Pia, kwa kuwa Wilaya hii ya Karatu ni pacha kabisa na jimbo la Mbulu Vijijini; Je, Vijiji vya Mbulu Vijiji ambavyo vinafanana kabisa kwa majina haya ya Gendaa ambavyo viko Mbulu Vijijini na Bashay ambavyo viko Mbulu Vijijini na Vijiji vingine vya Endara Gadati na Vijiji na Haidereri, Kantananati, Bashay, Yaeda Ampa lini vitapatiwa umeme?
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ili niulize swali la nyongeza.
Kwa kuwa Jimbo hili la Same Mashariki linafanana kabisa na Jimbo la Mbulu Vijijini kwa mahitaji. Same Mashariki wanalima kitu kinachoitwa tangawizi, Mbulu Vijijini tunalima vitunguu na tuna tatizo hili la soko. Je, Serikali ina mpango gani kusaidia wananchi wa Mbulu Vijijini kwa zao hili la vitunguu swaumu maana yake ni maarufu sana pale Bashineti Mbulu ili kuhakikisha kwamba maisha haya yanakwenda vizuri?
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Naibu Spika, ninakushukuru sana kwa kunipatia muda wa kuweza kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa Mheshimiwa Waziri amesema amefika mikoa hii 23, kwanza nimshukuru sana kwa kuweka plan ya kujenga barabara ya Mbulu - Karatu, Mbulu - Haydom - Singida kwa kiwango cha lami. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, ni lini sasa Serikali itaanza kujenga barabara hii kwa kuanzia na upembuzi yakinifu? Ahsante sana.
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, Mbulu ni Wilaya kongwe, imeanza 1905, sawa na Nairobi. Pamoja na ahadi zilizotolewa kwa muda mrefu na Marais waliyotangulia. Je, kwa kuchelewa kutengeneza barabara hii, huoni kwamba ni kuwadanganya wananchi wa Mbulu na kuwakatisha tamaa?
Swali la pili, kwa kuwa barabara hii ya kwenda Hydom, ipo Hospitali kubwa ya Rufaa ya Hydom ambayo ni Hospitali ya Kanda; na sasa hivi daraja la Enagao limevunjika na wananchi hawezi kwenda kwenye Hospitali hiyo: Je, Serikali haioni kwamba kwa kuendelea kutopitika barabara hii kunaweza kuendelea kupoteza maisha ya watu na wasipate huduma katika hospitali hiyo? (Makofi)
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa muda wa kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Kwa kuwa umeme umefika Dongobesh miaka 11 iliyopita na haujawahi kwenda kijiji hata kimoja na pia miaka ya tisini umefika Haydom. Je, Serikali iko tayari sasa kusogeza umeme huo kutoka Kata hizo ambazo nimezisema kuelekea kwenye Kata ambazo amezitaja? (Makofi)
Swali la pili, kwa kuwa tuna miradi ambayo ni ya maji, na inahitaji umeme na kwenye REA phase two, hatujawahi kupata mradi huo: Je, Serikali iko tayari kukubali sasa kuanza na Vijiji hivi vya Kata ya Hayderer, Getanyamba, Dinamu, Maretadu, Masieda, Laba na Dinamu?
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana kunipatia muda wa kuuliza maswali mawili ya nyongeza.
Kwa kuwa Hospitali ya Haydom inahudumia Mikoa ambayo umeitaja ya Singida, Simiyu, Arusha, Dodoma na Mara; na nashukuru Serikali kwa kutoa fedha na kupanga kiwango hiki cha shilingi milioni 570.
Je, kwa kuwa Serikali sasa imesema haya na hela iliyopelekwa ni kidogo, haioni sasa ni muda wa kuongeza ruzuku hii ili hospitali hii ikaweza kutoa huduma nzuri kwa watu wanaozunguka?
Swali la pili, kwa kuwa tumeleta maombi ya hospitali hii kupandishwa hadhi kuwa hospitali ya Kikanda na kwa kuwa Wabunge wanaozunguka hospitali hii na Mikoa niliyoitaja tumeomba namna hiyo.
Je, ni lini sasa Serikali itajibu maombi haya ya kuipandisha Hospitali ya Haydom kuwa Hospitali ya Kanda?
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kunipa muda wa kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa Mheshimiwa Waziri ametoa majibu mazuri sana, kwanza nampongeza. Pili kwa kuwa kundi la walemavu limekuwa likisahaulika sana hasa katika suala hili la mikopo, ukizingatia wapo vijana wa kike na wa kiume, lakini je, kwenye mpango huu wa milioni 500, kundi la walemavu limekuwa considered namna gani. Je, Mheshimiwa Waziri anaweza kunithibitishia hilo?
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa Jimbo la Mheshimiwa Profesa Maji Marefu la Korogwe Vijijini ni pacha kabisa na Jimbo la Mbulu Vijijini kutokana na hali ya kukosa mawasiliano. Je, Serikali ina mpango gani wa kupeleka mawasiliano kwenye Kata ya Ari, Tumati, Mung’ahai, Ng’orati, Masieda, Endagi, Chani kule Mbulu Vijijini?
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Kwa kuwa Jimbo la Morogoro Mjini linafanana kabisa na Jimbo la Mbulu Vijijini juu ya tatizo hili la ukosefu wa maji. Kwa kuwa Waziri alishaniahidi kwamba tukipeleka certificate atawasaidia wakandarasi kuwalipa fedha waendelee na mradi. Je, ni lini sasa watapatiwa fedha, miradi ya Mbulu iliyopo Haidom na Dongobeshi ili wakandarasi waweze kumalizia na wananchi wapate maji? Ahsante
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Mwenyekiti, nikushukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali moja la nyongeza.
Kwa kuwa Jimbo la Mpwapwa linafanana kabisa na Jimbo la Mbulu Vijijini kwa ukosefu wa maji kwa eneo kubwa mno, je, ni lini Serikali itakuwa tayari kuja kuviangalia hivi vijiji na kata za Labay, Bisigeta, Maretadu, Endamilay, Endahagichan, Bashnet na Dinamu, ili kuzipatia visima virefu na wananchi wa Jimbo la Mbulu Vijijini kupata maji?
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Naibu Waziri amefika katika hospitali ya Hydom, lakini nina maswali mawili madogo ya nyongeza. Swali la kwanza; kwa kuwa Naibu Waziri amekiri kwamba hospitali hii imepandishwa hadhi miaka sita toka 2010 hadi leo ya kuwa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa na haijapata hata siku moja ile haki ya kibajeti ya hospitali ya Mkoa. Je, sasa ni lini hospitali hii itatengewa bajeti ili ifanane na hospitali zote za Rufaa za Mikoa ya Tanzania?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; kwa kuwa kwenye majibu ya msingi amesema hospitali hii ina tatizo la miundombinu na watumishi. Je, Serikali ina mpango gani sasa wa kuijengea uwezo na kuipatia watumishi ili hospitali ya Haydom iweze kutoa huduma kwa sababu na yeye amekiri kwamba inafikika na maeneo ya jirani na mikoa hii?
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Kwa kuwa hali ya barabara za Lulindi ni nafuu kuliko Mbulu Vijijini; na kuna barabara imeahidiwa ya Karatu - Mbulu; Mbulu – Hydom; Hydom – Sibiti na Mheshimiwa Rais, kwa kujengwa kwa lami; na majibu ya MheshimiwaWaziri yalikuwa yanasema mwanzoni uchambuzi yakinifu umeshaanza. Je, barabara hii inajengwa lini sasa ili wananchi wa Mbulu na maeneo mengine wapate nafuu ya kiuchumi na kupita hasa kuelekea kwenye Hospitali ya Hydom?
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa sasa wanafunzi wa vyuo vikuu wamekuwa wengi ukizingatia Chuo hiki cha Maendeleo ya Jamii Tengeru kimeanza kujaa. Je, Serikali ina mpango gani wa kupandisha vyuo vidogo vya diploma kama vile vya Monduli CDTI ili kuwa university kuweza kuwa-accommodate vijana waweze kusoma kwa wingi maana elimu inayotolewa na vyuo hivi ni nzuri sana kwa ajili ya Taifa letu?
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi hii adimu. Mbulu Vijijini tuna tatizo linalofanana na Ngara.
Mheshimiwa Spika, tuna Bwawa la Dongobesh ambalo limejengwa zaidi ya shilingi bilioni mbili; na kwa kuwa limekaribia kukamilika na Naibu Waziri ameshafika; kilichobaki ni njia tu ya maji ya kwenda kuwafikia watumiaji. Je, Mheshimiwa Waziri atuambie lini anapeleka fedha kwa ajili ya kumalizia tu hilo bwawa ambalo kimsingi limekamilika bado tu njia ya kwenda kupeleka maji kwa watumiaji?
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Mwenyekiti nikushukuru kwa kunipa nafasi. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri nina swali moja la nyongeza.
Kwa kuwa Daraja la Magala na barabara yetu ya Karatu - Mbulu - Haydom - Sibiti Mheshimiwa Waziri aliahidi kwamba itaanza upembuzi yakinifu, sasa swali, je, barabara hii iko kwenye hatua gani, upembuzi yakinifu na lini anafikiri kwamba itaanza ujenzi?
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu mazuri ya Naibu Waziri, ninayo maswali
mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa tumeleta maombi haya muda mrefu; na vikao hivi vimekaa muda mrefu; na tuna miji miwili ya Dongobesh na Haydom; na kwa kuwa muda umepita, je, Mheshimiwa Waziri yuko tayari sasa
kutuma wataalamu wake kutoka TAMISEMI ili kushirikiana na wataalamu walioko Wilayani kusaidia vigezo hivi kutimia?
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama Mheshimiwa Waziri yuko tayari, je, ni lini sasa atawatuma wataalamu hawa ili
kiu ya wananchi wa Mbulu Vijijini itimie?
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana. Kwa kuwa Mbulu Vijijini katika REA Awamu ya Pili tumepata vijiji viwili tu na sasa Mbulu Vijijini hatuna sub-station tunapata umeme kutoka Katesh na Mheshimiwa Waziri anafahamu, amekuja, tunapata kutoka Babati na Mbulu Mjini. Je, mtatuhakikishiaje sasa katika awamu hii REA itafika maeneo yote ya kata na hasa katika vijiji vya mwanzo vya Mbulu Vijijini?
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana. Pamoja na majibu mazuri sana ya Mheshimiwa Naibu Waziri, nataka nimpe taarifa kwamba katika Kata ya Hayderer kuna mnara wa Airtel umeanzishwa, una miaka miwili, haujamalizika kabisa, uko kwenye foundation. Sasa kwa kuwa Kata za Yaeda Ampa na Tumati zinakaribiana. Je, Wizara iko tayari sasa kujenga mnara katikati ya kata hizi ili angalau katika mnara huu uliotangazwa tender, kata hizi mbili zikapata mawasiliano?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili. Kwa kuwa maeneo mengi mitandao haifiki, maeneo ya Endagichan, Endamasak, Enargatag, Runguamono, Munguhai, Gembak na Gidamba. Serikali sasa ituambie, ina mpango gani tena wa kuingiza vijiji hivi na kata hizi ili angalau basi Jimbo langu lipate mawasiliano? (Makofi)
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa Mheshimiwa Waziri alifika Jimboni kwangu na amekiona Kituo cha Dongobesh na tukaleta ombi la kujengewa theater, je, Mheshimiwa lini sasa theater ile inajengwa ili wananchi wangu wapate matibabu hayo ya upasuaji? Ahsante.
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipatia nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza.
Kwa kuwa pembejeo nyingi mwaka huu mawakala wengi walipewa muda wa kupeleka kwa wakulima na hazikufika kwa wakulima mwaka huu, mawakala wameshapewa na Kamati ile ya pembejeo za Wilaya na sasa pembejeo hazijafika.
Je, Serikali inatuambia nini kwa pembejeo hizi ambazo hazijafika wakulima bado wanasubiri na msimu umeshapita?
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza, Kwa kuwa, Serengeti Boys vijana wale walionesha umahiri mkubwa wa kiwango kile cha soka kinachotakiwa na wakatutangaza sana kule nje na sasa wamerudi. Je, Wizara ina mpango gani sasa kuwaendeleza vijana hawa ili kutokuwa na ile kazi ya zimamoto, wachezaji hawa wakaendelea kufanya vizuri wakati mwingine wa ligi za kimataifa. (Makofi)
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Mradi wa Maji wa Haydom unafanana kabisa na jinsi ambavyo matatizo ya Ngara yalivyo.
Mheshimiwa Naibu Spika, Mradi huu wa Haydom umekaa miaka saba, mkandarasi amechukua pesa na muda wa kukabidhi mradi umeshafika. Mkurugenzi kafanya jitihada mpaka leo mradi haujaisha.
Je, Mheshimiwa Waziri atanisaidiaje sasa kuisaidia Halmashauri yangu ule mradi wa Haydom ukaisha na wananchi wakapata maji?
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza.
Kwa kuwa Serikali ilitoa ahadi ya kujenga Kituo cha Polisi katika bonde la Yaeda Chini na muda umepita sasa na wananchi wanaibiwa mifugo na kutokea mauaji katika lile bonde.
Je, ni lini sasa Serikali itatekeleza ahadi ya kutengeneza Kituo cha Polisi ya Yaeda Chini? (Makofi)
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri na kutaja vizuri vijiji hivi, nina swali la nyongeza. Mwaka jana bajeti yetu ilikuwa shilingi bilioni 2.4 ikarudi na sasa hivi Mheshimiwa Waziri amesema tumetengewa shilingi bilioni, tatizo lililoko pale ni kwamba wakandarasi wanaojenga miradi hiyo baadhi yao hawako site ndiyo maana bajeti mwaka jana imerudi na kadri inavyoendelea hivi bajeti ya mwaka huu kuna wasiwasi wa kurudi. Je, atanisaidiaje kusukuma sasa bajeti hii iishe kwa kuwa wakandarasi wengi hawako site?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, mradi wa Haydom mpaka sasa una tatizo la kwisha pamoja miradi hii ambayo ameitaja mwenyewe ya Arri-Harsha, Barshai, Quantananat na mradi wa Mongahay kuja Tumati. Je, atakuja lini kule na kuwaahidi wananchi wangu ili aweze kuona jinsi ambavyo wakandarasi wanawadanganya kutomaliza miradi na pesa za maendeleo kurudi?
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.
Kwa kuwa Mheshimiwa Rais aliahidi maeneo mengi hasa wakati wa kampeni katika Jimbo la Mbulu Vijijini aliahidi ujenzi wa barabara kilometa tano katika Mji wa Haydom na Dongobesh kilometa mbili. Je, ni lini sasa ahadi hizi za Mheshimiwa Rais zitatekelezwa?
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi hii. Kwa kuwa, Mheshimiwa Naibu Waziri ametoa majibu mazuri ya kueleweka katika maswali haya na katika majibu yake ya msingi. Je, yupo tayari sasa kuandika maelekezo haya yaende kwenye Halmashauri yetu ili hizi Community Centers zifanye kazi yake iliyokusudiwa? (Makofi)
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Kwanza naipongeza Serikali kwa kuandaa mpango huu wa kunusuru kaya maskini. Katika jimbo langu Mheshimiwa Waziri alishawahi kuwa Mkuu wa Wilaya. Je, Mheshimiwa Waziri, kwa sababu anajua Bonde la Yaeda Chini kwa Hadzabe kule wana tatizo hili la umaskini. Je, ataweza kutuongezea angalau Vijiji vile Mungwamono, Eshkeshi na Endagechani tukapata zaidi msaada huu wa TASAF?
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa muda wa kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Hospitali hii ya Haydom kwenye swali la msingi iko katika jimbo langu na inaihudumia Mikoa ya Arusha, Manyara, Mara, Singida na Shinyanga. Kwa kuwa Mheshimiwa Waziri Mkuu alishafika na kutuahidi kwamba atatupatia watumishi zaidi na Mheshimiwa Ummy amefika kwenye hospitali hiyo. Je, lini sasa Serikali inatimiza ile ahadi yake ya kutupatia watumishi katika hospitali hii ambayo inahudumia mikoa mingi niliyoisema?
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa ahadi za Rais, zimekuwa zikitolewa na moja ya Mji wetu wa Haydom, Mbulu na Dongobesh tumeahidiwa kujengwa barabara ya lami kwa kilometa tano. Je, lini Serikali inatekeleza ahadi hii ya Mheshimiwa Rais?
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa muda wa kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa Serikali imefanya feasibility study (upembuzi yakinifu) kwenye malambo mengi na kwa kuwa swali la msingi la Bunda linafanana na Mbulu Vijijini na Mbulu Mjini, je, Serikali ina mpango gani kuyajenga malambo hayo?
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza napenda kueleza masikitiko yangu kuhusiana na mradi huu, mwaka 2014 alikuja Katibu Mkuu wa Chama akadanganywa kuhusu mradi huu. Akaja Waziri Kamwelwe Januari mwaka jana akadanganywa kuhusu mradi huu, mimi nimekuja Ofisi na hao uliowasema mwaka jana Desemba mradi ulikuwa uishe tukadanganywa tena.
Mheshimiwa Naibu Spika, nahitaji muda gani na mara ngapi kuja hapa kuuliza maswali haya na uwongo wa kudanganywa namna hii, wananchi kule umetaja 17,000 hawana maji?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kwa kuwa miradi ya maji katika Jimbo la Mbulu Vijijini iko mingi, nayo hakuna muda ambao umetajwa wa kumalizika na mikataba imeisha, na mimi kule sina fundi kabisa au Mhandisi wa Maji ndani ya Halmashauri yangu.
Je, unanisaidia pamoja na kwamba tutakaa baadae kuhusu ya watumishi katika Wizara hii au katika sekta ya maji?
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Kwa kuwa Serikali imekiri kwamba Wenyeviti wa Vijiji na Vitongoji wanafanya kazi nzuri na imekuwa ikiwategemea kwenye kazi zote na hata kualika mikutano yote ya Wabunge, Madiwani na kufanya kazi kubwa, asilimia 20 ambayo Mheshimiwa Waziri ameitaja katika majibu yake ya msingi haijawahi kupelekwa hata siku moja.
Je, kwa nini sasa Serikali isilete namna nzuri ya kuwalipa moja kwa moja hawa Wenyeviti kwa sababu, ni viongozi ili pasiwe na utaratibu huu wa asilimia ambayo haijawahi kupelekwa tangu wameanza kazi hizi mpaka sasa? (Makofi)
Swali la pili, kwenye swali langu la msingi nilieleza habari ya Madiwani. Madiwani kimsingi wanapata posho ndogo ya shilingi 300,000 na kitu kama sikosei. Je, ni lini sasa mnaongeza posho hizi ili walau basi wafanye kazi nzuri katika chini ya Halmashauri zetu huko Wilayani? (Makofi)
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa swali la msingi linahusiana na usalama wa wasafiri, na kwa kuwa Mheshimiwa Waziri aliahidi kuja maeneo ya Mbulu na kwa kuwa ile barabara ya lami ya kilometa tano ya Hydom na Dongobesh bado. Je, Mheshimiwa Waziri lini sasa atakuja Hydom kuangalia barabara ile ambayo haina usalama kwa wasafiri? Ahsante.
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi hii.
Mheshimiwa Spika, kwa kuwa sasa kutokana na vyeti feki vimeondoa kabisa watumishi wa afya katika zahanati zetu. Je, ni lini hasa hawa watumishi wataenda kuajiriwa yaani wanayo time frame kwa sababu sasa hivi zahanati zina shida katika huduma hii ya afya? Ahsante sana. (Makofi)
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Mwenyekiti ahsante. Mheshimiwa Waziri alifika Hydom akaona matatizo ya maji yaliyoko pale na Dongobesh na certificate ziko Ofisini kwake, je atatusaidiaje sasa Certificates zilipwe kwa haraka ili miradi hii ikamalizika kwa wakati na kama alivyoahidi siku ile ulivyofika Hydom? Ahsante.
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kuniruhusu niulize swali la nyongeza. Kwa kuwa swali hili la Ndanda la Bwawa la Lukuledi linafanana kabisa na bwawa lililopo Mbulu Vijijini, Bwawa la Mangisa ambalo linahudumia Kata ya Yaeda Ampa, Bashay na Gidihim na hali yake kwa kweli inaelekea kuisha kabisa kwa sababu linakauka.
Je, Serikali itatusaidiaje ili hili Bwawa la Mangisa liweze kupatiwa ufumbuzi ili vijiji nilivyovitaja viendelee kupata huduma ya maji?
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Jimbo la Liwale linafanana kabisa na Jimbo Mbulu Vijijini; katika Mji wa Haydom hakuna Mahakama ila kuna kituo kikubwa cha polisi, kwa hiyo, mahubusu inabidi wapelekwe kilometa 86 kutoka Haydom mpaka Mbulu. Je, ni lini sasa pamoja na maombi niliyoleta watajenga Mahakama katika Mji wa Haydom?
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwa kuwa Mheshimiwa Waziri ametoa majibu yake kuhusiana na swali la msingi, je, ahadi hizi zinazotolewa kuhusu barabara hizi hasa ya Mbulu by-pass ambayo inakwenda mpaka Maswa, ni lini sasa Serikali itakuja na mpango wa kuzijenga kwa kiwango cha lami?
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa muda wa kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Spika, tatizo sugu linaloonekana kwenye swali la msingi la Wanging’ombe linafanana kabisa na tatizo sugu la kukosekana maji Mbulu Vijijini. Kwa kuwa Mheshimiwa Waziri amefika katika Jimbo langu, kwanza namshukuru, lakini sasa tumesaini Mkataba na DDCA wa kuchimba visima sita (6), tangu Januari mpaka leo hawaonekani na hawakuchimba visima vile. Waziri atatusaidiaje sasa DDCA waje kuchimba visima ambavyo tumeingia nao mkataba na Halmashauri yangu Jimbo la Mbulu Vijijini? (Makofi)
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, ninayo maswali mawili ya nyongeza:-
Mheshimiwa Spika, swali la kwanza, kwa kuwa katika majibu yake Mheshimiwa Naibu Waziri amesema mkataba ukisainiwa utachukua miezi sita mpaka mnara ujengwe. Nina minara mitatu ambayo kimsingi imejengwa miaka miwili mpaka sasa haijamalizika, kwa mfano; mnara wa Airtel ambao uko Maga, mnara wa Halotel ambao upo Gidilim na mnara wa Halotel mwingine ambao upo Tumati haujakamilika. Je, Mheshimiwa Waziri atasaidiaje minara hii ikamilike kwa sababu Serikali imeweka fedha nyingi ili wananchi wa Mbulu vijijini wapate mawasiliano?
Mheshimiwa Spika, swali la pili, kwa kuwa vijiji ni vingi ambavyo havina mawasiliano, Mheshimiwa Waziri yuko tayari sasa kuja kuonja taste ya kukaa nje ya mawasiliano? Kwa mfano; Getereri, Mewadan, Migo, Harbaghe, Endadug, Eshkesh, Endamasaak, Gorad na Endamilai, yuko tayari sasa kuja ili uone hali ya mawasiliano ilivyo vibaya Mbulu Vijijini ili akatupangia vijiji hivi kupata minara?
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana pamoja na majibu haya ya Serikali Jimbo la Mbulu Vijijini lina Kata 18 na tuna kituo kimoja tu cha afya na kama alivyosema kwamba tumetenga maeneo na wananchi wameshakusanya material yaani mchanga, simenti na wengine tumeanza kujenga, je, Serikali itaongeza nini katika jitihada hizi za wananchi ambao wenyewe wameamua kujenga vituo vya afya? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili kwa kuwa wamekiri kwamba Zahanati ya Hayderer miundombinu yake haifai ili zahanati ile ikahuishwe ikawa kituo cha afya, je, uko tayari sasa kuja pale ili kuangalia namna gani na kutusaidia ili tukapata walau kituo cha pili katika Jimbo la Mbulu Vijijini? (Makofi)
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, ninayo maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naomba nitoe ombi, Hospitali ya Haydom umeme unakatika mara nyingi sana. Kwa hiyo, namwomba Mheshimiwa Waziri atafute namna mbadala ya kusaidia umeme wa Haydom.
Swali sasa kwanza, nimshukuru Mheshimiwa Waziri alifika katika Jimbo la Mbulu Vijijini na kuahidi kwamba umeme utafika Endagichan Masieda, Endagichan Endamila, Yaeda Chini na Eshkeshi; je, ahadi hiyo bado ipo na umeme utafika vijiji hivyo?
Swali la pili; kwa kuwa Hospitali ya Haydom inatumia shilingi milioni 12 kwa ajili ya jenereta za dizeli kwenye vyanzo vya maji, je, Serikali ina mpango gani wa haraka ili kuisaidia hospitali ile kujihudumia vizuri kwa umeme kufika pale katika vyanzo vya maji?
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, ninayo maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara kutoka Babati - Basodesh kuna korongo kubwa sana ambalo linawazuia watoto kwenda shule na kutokana na mvua hizi, ndiyo kabisa hali imekuwa mbaya. Je, Serikali ina mpango gani kuwasaidia watu hawa wa Hanang ili daraja au korongo hili likaweza kujengwa kwa sababu bajeti ya Halmashauri ya Hanang ni ndogo haiwezi kujenga barabara?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, Wilaya ya Hanang na Jimbo la Mbulu Vijijini lilikuwa pacha. Kuna barabara nyingine inayotoka Dongobesh kupitia Maretadu kwenda Haydom hapitiki kabisa kwa sababu ya mvua hizi ambazo zimekuwa nyingi maeneo ya kule Mbulu. Je, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, ina mpango gani wa kusaidia kukarabati barabara hizi ambazo mvua nyingi zimeharibu kabisa?
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Mwenyekiti, nikushukuru sana kwa kunipa nafasi hii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa Jimbo la Mbulu Vijijini na Halmashauri ya Mbulu tumejenga Shule ya Kidato cha Tano na kila kitu tayari na Mheshimiwa Naibu Waziri wa TAMISEMI amekuja kuigagua. Tumetuma maombi na Naibu Waziri anafahamu tunahitaji kuianzisha mwaka huu na kila kitu tayari. Je, kibali hicho kinatoka lini ili mwaka huu watoto hawa waingie shuleni na kusaidia Tanzania ya elimu? (Makofi)
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, changamoto iliyopo Ubungo inafanana kabisa na changamoto iliyopo Jimbo la Mbulu Vijijini. Tuna kituo kimoja tu cha afya Jimbo zima; je, Serikali ina mpango gani sasa wa kutuongezea angalau kituo kimoja ili katika huduma za afya jimboni, pakawa na hali ya kuwasaidia wananchi?
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Kwa kuwa, Mheshimiwa Waziri amesema fedha za TARURA ni kidogo na yeye amepita barabara za Mbulu, hasa Tumati kwenda Martado ni mbaya sana. Je, atatusaidiaje kwenye kipindi hiki ili barabara zile ziweze kutengenezwa na wananchi wakaondoa ile adha ya kupita kwenye barabara ambayo haipitiki kwa sasa?
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Jimbo la Mbulu Vijijini lina uhaba sana wa umeme na Mheshimiwa Waziri amefika. Sasa lini atakuja kuwasha umeme katika Jimbo la Mbulu Vijijini na anafahamu kwa sababu amefika na vijiji vingi havina umeme. Atutajie tu lini atafika Jimbo la Mbulu Vijijini kuwasha umeme? Ahsante.
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Katika swali la msingi la Korogwe Vijijini na hali ya pale inafanana kabisa na Mbulu Vijijini. Barabara ya kutoka Sibiti-Hyadom-Mbulu kuelekea Karatu imeahidiwa kwenye Ilani. Je, ni lini sasa barabara ile itawekewa fedha hasa ukizingatia kwamba huu mwaka unaelekea kuwa wa mwisho?
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwanza nitakuwa mchoyo wa fadhila kama nisiposhukuru kwa kweli kwa utayari wa Serikali kuanzisha Baraza la Ardhi la Wilaya ya Mbulu.

Mheshimiwa Spika, lakini bado, kwa kuwa Mheshimiwa Waziri ameonesha katika majibu yake ya msingi kwamba kuna changamoto hizi za watumishi na kwa kuwa wananchi wa Mbulu bado watakuwa wanakwenda Babati ambaki ni mbali kwa kutafuta hiyo huduma. Je, ni lini sasa ataanzisha Baraza hili ili wananchi hao wasisafiri umbali mrefu?

Mheshimiwa Spika, swali la pili, kwa kuwa wataalam walishakuja kuangalia maeneo ya kuanzisha Baraza hilo na tumeshawapa na jengo na kwa kuwa Wilaya ya Mbulu ni kubwa. Je, Mheshimiwa Waziri yuko tayari sasa kuja kuangalia na kuona eneo gani sahihi la kuanzisha barabara hilo?
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza nafasi kuuliza swali dogo la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa tatizo la umeme limekuwa na kasi na hali ni mbaya katika Jimbo la Mbulu Vijijini na Mheshimiwa Naibu Waziri amefika na vile vijiji alivyoahidi mpaka sasa umeme haujapatikana: Je, atatusaidiaje angalau umeme uweze kupatikana kwenye vijiji alivyoahidi Mbulu Vijijini?
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Jimbo la Mbulu Vijijini lina kituo kimoja tu cha afya, je wananchi wa Maretadu wamejenga sana kituo cha afya cha Maretadu, je, Mheshimiwa Waziriy uko tayari kutusaidia fedha ya kumalizia kituo cha afya Maretadu?
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri, ninayo maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza, kwa kuwa Halmashauri hazina uwezo wa kuwalipa Madiwani na mpaka sasa Madiwani wengi wamekopa posho zao; na kwa kuwa mapato madogo na hali hii inapelekea Madiwani kutolipwa stahiki zao: Je, Serikali ina mpango gani kubadilisha namna hii ili Serikali ilipe toka Hazina kama walivyo Watumishi wengine sasa?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, Wenyeviti wa Vitongoji na Wenyeviti wa Vijiji nao wanafanya kazi sawasawa na Madiwani na Watendaji, hao Ma-VEOs na WEOs wanalipwa mishahara: Je ni lini sasa Serikali itawaona Wenyeviti wa Vijiji na Vitongoji ili kuwalipa posho au mshahara?
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Mwenyikiti, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza, nimpongeze Mheshimiwa Naibu Waziri amefika Jimbo la Mbuli Vijijini na ameona changamoto iliyopo hapo inayofanana na Jimbo la Mlimba. Mheshimiwa Naibu Waziri aliahidi kisima kichimbwe Hyadom na tumeomba shilingi milioni 80 na akaahidi itatumwa. Je, ni lini sasa atatupatia fedha za kuchimba kisima pale Hyadom?
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Zao hili la tumbaku ina changamoto zinazofanana na zao la vitunguu swaumu. Je, mna mpango gani sasa wa kusaidia zao la vitunguu swaumu kama zao la biashara kama ilivyo tumbaku?
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Kwanza nimshukuru sana Mheshimiwa Naibu Waziri amefika na Serikali imetupa fedha ya kujenga hospitali ya wilaya, lakini Mheshimiwa Waziri atakumbuka tulimsimika kama Mzee wa Mbulu Vijijini na akatuahidi atatupatia Kituo cha Afya kile cha Maretadu na maombi yako kwake. Ndugu yangu awaambie watu wa Maretadu je, kituo cha afya kitaletewa fedha lini? Ahsante sana.
MHE. FLATEY G. MASSAY: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa majibu ya Mheshimiwa Waziri yanasema fedha hazipatikani na zitengwe kwenye mapato ya ndani ya Halmashauri ya Karatu; na kwa sababu ukiangalia mapato ya Halmashauri hayana uwezo wa kujenga hata bwawa: Je, Serikali haioni sasa itumie namna mbadala kutokana na hali hii ili kusaidia watu wa Bonde la Eyasi?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; kwa kuwa Wilaya ya Karatu na Wilaya ya Mbulu zilikuwa Wilaya moja na Bonde la Eyasi ni sawasawa na Bonde la Bashai: Je, kuna mpango gani pia wa kusaidia Bonde la Bashai kulipatia fedha ili skimu hii ipate kuendelea?
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Mbulu Vijijini, Mji wa Haydom hauna Mahakama na kutoka Haydom mpaka Mahakama ya Wilaya ni kilomita 86 na tunayo ahadi ya kujengewa Mahakama ya Mwanzo pale. Kutokana na Mbulu tumeshawapa eneo:-

Je, Mheshimiwa Waziri yuko tayari sasa kutenga bajeti ya kujengewa Mahakama ya Mwanzo katika Mji mdogo wa Haydom? (Makofi)
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza Kijiji cha Yaeda Chini, Masieda, Endamilay na Mbullu Vijijini wamesaini mikataba ya kujenga minara TTCL na Holotel wameondoka. Je, ni lini Mheshimiwa Waziri watarudi hawa TTCL kujenga minara Mbullu Vijijini?
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Spika, ahsante, kwa kuwa masoko haya ya vitunguu yamekuwa tatizo karibu maeneo mengi, je, kuna mpango gani sasa kama Serikali kusaidia eneo hilo la msitu wa tembo na maeneo hayo ili wachuuzi wanapokuja basi waweze kuuza vitunguu vyao katika hali ya biashara.

Mheshimiwa Spika, swali la pili, kwa kuwa eneo la Simanjiro ni kubwa sana na walima vitunguu kwa maeneo hayo. Je, unaonaje, uko tayari kushirikiana na Mbunge wa Simanjiro ili kusaidia ujenzi wa soko la vitunguu katika Jimbo la Simanjiro? (Makofi)
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana. Hali ya ukosefu wa maji iliyopo Simanjiro inafanana kabisa na Mbulu Vijijini, Mheshimiwa Naibu Waziri umefika Mbulu Vijijini. Je, miradi hii ya maji na kisima cha Hyadom ulichotoa ahadi nini unatimiza, ahsante. (Makofi)
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante pamoja na mazuri ya Serikali ninayo maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa Bashay tunazalisha vitunguu na tunasindika pale pale kama alivyosema Mheshimiwa Naibu Waziri tunasindika kwa kutumia mashine ile na kwakuwa tuna rojo na oil na tuna powder; je, Mheshimiwa Naibu Waziri haoni kwamba sasa umefika wakati wewe mwenyewe kuja Bashay kuwasaidia wakulima kwa changamoto hii ya uuzwaji wa vitunguu saumu?

Mheshimiwa Mwenyekiti, pili kwa kuwa kuna wanunuzi na walanguzi ambao hawafuati taratibu kama alivyosema kwenye jibu la msingi; je, aoni yeye mwenyewe hataisaidiaje AMCOS ya Bashay kuondokana na uchuuzi huo ambao haufuati vigezo?
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, swali la msingi lipo kwenye Jimbo la Mbulu Mjini na mimi nipo Jimbo la Mbulu Vijijini. Jimbo la Mbulu Vijijini kuna kata 18, Mheshimiwa Waziri umefika umekuta kituo kimoja cha afya kama mke wa Mkristo; unaonaje ndugu yangu? Maretadu wamejenga kituo cha afya wamefika lenta; utatupatia fedha ili walau tuwe na kituo cha pili cha afya?
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Kwanza pamoja na majibu aliyonipa Mheshimiwa Naibu Waziri umeme mahali ambako umekwenda kama alivyosema kwenye majibu ya swali maeneo ya taasisi na visima vya maji vimerukwa. Swali la kwanza kata za Mahitadu, Masieda, Endage Chan, Heda Chini, Getiree, Bashai, Endamillai, Rolward, Endargati, Esheshi, lini zinapata umeme?

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nikushukuru pia umefika kwenye jimbo langu na Mheshimiwa Waziri amefika na iko ahadi ya vijiji 22 kupatiwa umeme mwaka huu. Na leo ni bajeti ya wizara yako je, Mheshimiwa Waziri vijiji hivi na ahadi hii vipo katika bajeti hii au nitegemee nini niwaambie wananchi wa Mbulu Vijijini?
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, umepita Barabara ya Mbulu kwa upande wa Mashariki na Mheshimiwa Naibu Waziri amepita barabara hiyo ya Mbulu kwa upande wa Magharibi. Je, Mheshimiwa Naibu Waziri utuambie sasa na uwaambie wananchi wa Mbulu, barabara ile ya Mbulu – Haydom – Mbulu inajengwa lini kwa kiwango cha lami?
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, Kituo cha Polisi Yaeda Chini kimejengwa na wananchi mpaka kufikia mwisho, kilichobaki ni nyumba za askari. Je, Serikali ipo tayari kuleta fedha za kujenga nyumba za askari ili kituo hicho kifunguliwe?
MHE. FLATEI G. MASSAY:Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali hili muhimu sana la nyongeza. Kwa kuwa amesema katika majibu yake ya msingi kwamba ametenga milioni 401 na ni wazi haiwezi kujenga barabara na Rais ameahidi mara mbili kwenye vipindi vyake viwili, je, haoni sasa aje na mpango mzuri wa kujenga barabara hii kwa kuitengea fedha?
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi kwa kuuliza maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza, kwa kuwa Mheshimiwa Naibu Waziri amekiri mwenyewe kwamba barabara hii ina umuhimu na sasa kwa miaka miwili imekuwa ikiwekwa kwenye bajeti na haikujengwa na amesema imetegwa shilingi bilioni 5, je, atuambie ni lini atatangaza tenda ili barabara hii ianze kujengwa?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kwa kuwa anajua wazi kwamba bilioni 5 haiwezi kujenga barabara na barabara hii iko kwenye Ilani ya uchaguzi mwaka 2015-2020 na 2020-2025 na Mheshimiwa Rais ameahidi kwenye kampeni juzi hapa, je, yupo tayari kuweka fedha kwenye bajeti ya mwaka 2021/2022 ili kumaliza kilomita zingine 20 kufika 70 kufikia eneo la Haydom?
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza, Mbulu Vijijini tumepata minara sita ambayo imejengwa. Mwingine umejengwa 2017, mingine inayofuata imejengwa mpaka juzi hapa lakini sasa minara hii sita haifanyi kazi.

Je, Mheshimiwa Waziri ana mpango kuwafuata au kuwaona wakandarasi ili wawashe minara hii sita ambayo sasa wananchi wanaisubiri mpaka leo? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kwa kuwa amesema kata hizi atazipelekea mawasiliano na kujenga minara; je, kata zilizobaki lini zinakwenda kupata hiyo minara ambayo amekwishaisema?
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, ninalo swali la nyongeza.

Kwa kuwa asilimia hizi zipo kisheria na bado kuna ukakasi katika mgawanyo huu; je, yupo tayari sasa kuja kuona uhalisia wa suala lenyewe katika Jimbo la Mbulu Mji na Vijijini?
MHE. FLATEI I. MASSAY: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Jimbo la Butiama ni majimbo ya zamani kama ilivyo Mbulu Vijijini na changamoto ya umeme karibu zinafanana. Zipo Kata za Masieda, Eda Chini, Eshkesh ambazo Mheshimiwa Waziri naye alikuja akaziona. Je, ni lini sasa maeneo hayo niliyoyataja yatapata umeme?
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Jimbo la Mbulu Vijijini liko juu ya Bonde la Ufa na vijiji vingi sana havina maji, ni kwasababu ya Bonde la Ufa. Na Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan, alifika wakati wa kampeni na kuahidi vijiji vile vitapata maji kutoka kwenye Ziwa la Madunga, Je. Mheshimiwa Waziri, lini ahadi ya Mheshimiwa Rais itatimizwa kwa wananchi hawa kupata maji?
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa vijiji vya Aicho vina vijiji pacha vya Gembak, Kamtananat, Maretadu-Chini, Khaloda, Umburu, je, ni lini vijiji hivi vitachimbiwa visima vya maji?

Mheshimiwa Spika, swali la pili, kwakuwa Wakala wa Maji alishachimba visima sita Jimbo la Mbulu Vijijini katika Kijiji cha Khababi, Labai, Endagichani, N’ghorati, Gendaa Madadu-Juu, je, lini sasa watamalizia kazi ya usambazaji kwa sababu walishamaliza kazi ya uchimbaji? (Makofi)
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Pamoja na majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri wa Elimu, kutoka Mbulu Vijijini sehemu ya Haydom kwenye Mbulu Mjini ni kilometa 90 na kwenda Babati ni zaidi ya kilometa 130. Kwa majibu yake haoni kwamba atakuwa amewaondolea fursa vijana wa Mbulu Vijijini kupata uzoefu na ufundi?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kwa kuwa Mbulu Vijijini hatuna kabisa chuo, je, yuko tayari kutenga fedha sasa ili bajeti ijayo tuweze kupata chuo katika Jimbo la Mbulu Vijijini? (Makofi)
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali. Swali la msingi linafanana kabisa na Jimbo la Mbulu Vijijini na changamoto iliyopo Hanang’ inafanana kwa sababu ilikuwa ni wilaya moja. Barabara ya kutoka Mugitu kuja Hydom iliahidiwa na ipo kwenye Ilani ya Uchaguzi na Mheshimiwa Naibu Waziri aliipita. Je, ni lini tunajengewa kwa kiwango cha lami?
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza; kwanza nionyeshe furaha yangu kwa Serikali kwa kukubali kujenga hii Mahakama ya Mwanzo ya Hydom. Swali, Mahakama ya Wilaya bahati mbaya eneo lake limepitiwa na barabara, je, Wizara ina mpango gani wa kuingiza kwenye bajeti zao ili Mahakama ile ipate kujengwa?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; Waziri amesema Mahakama imeanza kujengwa, je, yupo tayari sasa kwenda Hydom kuona ule ujenzi unaendeleaje ndani ya Jimbo la Mbulu Vijijini?
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipatia nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, nikisikia barabara inayotoka Simiyu kuja Kolandoto ni kama inanitonesha vile kidonda. Mheshimiwa Naibu Waziri ulisema tender itatangazwa; je, lini mnatangaza tender kwa barabara hii?
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kunipatia nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hospitali nyingi za Halmashauri zimebaki bila kumalizika na kwa bahati mbaya Serikali imekuwa na tabia ya kupeleka fedha na mwisho wa bajeti inazichukua. Jimbo la Mbulu Vijijini hospitali imefikia asilimia 95 kumalizika.

Je, ni lini Serikali itarudisha shilingi milioni 300 ilizozichukua ili hospitali ile iweze kumalizika?
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, hiii ndiyo ile barabara ambayo nilitaka kuruka somersault humu ndani. Kwanza niishukuru Serikali kwa kutangaza hizi kilometa 25.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa kwenye bajeti ya Serikali ziko kilometa 50;

Je, ni lini unatangaza tena slot iliyobaki ya kilometa 25?

Mheshimiwa Naibu Spika, na kwa kuwa amesema barabara hii ina kilometa 70,

Je, kilometa 20 zinazobaki point tano atatangaza lini?
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kwa
kuwa mgawanyo wa Halmashauri hizi mbili ulitangazwa kwenye GN ya mwaka 2015, kwa nini sasa ichukuwe miezi mitatu wakati tangazo liko wazi na sheria hii iko wazi sana?
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Kwanza, nimpongeze Naibu Waziri kwa kazi anayofanya na Waziri mwenyewe kwenye Wizara hii. Lakini tatizo lililoko sasa REA inapokwenda kwenye kupeleka umeme vijijini zinapelekwa nguzo 20 tu na kwa sababu ni vijijini, nyumba ziko mbalimbali inatokea nyumba 10 tu zinapata umeme vijijini. Je, REA mnaonaje kwa nini msiongeze nguzo ili nyumba nyingi zikapata nguzo kuliko kupata nguzo hizo 20? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, Waziri amekuwa akitoa taarifa ya wateja wanaotumia unit chini ya 70 kuuziwa unit kwa shilingi 100. Lakini sasa wateja hawa wanauziwa unit kwa shilingi 300. Je, Serikali ina mpango gani wa kutoa taarifa humu ili wananchi hawa wakajua nini hasa, umeme unatakiwa kulipiwa kwa hawa wateja wanaofikisha unit chini ya 70? (Makofi)
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo. Jimbo la Mji Korongo hili la Gunyoda linalosemwa lipo kwenye barabara moja hiyo hiyo kuja Jimbo la Mbulu Vijijini, lipo korongo la Hudaya ambalo lina thamani kubwa ya 1,200,000,000.

Je, Serikali ipo tayari sasa na hii ya Hudaya kuweka kwenye mpango kwa sababu ukiweka hili la Gonyoda la Hudaya utakuwa hujaweka kwenye mpango wa kujengwa barabara hiyo itakuwa haitumiki kabisa.
Je, Waziri yupo tayari na hili ili barabara itumike?
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipatia nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa Serikali imetangaza kilometa 25 nashukuru. Je, bajeti ya sasa ina kilometa 50 ni lini sasa utatangaza kilometa 50 ili kufikia Hospitali ya Hydom barabara ile kujengwa kwa kiwango cha lami?
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Kwanza namshukuru Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan kwa kutupatia shilingi 1,500,000,000 tukajenga Hospitali ya Halmashauri. Sasa hospitali hii inafanya clinic ya watoto pake yake, haina vifaa tiba na hasa madaktari bingwa.

Je, Serikali ina mpango gani wa kuleta vifaa tiba ili hospitali ile ifanye kazi kama ilivyokusudiwa na Serikali?
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, pamoja na majibu mazuri ya Serikali, kwanza nimshukuru sana Mheshimiwa Naibu Waziri, amekuja kuzindua umeme katika Jimbo la Mbulu Vijijini. Lakini nataka nimtaarifu kwamba pamoja na kuja kuzindua ule umeme baada ya kuondoka hakuna kilichoendelea, maana yake mkandarasi hayuko site.

Je, atafanya nini ili walau mkandarasi yule arudi site aweze kuendelea kuunganisha vile vijiji ambavyo mkandarasi amesaini kama mkataba?

Mheshimiwa Mwenyekiti, pili, ziko kata ambazo kwa kweli zina hali mbaya na uliahidi kwamba umeme utafika; ni lini hasa zile kata ambazo wewe mwenyewe alitamka wakati anazindua umeme Mbulu Vijijini zitapata umeme? Maana sasa hivi kama nilivyosema, wakandarasi hawako site. Ahsante.
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza: -
Mheshimiwa Spika, kwanza nimshukuru Naibu Waziri amefika na ametembelea Jimbo la Mbulu Vijijini. Wananchi, wameshajenga vitu vitatu vya afya ambavyo viko hatua mbalimbali; cha Maretadu, Getanyamba na Gembako. Je, Serikali ina mpango gani wa kupeleka fedha katika vituo hivi ili kuvimalizia?
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa Mbulu Vijijini tumeshapata halmashauri na majengo yameshakamilika, na kwa kuwa Mbulu ina halmashauri mbili; je, lini mnatupatia mamlaka ya kuwa na wilaya?
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Kwa kuwa kwenye swali la msingi kulikuwa na hiyo barabara ya Kiberashi na imetengewa Kilometa 25 na tender imeshatangazwa; na Mbulu Vijijini, barabara ya Haydom – Mbulu kulikuwa na tender ya namna hiyo hiyo: -

Je, unataumbaje; tenda hiyo imetangazwa?
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Spika, ahsante nampongeza kwanza Mheshimiwa Waziri kwa kusoma vizuri vijiji hivyo, lakini kuna mnara ambao uko Masqaroda haujawaka mpaka leo na umejengwa kwa gharama kubwa.

Je, lini Mheshimiwa Waziri mnara huu utapata kuwaka ili mawasiliano yakapatikana Jimbo la Mbulu Vijijini?

Pamoja na majibu yako haya na kata ulizotaja na kwa kuwa hakuna uhalisia wa kutosha; je, uko tayari kufuatana na mimi kwenda Jimboni ukayaona haya yote uliyoyasema na majibu yako haya? (Makofi)
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Barabara ya Dongobesh – Dareda, ni lini itajengwa kwa kwiango cha lami?
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Spika, ahsante. Halmashauri ya Mbulu Vijijini haina vifaatiba. Je, Serikali ina mpango gani kuleta vifaatiba kwenye Halmashauri hii?
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Pamoja na majibu haya ya Mheshimiwa Naibu Waziri, ninayo maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, shilingi bilioni mbili aliyoisema kwenye majibu yake ya msingi, ni ndogo sana kutokana na swali lilivyoulizwa wa kila Kijiji kuchimbwa mabwawa.

Je, Serikali ina mpango gani sasa kuongeza bajeti ili maeneo haya anayoyasema yaweze kuchimbwa mabwawa? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; tumeleta maombi ya Mbulu Vijijini kuchimbiwa mabwana katika vijiji vya Gidihim, Eshkesh, Yaeda, Masieda na Endagichan na wewe Naibu Waziri unafahamu: Lini mtatuchimbia hayo mabwawa kama tulivyoomba?
MHE. FLATEI G. MASSAAY: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru Mheshimiwa Naibu Waziri alifika Mbulu Vijijini na Mheshimiwa Waziri kwenye Kata ya Maga. Je, ni lini watatuletea fedha kwa ajili ya kujenga kituo cha afya katika Kata ya Maga?
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Ni nini kinakwamisha ujenzi wa barabara kipande cha Haydom mpaka Labay?
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Jimbo la Mbulu Vijijini ziko sekondari 16 lakini sekondari 11 hatuna vifaa vya maabara ya sayansi.

Je, Mheshimiwa Waziri lini utapeleka vifaa hivyo ili wanafunzi waweze kujifunza vizuri?
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza, pamoja na majibu mazuri ya Serikali ya kutoa elimu ninalo swali hili: -

Mheshimiwa Spika, kwa sababu matukio haya ya uvunjifu wa sheria kwa vitendo hivi ambavyo nimevieleza katika swali la msingi vimeanza kuwa na matukio mengi, na sasa hivi yanapelekea matishio hata kwenye shule zetu za msingi na sekondari: Je, kwa nini Serikali isianzishe kampeni ya kutoa elimu ambayo itakwenda kila maeneo kunusuru Taifa hii na vitendo hivi vya uvunjifu wa sheria?
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa nafasi. Serikali imeahidi kujenga Chuo cha VETA Jimbo la Mbulu Vijijini na tumeandaa ekari 50, na umetuma wawakilishi wako; je, lini mnaanza kujenga Chuo cha VETA Mbulu Vijijini?
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi.

Kwanza niishukuru Serikali kwa kuchimba maji katika Mradi wa Dambia na yanapatikana kwa wingi.

Je, Mheshimiwa Waziri lini mnajenga Mradi ule wa Dambia ambao unaufahamu?
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Spika, ni lini Serikali itajenga Skimu ya Mogahay, Dirimu na Yaeda Chini?
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa mabwawa ambayo yanajengwa na tumeleta kwenye Wizara yako, Bwawa la Mungahai, Dirimu, Yaeda Chini, Masieda, Endagichani, Basodere, Eshdeshi, Getire na Haribapeti.

Je, ni lini unatujengea mabwawa haya ambayo tumeshayaleta kwenye Wizara yako?

Mheshimiwa Spika, swali la pili kwa kuwa Waziri alikuja Haydom na akaahidi kwamba tusubiri wali wa kushiba unaonekana mezani, na akaahidi kisima cha Haydom.

Je, ni lini kinachimbwa?
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Jimbo la Mbulu Vijijini liko ukanda wa juu wa Rift Valley visima vingi vilivyochimbwa na Serikali kwenye Shule na Taasisi nyingi vimekauka. Bahati nzuri tuna Ziwa Basutu tuna ziwa Madunga, je, ni nini mpango wa Serikali wa kupeleka maji kwenye Jimbo hilo?
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Jimbo la Mbulu Vijijini lina uhaba mkubwa wa Afisa Maendeleo ya Jamii pamoja na Walimu wa Sayansi: -

Je, katika mgao huu ukoje? Mtaangalia majimbo haya ya vijijini ili kuweka mgao sawa?
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Kwa kuwa barabara hii ina vipande vingi; je, kipande hiki cha Labay kwenda Hydom na cha Dongobesh kwenda Dareda mnakijenga lini?
Mheshimiwa Spika, swali la pili, kwa kuwa kipande hiki cha Mbulu kuja Garbabi mmeshamuweka mkandarasi pale na yuko site na hamjamlipa advance payment na hajengi tena barabara;

Je, ni lini mnamlipa advance payment ili ajenge barabara au mpaka turuke tena?
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali. Pamoja na Mkandarasi anayetekeleza kazi kwa Jimbo la Mbulu Vijijini kusuasua, sasa ameanza kuweka nguzo katika kila Kijiji, vingine nguzo 12, 13 na 15.

Je, ni kiasi gani cha nguzo kinatakiwa kiwekwe kila Kijiji ili sisi tusimamie?
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Spika, ahsante. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa, Mbulu Vijijini tumeshaanzisha slogan ya kuhamasisha ujenzi wa vituo vya afya mimi na DC Kheri James. Tuna vituo vya afya vya Hayderer, Geterer, Masqaroda, Dinamu, Ladha, Endamilay na Maghang. Je, uko tayari sasa kupeleka fedha hizo ili kuzihamasisha juhudi za wananchi?

Mheshimiwa Spika, swali la pili. Kwa kuwa, Hospitali ya Halmashauri bado haijaisha na inahitaji Shilingi milioni 500 na Kituo cha Hydom hakina jengo la upasuaji: Je, ni lini utapeleka fedha hizo ambazo maombi yetu unayo?
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, mwaka jana tulipitisha bajeti hapa ya kujengwa kipande cha Haydom mpaka Labay kwa kiwango cha lami na bajeti ya Waziri bado hatujapitisha.

Je, ni lini atasaini mkataba ule ili barabara ile ijengwe kipande hiki nilichosema kwa kiwango cha lami au tuje na sarakasi kwa namna nyingine tena kwenye bajeti hii ya Jumatatu?
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa nafasi. Barabara ya Mbulu – Karatu – Haydom – Sibiti mliahidi kujenga kwa kiwango cha lami na kipande hiki cha Mbulu – Haydom, Mheshimiwa Waziri uliahidi utasaini mkataba kabla ya bajeti yako Jumatatu. Hebu tuambie leo na uwambie wananchi wa Mbulu, mkataba huo utasaini lini?
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Spika, ahsante. Je, ni lini Serikali itajenga Soko la Haydom na stendi yake na bahati nzuri Mheshimiwa Naibu Waziri ulifika, ahsante. (Makofi)
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Tumejenga vituo vya afya viwili vya Hydom na Eshkesh, havina vifaa tiba na mmetuletea madaktari: Je, lini mnapeleka vifaa tiba ili wananchi wapate huduma ya utabibu?
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Kwanza namshukuru Naibu Waziri amefika kwenye jimbo langu. Je, minara ya Kata za Eshkesh, Endahagichan, Geterer, Maretadu, Gidarudagaw na Endamiley lini inajengwa?
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Spika, kwa kuwa mmepeleka fedha shilingi milioni 500 na mmechukua milioni 300. Je ni lini inapeleka fedha kwa ajili ya kumaliza kituo cha afya cha Maretadu?

MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Spika, kwa nini Serikali isiweke mfumo kwa wastaafu na ukajulikana kabisa kulikoni kusumbuliwa kuleta barua kila wakati wanapodai madai yao?
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Pamoja na majibu mazuri naomba niweke kumbukumbu sawa ya majina haya. Miqaw, Aidurdagawa, Qamtananat, Endahagichan.

Swali langu la nyongeza, Je, ni lini sasa minara hii unakwenda kuijenga hasa vijiji nilivyotaja na Endahagichan?

Swali la pili, kwa kuwa umefika Jimbo la Mbulu Vijijini na wewe mwenyewe umeona kabisa. Ninaimani hakuna sababu ya kufanya tathmini kwa kuwa umefika mwenyewe na minara haipo katika vijiji nilivyovitaja na iko mbalimbali. Je, ni lini sasa unaweka kwenye mpango huu unaokuja ili vijiji hivi vikapata mawasiliano?

MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali. Mwaka jana Jimbo la Mbulu Vijijini na Jimbo la Babati na Mbulu Mji wakulima waliahidiwa kukopeshwa kulima vitunguu, mahindi katika eneo hilo. Kwa bahati mbaya hawakukopeshwa mpaka msimu umeanza mpka leo.

Je, ni nini kauli ya Serikali kuhusiana na jambo hili?
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa nafasi, pamoja na mkakati uliosema wa kugeuza kilimo kama cha biashara.

Je, kuna mkakati gani kwenye eneo la Yaeda Chini na Eshkesh ambayo ni kame unavyojua kuyageuza maeneo hayo?
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Moja ya sababu za kushuka kwa ufaulu katika maeneo ya vijijini hasa Mbulu Vijijini ni kukosekana kwa nyumba za walimu na sisi tumejenga maboma yamefikia hatua mbalimbali.

Je, ni lini uko tayari kupeleka fedha katika majengo hayo? (Makofi)
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Spika, ahsante. Jimbo la Mbulu vijijini tumepata vituo vya Afya vitatu na tuna upungufu wa watumishi. Je, ni lini mnatuletea watumishi hao?

MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa nafasi. Mbulu Vijijini wananchi wamechanga na wamejenga kwenye Kata ya Geterei OPD kama Kituo cha Afya, na Kata ya Maseda vilevile; je, lini mtapeleka fedha kuunga juhudi za wananchi?
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu ya Mheshimiwa Waziri nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, Kata za Eshkesh, Yaeda Chini na wakati unajibu swali mwaka jana ulisema mwezi wa saba ndiyo watapata umeme lakini sasa umepeleka mwezi wa 12. Je, huoni kwamba utakuwa unatucheleweshea kupata umeme katika Kata hizi?

Mheshimiwa Spika, swali la pili Waziri ametupa vijiji kadhaa ambavyo vitapa umeme kama underline. Kwa sisi wa vijijini, vijiji vyetu lazima umeme upelekwe ndio uweze kupatikana umeme na kama utapeleka umeme katika maeneo ya underline peke yake ni kwamba sisi wa vijijini hatutapata umeme.

Je, Mheshimiwa Waziri uko tayari sasa kubadilisha kauli hii na mpango huu ili kuhakikisha sisi wa vijijini tupate umeme?
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mbulu Vijijini kuna vitongoji 400 na vijiji 76; ulifika Mheshimiwa Waziri ukatoa ahadi vijiji vyote vitapata umeme.

Je, ni lini ahadi yako inatekelezwa? (Makofi)
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali ya nyongeza.

Kwa kuwa, Serikali imekiri kwamba inatafuta fedha kulipa Madiwani na Wenyeviti wa Vijiji na Vitongoji na umeelekeza kwamba Halmashauri ifanye utaratibu huo. Je, uko tayari kuelekeza Halmashauri zote ili hela hizi zilipwe kwenye Mfuko Mkuu ili watu hawa wakapate kulipwa katika bajeti ya mwakani?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, tunampongeza Mheshimiwa Rais kwa sababu ameona na amesikia kilio cha wafanyakazi ameongeza asilimia 23 kwenye mshahara. Je, huoni kwamba sasa ndiyo muhimu kuona kwamba watumishi wengine na hasa hawa niliowataja kwenye asilimia hii wapo?
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Kwanza nishukuru Serikali kwa kujenga Mahakama ya Hydom imekamilika kabisa. Je, ni lini sasa Mheshimiwa Waziri mnafungua Mahakama ile ya Hydom ili ipate kutumika?
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Mbulu Vijijini kuna kata tatu ambazo hazina umeme na vijiji 15. Nakubali majibu ya Mheshimiwa Waziri kwamba REA wameondoka site kutokana kupanda umeme na kupanda gharama za umeme: -

Je, ni lini mnamaliza huo utaratibu wa kukubaliana na hao wakandarasi ili warudi site wakakamilishe mradi huu wa REA?
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza.

Kwanza nishukuru sana Mheshimiwa Rais kutupatia shilingi 711,000,000 kwa Skimu ya Magisa, lakini skimu ile sasa inakwenda kuharibika kwa sababu ya uchakavu na uliniahidi kwamba utakuja kufanya ukarabati.

Je, ni lini utatekeleza ahadi ya Serikali ya kufanya ukarabati kwenye Skimu ya Magisa? (Makofi)
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, Serikali imeahidi kujenga barabara kilometa tano kwenye Mji wa Hyadom; je, ni lini Serikali watatimiza ahadi ya kujenga kilometa hizi za lami?
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Kwanza nishukuru Serikali kwa kujenga Mahakama ya Hydom imekamilika kabisa. Je, ni lini sasa Mheshimiwa Waziri mnafungua Mahakama ile ya Hydom ili ipate kutumika?
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Spika, ahsante, kwa kuwa wananchi wa Haydom wameshawapa eneo la kujenga majengo ya mkandarasi ili aanze kazi na wewe ulikuja kusaini ule mkataba.

Je, ni lini anakuja kujenga yale majengo ili barabara ianze kujengwa ya Haydom – Labay?
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, Barabara ya Orbesh ambayo inatoka kwenye Kata yako kuja Bashneti na kwenda mpaka Haiderere iliahidiwa na Katibu Mkuu kujengwa na sasa hivi hali ni mbaya.

Je, ni lini TARURA itakwenda kujenga barabara ile ili wakulima wapate nafuu ya kuleta mazao yao?
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali, lakini nina maswali mawili. Swali la kwanza; je, Mheshimiwa Waziri yuko tayari kuweka fedha kwenye bajeti ijayo ili Barabara hii ya Ugalla - Kahama ikawa kwenye bajeti kwa uhakika?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; Barabara ya Dareda - Dongobesh aliiweka kwenye mpango wa kujengwa kwa kilomita tisa na mpaka leo haijaanza kujengwa. Je, ni lini ujenzi wa barabara hiyo utaanza?

MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa nafasi.

Jimbo la Mbulu Vijijini Kata ya Yaeda Chini ulikuja Mheshimiwa Waziri ukatuhamasisha tukajenga Kituo cha Polisi, sasa nguvu za wananchi pamoja na mimi tumeshindwa kujenga nyumba za Polisi. Utatusaidiaje kwenye bajeti hii ili nyumba hizo zipate kujengwa?
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Nina maswali mawili ya nyongeza.

Swali la kwanza; kwa kuwa sasa barabara hii ya Mbulu – Garbabi ni kweli Mkandarasi yupo site, lakini ana tatizo hilo la kutolipwa fedha baada ya yeye ku-raise certificate ambayo iko ofisini kwa Mheshimiwa Waziri. Je, lini atalipwa hiyo fedha ili aendelee kuweka au kumalizia barabara hii ya Garbabi kwenda Mbulu?

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine, nashukuru kwanza Mheshimiwa Naibu Waziri alikuwepo katika kusaini Mkataba wa Barabara ya kutoka Haydom kuja Labay. Sasa ni miezi sita, tumesaini tarehe 25 Mei, 2023. Je, ni lini sasa barabara hii itaanza kujengwa kwa kiwango cha lami ili wananchi waweze kupita? (Makofi)

Hon. Dr. Tulia Ackson

Speaker

Legislative Role

Profile

Ask the Speaker / Comments

Ms. Nenelwa J. Mwihambi

Clerk of the National Assembly

Legislative Role

Profile

Ask the Clerk / Comments

View All MP's