Parliament of Tanzania

Questions By: Hon. Zuberi Mohamedi Kuchauka

Supplementary Questions
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kuniona. Migogoro ya ardhi kati ya hifadhi zetu na wananchi wanaozunguka hifadhi imekuwa ni migogoro ya muda mrefu na imeenea katika nchi nzima. Katika Jimbo langu la Liwale sisi ni miongoni mwa tuliozungukwa na Hifadhi ya Selous.
Mheshimiwa Naibu Spika, tunao mgogoro mkubwa sana kati ya hifadhi ya Selous pamoja na Kijiji cha Kikulyungu wakigombea bwawa la Kihurumila. Mgogoro huu umeshapoteza maisha ya watu kwa muda mrefu na hata Mbunge aliyepita wa Jimbo la Liwale mgogoro huu umemfanya asirudi tena Bungeni pale alipotamka Bungeni kwamba anasikia watu wamefariki katika bwawa hilo, badala ya yeye kwenda kujiridhisha na kuangalia hali halisi ya mgogoro huu.
Mheshimiwa Naibu Spika, ni lini basi Mheshimiwa Waziri atashiriki katika kutatua mgogoro huu ili maisha ya watu wa Liwale yasiendelee kupotea wakigombea bwawa la Kihurumila? Naomba majibu.
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Nasikitika sana kwa majibu ya kukatisha tamaa yaliyotolewa na Mheshimiwa Naibu Waziri. Wilaya ya Liwale ina umri wa miaka 41 leo, Serikali ya Chama cha Mapinduzi inasema haina mpango wowote wa kujenga Kituo cha Polisi pale, anaposema kwamba ni zaidi ya Wilaya 65, sidhani kama hizi Wilaya nyingine ambazo anazi-include yeye zina umri wa miaka 40. Wilaya ya Liwale ina jumla ya kilometa 66,000 na hizi tarafa anazozisema zipo umbali wa kilometa zaidi ya 60 kutoka Liwale Mjini… (Makofi)
SPIKA: Mheshimiwa Kuchauka, swali sasa!
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Spika, najenga hoja. Wilaya ya Liwale mpaka leo, nimetembelea kile kituo, mafaili yale wanafunika na maturubai, lile jengo walilopanga la mtu binafsi linavuja. Sasa ninachoomba, nipewe time frame, ni lini Kituo cha Polisi Liwale kitajengwa. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, vilevile katika Tarafa ya Kibutuka, ndiyo tarafa inayoongoza kwa ufuta na wafanyabiashara wakubwa wako pale na Kata ya Lilombe sasa hivi kuna machimbo na wafanyabiashara wengi wako pale, ni lini Kata hizi zitajengewa vituo vya Polisi?
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, natoa shukrani zangu kwa Mheshimiwa Waziri kwa majibu ya kutia matumaini. Lakini nataka ieleweke kwamba Wilaya ile ya Liwale ipo mbali sana na makao makuu ya Mkoa, Wilaya ya Liwale haina usafiri, haina barabara za kutosha yaani za kuaminika, Wilaya ya Liwale haina mtandao wa simu unaoaminika, Wilaya ya Liwale haina usikivu wa redio. Sasa muone jinsi Wilaya hii ilivyo kisiwani, hawa ni miongoni mwa walipa kodi wa nchi hii, sijui kama kodi zao watanufaika nazo vipi? Nashukuru kwa jibu la kwanza nimepata timeframe na mimi nitafuatilia kuhakikisha hii timeframe inafikiwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kwa swali la pili napata wasiwasi, nimepata tu majibu ya moja kwa moja. Nahitaji kujua ni lini Redio Tanzania itasikika Liwale? Hapa nimepewa tu majibu ya jumla jumla. Mwisho kabisa hapa amesema kwamba mpango wa muda mrefu sasa hata huo mpango wa muda mfupi nao haujatajwa, huo ni wa lini? Naomba nipatiwe majibu.
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali moja la nyongeza. Matatizo yaliyopo kwenye hii Wilaya ya Busanda yanafanana kabisa na yale yaliyoko katika Wilaya ya Liwale. Wilaya ya Liwale hatuna Chuo cha Ufundi, je, ni lini Serikali itatujengea Chuo cha Ufundi Wilayani Liwale?
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Naibu spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi niulize swali la nyongeza. Kukamilika kwa daraja la Mto Kilombero ni wazi kwamba sasa Mkoa wa Morogoro unafunguliwa kibiashara. Nini mipango ya Serikali kuunganisha Mkoa wa Morogoro na Mkoa wa Lindi kwa barabara inayopitia kutoka Liwale kuelekea Morogoro? Ahsante.
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa swali la nyongeza. Kwa kuwa, tatizo kubwa la miradi hii ya umwagiliaji ni ule upembuzi yakinifu sijui na usanifu. Kwa sababu, katika Jimbo langu la Liwale kuna Mradi wa Umwagiliaji wa Ngongowele umetumia zaidi ya shilingi bilioni nne na mradi ule sasa hivi uko grounded, hautegemei tena kufufuka. Je, ni nini kauli ya Serikali juu ya pesa zile zilizopotea pale na hatima ya mradi ule?
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante.
Wilaya ya Liwale iko katika Mkoa wa Lindi na ndiyo Wilaya pekee ambayo bado mpaka leo hii inatumia umeme wa mafuta na mashine zile tumezitoa Rufiji, mashine zile zimechoka. Nini kauli ya Serikali kuipatia umeme wa gesi Wilaya ya Liwale ili tuweze kuwa na umeme wa uhakika?
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.
Sambamba na Sheria ya Ndoa, Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania iliridhia Sera ya Wazee tangu mwaka 2003. Ni lini Serikali italeta sheria kamili ya wazee ili waweze kutambuliwa katika nchi yetu?
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi kuuliza swali moja la nyongeza. Barabara ya Nangurukulu – Liwale, Nachingwea – Liwale, ni barabara ambazo zimo kwenye Ilani ya Chama cha Mapinduzi, lakini mara nyingi nimekuwa nikiuliza barabara hizi, naambiwa itajengwa, itajengwa; sasa wana-Liwale wanataka kusikia ni lini barabara hizi zitaingia kwenye upembuzi yakinifu na hatimaye kujengwa kwa kiwango cha lami? Ahsante sana.
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Niseme tu nasikitika kwa majibu ambayo ni rahisi, majibu mafupi, majibu ambayo hayaoneshi matumaini.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama ambavyo Mheshimiwa Naibu Waziri...
...anasema ubinafsishaji wa matawi 22 yaliyokuwa National Milling tumepata shilingi bilioni 7.4, ni masikitiko makubwa sana; na hii inaonyesha moja kwa moja kwamba sisi huu umasikini umetuandama. kwa sababu kama tunaweza tukatupa…
..ni masikitiko makubwa sana. Msheshimiwa Mwenyekiti, najenga hoja.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna matawi kama Plot 33, Plot 5, Tangold yale matawi sasa hivi yote ni ma-godawn. Watu walionunua matawi ya National Milling ambayo yanafanya kazi ni Bakheresa na Mohamed Enterprises peke yake, lakini matawi mengine yote yaliyobaki yamekuwa ma-godawn na ninyi mnasema mnaenda kwenye viwanda, mimi hapa sijapata kuelewa. Nini hatima ya hayo mashirika ambayo sasa hivi ni ma- godawn badala ya kuwa viwanda? (Makofi)
(b) Kwanza niseme wazi kwamba na mimi ni mmoja kwenye taaluma hii ya usindikaji wa nafaka. Nimefanya kazi National Milling si chini ya miaka 10. Kwa upande wa Kurasini mnamo tarehe 31 Aprili, 2005 waliletewa barua aliyekuwa Meneja pale kwamba kiwanda hicho akabidhiwe Mohamed Enterprises anayekaribia kununua, alikabidhiwa tu kwa sababu anakaribia kununua. Si hivyo tu, wafanyakazi waliokuwepo pale mpaka leo hii wanaidai Serikali hii zaidi ya shilingi milioni 234.3, bado hatima yao haieleweki na kesi imekwisha. Vilevile si hivyo tu, tarehe 20…Hazina wameitwa mahakamani hawataki kwenda, nini hatima ya wafanyakazi wale?
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi niulize swali la nyongeza kuhusu Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano. Nimekuwa nikisimama hapa mara nyingi naongelea Barabara ya Nangurukuru – Liwale na Barabara ya Nachingwea – Liwale. Majibu ninayoyapata ni kwamba barabara hizi zitajengwa katika kipindi hiki cha miaka mitano, lakini barabara hizo sasa hivi hazipitikia kutokana na mvua za masika zilizokatika sasa hivi. Je, nini commitment ya Serikali kwa kuwaokoa hawa Wanaliwale ili waweze kupata barabara inayopitika masika na kiangazi? Ahsante sana. (Makofi)
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi nami niulize swali la nyongeza. Kwa kuwa dhamira ya Serikali ya Awamu ya Tano ni kuelekea kwenye nchi za viwanda; na ninavyofahamu mimi ili twende huko, lengo kubwa ni kuchakata mazao yanayolimwa hapa nchini; lakini kama ambavyo swali namba 206 lilivyojibiwa, sijaona mkakati unaowekwa kwenye zao la ufuta. Ni namna gani Serikali imejipanga kutangaza ili tupate wawekezaji kwenye kusindika mazao ya ufuta?
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Mheshimiwa Waziri anasema kwamba mpango mkakati mmojawapo ni kutangaza kuingiza hiyo tovuti na filamu. Hapa swali lilikuwa linataka kujua mkakati thabiti wenye dhamira ya kweli kwa sababu hapo wanaposema, hata barabara ya kufika kwenye hivyo vivutio hakuna. Sasa huu mkakati, hata hao watu unaoingiza kwenye filamu, watafikaje kule Kilwa ambapo kwenye hivi vivutio hamna barabara. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, siyo hivyo tu, nataka nimwambie Mheshimiwa Waziri kwamba Pwani ya Afrika Mashariki ni mahali ambapo kwanza walikuwa na currency yao, yaani walikuwa na pesa yao; ni Kilwa, lakini haya yote watu hawayajui.
Mheshimiwa Naibu Spika, vile vile kwa mfano, ukiangalia Vita ya Majimaji; asili ya vita hii ni Kilwa, lakini makumbusho ya Vita ya Majimaji yako Songea. Sasa Wananchi wa Kilwa walitaka waone, Serikali inafanya taratibu gani kuirudisha Vita ya Majimaji Kilwa na kuitangaza Kilwa kama sehemu ya Utalii? Hilo ni swali la kwanza.(Kicheko)
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi na mimi niulize swali la nyongeza.
Kama ambavyo Halmashauri ya Itilima ilivyokuwa na tatizo la Hospitali ya Wilaya, Wilaya ya Liwale ni Wilaya ya zamani sana na lile jengo lake la Hospitali ya Wilaya limeshachakaa na limezidiwa uwezo. Kwa kutambua hilo Halmashauri yetu ya Wilaya ya Liwale imetenga eneo kama hekari 50 hivi kwaili ya mradi wa hospitali mpya ya Wilaya ya Liwale. Je, Serikali ipo tayari kutuunga mkono katika mradi huu?
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ili niulize swali la nyongeza. Kunakuwa na matatizo mengi ya miradi mingi ya maji nchini ambayo haikamiliki kutokana na matatizo ya fedha, lakini mara nyingi tukiuliza hapa, nakumbuka Bunge lililopita, Mheshimiwa Naibu Waziri wa Wizara hii alikuwa anasema kwamba Wakurugenzi wetu wakamilishe taratibu za manunuzi, pesa zipo kwenye Wizara.
Mheshimiwa Naibu Spika, nilipokwenda kwenye halmashauri yangu kwa mfano, nilienda kuulizia suala hili wakasema wameshaandika maandiko mengi kupeleka Wizarani, lakini mpaka leo hawajaletewa hizo pesa na miradi mingi imekwama . Sasa naomba kupata Kauli ya Serikali; ni nini Kauli ya Serikali kwa miradi ile ya maji iliyokwama kwenye halmashauri zetu mbalimbali hapa nchini?
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Spika,ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Spika, kutokana na kuharibikaharibika kwa mara kwa mara kwa kinu cha gesi pale Kilwa na kutokana na uchakavu wa mitambo ile, hitajio la Wilaya za Kilwa, Lindi pamoja na Liwale, I mean Kilwa pamoja na Rufiji pamoja na Liwale kuingizwa kwenye Gridi ya Taifa ni muhimu sana.
Mheshimiwa Spika, sasa naomba Waziri atueleze hapa ni nini kinachelewesha wilaya hizi kuongizwa kwenye Gridi ya Taifa kwa sababu ya uchakavu wa mitambo ya Kilwa kunafanya umeme usiwe wa uhakika katika Wilaya hizi tatu? Ahsante sana.
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.
Kwa sababu tunataka tuingie kwenye Tanzania ya viwanda na Tanzania ya viwanda ni lazima iende sambamba na uwekezaji kwenye ardhi lakini uwekezaji kwenye ardhi unakumbwa na matatizo makubwa. Tatizo la kwanza vijiji vyetu vingi havijaingia kwenye matumizi bora ya ardhi, matokeo yake mwekezaji anakosa nafasi na hata pale ambapo vijiji vimeshaingia kwenye matumizi bora ya ardhi kuna tatizo kwenye Makamishna wa Kanda katika upatikanaji wa ardhi lakini sio hivyo tu, hata kwenye Ofisi ya Rais ambapo nako kuna matatizo...
Je, nini kauli ya Serikali kwa wawekezaji wanaohangaika kutafuta ardhi ya kufanya uwekezaji katika kilimo? (Makofi)
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama ilivyo kwenye matatizo ya mazao ya mbaazi vivyo hivyo kuna tatizo la zao la ufuta, lakini tatizo kubwa la mazao haya ni Bodi ya Mazao Mchanganyiko. Ni nini kauli ya Serikali katika kuiboresha hii Bodi ya Mazao Mchanganyiko iwe na mipango endelevu ya kuendeleza haya mazao ili wananchi wetu waweze kupata soko la uhakika?
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kuniona na kunipa nafasi kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote, nitoe shukrani kwa Serikali, wanasema kwamba usiposhukuru kwa kidogo basi hata kikubwa hutaweza kupata, kwa sababu nililalamika hapa sina hata kituo cha afya kimoja, lakini sasa hivi nimepewa pesa kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha afya cha pili na pesa za kuboresha kile kituo cha afya cha zamani ambacho nilisema ni mfu, kwa hiyo nasema ahsanteni sana. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini bado Hospitali ya Wilaya ya Liwale ina tatizo la nursing officers na mpiga picha wa x-ray. Ni lini Serikali itaweza kutupatia watumishi hawa wa kada mbili; mpiga picha wa x-ray na nursing officers? Ahsante sana. (Makofi)
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi na mimi nipate kuuliza swali la nyongeza.
Matatizo ya mawasiliano katika Halimashauri ya Wilaya ya Liwale na Wilaya nzima ile ni makubwa sana na ujio wa Kampuni ya Halotel pamoja na TTCL tuliona kwamba inaweza kuwa kama mkombozi kwa ajili ya mawasiliano katika Halmashauri ile. Kwa bahati mbaya zaidi, miradi ambayo ilikuwa tayari wananchi wametoa maeneo yao kwa ajili ya kujenga minara katika Kata za Mirui, Ngongowele, Mpigamiti, Mkutano, Ndapata na Igombe na Mtunguni miradi ile yote imesimama hatuwaoni tena wale Halotel…
Mheshimiwa Mwenyekiti, nini kauli ya Serikali juu ya kukwama kwa miradi hii katika hizo Kata nilizozitaja?
MHE. ZUBER M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi nami niulize swali la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, vijiji vya Mpigamiti pamoja na Kikulyungu ni vijiji ambavyo vimepakana na hifadhi ya Selous katika Halmashauri ya Wilaya ya Liwale, lakini kuna mgogoro mkubwa sana wa ardhi kati ya Kikulyungu pamoja na Selous.
Je, ni lini Mheshimiwa Waziri utaweza kutatua mgogoro huu ambao umedumu zaidi ya miaka 10 na watu tayari washapoteza maisha?
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Moja ya sababu zinazofanya ucheleweshwaji wa malipo ya korosho ni pamoja na tamko la Mkuu wa Mkoa wa Mtwara, alitamka kwamba korosho zote za Mkoa wa Lindi na Mtwara zipitie Bandari ya Mtwara kitendo ambacho bandari ya Mtwara ilishindwa kusafirisha korosho hizo kwa wakati na wanunuzi wakaacha kulipa kwa sababu korosho zao mpaka ziingie kwenye maji ndipo waendelee kufanya malipo. Mheshimiwa Mwenyekiti, siyo hivyo tu, sababu ya pili; ni kwamba hata hayo makampuni mnayosema kwamba mnayadhibiti pale ambapo yanakuwa yanachelewesha kulipa lakini bado kuna mtindo wa hayo makampuni kubadilisha majina. Unalifutia jina kampuni hili, mwenye kampuni ni yule yule anatengeneza kampuni nyingine…
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Je, Serikali inatoa kauli gani namna ya kukabiliana na matatizo hayo?
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.
Kutokamilika kwa miradi ya maji katika Halmashauri zetu kumekuwa ni tatizo sugu, niliwahi kumuuliza Mheshimiwa Naibu Waziri wakati huo ambaye sasa ndiyo Waziri alisema pesa Wizarani zipo ila watu wapeleke certificate. Ninasikitika kumwambia kwamba hapa ninayo makabrashi ambayo ni copy ya hizo certificate ambazo zimeshafika kwenye Wizara yake sasa ni zaidi ya mwaka mzima hizo pesa hazijawahi kutolewa, na kuna miradi kadhaa katika vijiji vya Kipule, Ngongowele pamoja na Mikunya.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kauli ya Serikali ni lini miradi hii itakamilika ili wananchi wa vijiji hivi waweze kupata maji. (Makofi)
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa utangulizi tu nipende kusema kwamba jibu ni jibu hata kama halikutosha kwa muuliza swali huwa ni jibu. Hii bla bla yote iliyotolewa kwenye aya ya pili mimi sioni kama ni jibu linalijitosheleza kwa sababu mradi huu umehujumiwa kwa kiwango kikubwa sana. Kwenye ziara ya Mheshimiwa Waziri Mkuu alipokuja kwenye Jimbo langu, mimi na Mkuu wetu wa Wilaya na Mkurugenzi wetu wa Halmashauri tulipanga ziara Mheshimiwa Waziri Mkuu akakague aone nini kimefanyika kwenye mradi ule. Hata hivyo, hao watu wa Kanda wa Umwagiliaji wakishirikiana na Mkuu wa Mkoa wa Lindi waliifuta hiyo ziara katika mazingira yasiyofahamika na ni kwa sababu tu huu mradi umehujumiwa kwa kiwango kikubwa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza, je, Serikali iko tayari sasa kama hii awamu wanayotaka kuisema awamu ya tatu, kutukabidhi Halmashauri mradi huu tuutekeleze badala ya kuwaachia hawa watu wa Kanda ambao wamekuwa wakiuhujumu mradi huu? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, je, Mheshimiwa Waziri yupo tayari kutembelea mradi huu ili aangalie pesa hizi shilingi milioni 746 za Serikali ambavyo zimepotea bila sababu zozote zile za msingi? (Makofi)
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Ninachotaka kujua TARURA ni chombo ambaco kimeundwa hivi karibuni, nataka kujua TARURA sasa kwa sababu barabara wanazoshughulikia ni zile zilikuwa zinashughulikiwa na Halmashauri chini ya Madiwani. Je, hiki chombo sasa kinasimamiwa na mamlaka gani kwa niaba ya wananchi, kwa sababu hawaingii kwenye Baraza la Madiwani?
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Kwanza nataka kumshukuru Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu ya kuridhisha.
Lakini kwa niaba ya wananchi wa Dar es Salaam na hasa wa hili eneo la Kawe, huu mgogoro ni wa muda mrefu sana. Kama ambavyo Naibu Waziri anasema anataka kushirikisha sasa jamii kuona namna ya kuwapa fidia wale wamiliki wa mwanzo mimi naomba kwamba ushughulikiaji wa suala hili Mheshimiwa Naibu Waziri bado ni mdogo sana. Sasa nataka tu nipate majibu ya uhakika kwamba Mheshimiwa Naibu Wziri unawahakikishia nini watu wa Kawe juu ya upatikanaji wa ardhi ili waweze kuondokana na adha hii ya upatikanaji wa ardhi?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, tatizo hili la migogoro ya ardhi Mheshimiwa Waziri mwenye dhamana hii alishawahi kutuletea taarifa Wabunge hapa Bungeni kwamba tuorodheshe migogoro mingi kwenye majimbo yetu, lakini asilimia kubwa ya migogoro ile bado haijashughulikiwa, nini kauli ya Serikali juu ya kushughulikia migogoro ya ardhi nchini? (Makofi)
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Ahsante Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali moja la nyongeza. Kama ambavyo Naibu Waziri ameitambua Kitowelo kwamba atatenga kwa ajili ya wachimbaji wadogo.
Vilevile eneo hilo liko ndani ya kijiji cha Lilombe, lakini tangu uchimbaji huu mdogo umeanza kijiji kile cha Lilombe hakijawahi kunufaika kwa lolote na Halmashauri nzima ya Liwale haijawahi kunufaika kwa lolote, kwa sababu vibali vya uchimbaji vinatoka Kanda, halafu wale wakitoka kwenye Kanda wanaingia moja kwa moja vijijini wanaanza uchimbaji.
Mheshimiwa Mwenyekiti, je, nini kauli ya Serikali juu ya manufaa wanayoyapata vile vijiji ambavyo tayari machimbo hayo yapo? (Makofi)
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwanza kabisa ninasikitika tu kwamba hili swali halijajibiwa; kwa sababu hapa nilizopewa ni story tu, nimeona hapa zimepatikana story tu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sababu tatizo letu Liwale ni kwamba Mji wa Liwale unategemea maji kutoka Mto Liwale na Mto Liwale sasa umekauka, kwa hiyo, shida yetu ni kutafuta chanzo cha pili mbadala cha maji. Sasa hapa Mheshimiwa Waziri anasema kwamba hatua ya awali yaani kwa muda mfupi wanakarabati matenki, wanakarabati chanzo cha maji na wananunua dira. Sasa unakarabati chanzo cha maji, unakarabati vipi? Mto umekauka unaukarabati vipi? Matenki unayokarabati unataka uweke nini na mita unazokwenda kufunga unataka zitoe nini? Hapo naona swali bado halijajibiwa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, siyo hivyo tu, katika muda mrefu wanasema wametenga shilingi bilioni 3.5 lakini hizi shilingi bilioni 3.5 kuna Halmashauri 14 zimewekwa hapa. Kwa nini sasa Mheshimiwa Waziri hajatenganisha kujua kwamba Halmashauri fulani ina kiasi gani maana kuzifumba hapa ni nini?

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la pili ninalouliza mo wamba, scheme ya Umwagiliaji ya Ngongowele itakamilika nini? Nimepewa story tu. Sasa nataka nijue hatua gani imefikiwa ili tuweze kupata chanzo cha maji mbadala kwa Mji wa Liwale, hilo ndio swali ambalo naomba niulize. Vilvile naomba nirudie, tunaomba mradi wa Ngongowele ukamilike. Je, Mheshimiwa Waziri upo tayari kwenda na mimi kuangalia huo mradi?
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi niulize swali la nyongeza. Kama ilivyo Mahakama ya Kasulu ni chakavu, lakini Wilaya ya Liwale ni Wilaya ambayo ina umri wa miaka 42 mpaka leo haina jengo la Mahakama. Jengo linalotumiwa ni lile jengo ambalo lilikuwa Mahakama ya Mwanzo ambalo sasa hivi limechakaa limefika mahali ambapo mafaili yanafunikwa na maturubai. Je, Mheshimiwa Waziri upo tayari kuijengea Liwale Mahakama ya Wilaya?
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali moja la nyongeza. Halmashauri ya Wilaya ya Liwale ina misitu mikubwa miwili; kuna ule msitu ambao unahifadhiliwa na WMA (Ustawi wa Vijiji) na ule msitu wa Serikali ambao ni Msitu wa Nyera, Kipelele. Msitu huu ni msitu ambao tumeurithi kutoka enzi za Wakoloni, lakini mpaka leo harversting plan ya msitu ule haijatoka. Nini kauli ya Serikali kuharakisha harvesting plan ya msitu huu ili wananchi waweze kupata faida ya kuwepo kwa msitu huu wa Nyera, Kipelele? (Makofi)
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Mheshimiwa Waziri anasema kwamba mpango mkakati mmojawapo ni kutangaza kuingiza hiyo tovuti na filamu. Hapa swali lilikuwa linataka kujua mkakati thabiti wenye dhamira ya kweli kwa sababu hapo wanaposema, hata barabara ya kufika kwenye hivyo vivutio hakuna. Sasa huu mkakati, hata hao watu unaoingiza kwenye filamu, watafikaje kule Kilwa ambapo kwenye hivi vivutio hamna barabara. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, siyo hivyo tu, nataka nimwambie Mheshimiwa Waziri kwamba Pwani ya Afrika Mashariki ni mahali ambapo kwanza walikuwa na currency yao, yaani walikuwa na pesa yao; ni Kilwa, lakini haya yote watu hawayajui.
Mheshimiwa Naibu Spika, vile vile kwa mfano, ukiangalia Vita ya Majimaji; asili ya vita hii ni Kilwa, lakini makumbusho ya Vita ya Majimaji yako Songea. Sasa Wananchi wa Kilwa walitaka waone, Serikali inafanya taratibu gani kuirudisha Vita ya Majimaji Kilwa na kuitangaza Kilwa kama sehemu ya Utalii? Hilo ni swali la kwanza. (Kicheko)
Swali la pili...
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa swali la nyongeza. Halmashauri ya Mji wa Liwale ulikuwa na miradi ya maji wa vijiji 10, lakini mpaka sasa hivi vijiji vyote 10 vimeshatobolewa lakini vijiji vilivyofungwa miundombinu ya maji ni vijiji vitatu tu. Vijiji ambavyo sasa hivi vina maji ni Kijiji cha Mpigamiti, Barikiwa, pamoja na Namiu. Je, vile vijiji saba vilivyobaki lini watatoa pesa kwa ajili ya kujenga miundombinu kumalizia vile visima ambavyo tayari vimeshatobolewa?
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi niulize swali moja la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Wilaya ya Liwale yenye kata 20 na kituo kimoja cha aya haina gari ya wagonjwa. Shida tuliyonayo ni kubwa sana ukizingatia mtawanyiko wa kata zetu zile pale Wilaya ya Liwale mwenyewe Mheshimiwa Naibu Waziri ni shahidi, umefika, umeona jinsi shida ya Wilaya ya Liwale ilivyo juu ya kupata gari la wagonjwa. Ni lini sasa Serikali itatupatia gari la wagonjwa katika Hospitali yetu ya Wilaya ya Liwale? (Makofi)
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mji wa Liwale ni mji unaokua kwa kasi sana hasa baada ya korosho kufanya vizuri na kuna mradi wa kutafuta chanzo cha maji mbadala kwa Mji wa Liwale. Mradi ule sasa hivi una zaidi ya miaka minne umesimama. Nini kauli ya Serikali juu ya kuwapatia maji wananchi wa Mji wa Liwale? (Makofi)
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza; wakati wa upanuzi wa Kiwanda cha Umeme cha Liwale wakati wanapanua ile plant yao, walichukua mashamba ya wananchi ambapo mpaka leo hii zaidi ya miaka mitano wananchi wale hawajui hatima ya malipo yao. Nini kauli ya Serikali namna ya kuwalipa wale wananchi mashamba yao?
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi kuuliza swali la nyongeza. Awali naomba uelewe kwamba haya maswali tunayoyauliza hapa na sisi wawakilishi yanaulizwa kwa niaba ya wananchi wetu, kwa hiyo, hii ni kero ya wananchi. Sasa tunapopata majibu yasiyoridisha na majibu ambayo yana mkanganyiko, tunapata mashaka sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mwezi wa Septemba, 2017 niuliza swali hili na Mheshimiwa Waziri mwenye dhamana alitumia sekunde zisizozidi tano akaniambia Mahakama ya Wilaya ya Liwale itajengwa mwaka 2018. Sasa leo hii naambiwa itajengwa kwenye bajeti ya 2018/2019. Kwa nini wanakuwa na majibu ya kudanganya wananchi wakati sisi ni wawakilishi wao na hizi ni kero wanatupa ili wapate majibu? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa naomba niulize maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza…
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, sambamba na Mahakama ya Wilaya ambayo nadanganywa kwamba itajengwa kwenye mwaka ujao wa bajeti, je, Serikali ina mpango gani kujenga Mahakama za Mwanzo katika Tarafa za Kibutuka na Makata? (Makofi)
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Pamoja na majibu yanayoridhisha ya Mheshimiwa Waziri, mgogoro huu, kama mwenyewe anavyokiri ni wa muda mrefu na mimi nimeshakwenda kwa Mheshimiwa Waziri wa Ardhi akaniambia kwamba mgogoro huu bado uko kwenye ngazi ya mkoa, watakaposhindwa ngazi ya mkoa watauleta Wizarani. Nimekwenda kwa Mkuu wa Mkoa ameniambia kwamba yeye ameshauandikia Wizarani kwa maana ya kwamba wameshashindwa.
Mheshimiwa Spika, hata h ivyo, mimi mwenyewe binafsi nimemuandikia Mheshimiwa Waziri kumjulisha mgogoro huu mpaka sasa hivi sijapata majibu yoyote. Sasa kutokana na huu mkanganyiko wa kauli za Serikali, Mkuu wa Mkoa anasema hili na Waziri anasema lingine, nini kauli ya Serikali juu ya mgogoro huu yaani nani kati yao yuko sahihi?
Mheshimiwa Spika, swali la pili, anasema mgogoro huu utashughulikiwa mwaka huu wa 2018/2019. Je, Mheshimiwa Waziri, yuko tayari kuandamana na mimi baada ya Mkutano huu twende akaangalie hali halisi? Kwa sababu tayari watu walishaanza kuchomeana ufuta, juzi hapa ufuta wa Kijiji cha Mirui umekatwa na wananachi wa kutoka Kilwa.
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi kuuliza swali la nyongeza. Utekelezaji wa REA Awamu ya Tatu kwenye Mkoa wa Lindi tumepata Mkandarasi ambaye uwezo wake ni mdogo sana. Mpaka sasa hivi awamu ya kwanza ya utekelezaji wa mradi huu ishafika nusu ya wakati wake lakini bado yuko kwenye Wilaya moja tu ya Ruangwa. Ni lini mkandarasi huyu ataweza kufika Liwale?
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi nami niulize swali la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mkoa wa Kusini unaozungumzwa ilikuwa uchangiwe pamoja na Wilaya ya Liwale, Nachingwea na Masasi kutokana na mikoa hii kuwa mbali na Makao Makuu ya Mikoa. Serikali kusitisha uanzishwaji wa Mkoa huu wa Selous, huoni kwamba ni kuwanyima haki ya kimsingi wananchi wanaokaa maeneo haya ambao wako mbali sana na Makao Makuu ya Mkoa? (Makofi)
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, vijiji vilivyotajwa na Mheshimiwa Waziri kwamba, ndiyo vinavyochangia katika Wilaya ya Liwale kwa Selous, vijiji hivi ndivyo vilivyoanzisha mgogoro kwa sababu vijiji hivi vimepakana na Selous kwa Mto wa Matandu. Kwa nini Kikulyungu peke yake ndio ambayo imeonekana kwamba imeondoka Matandu na ndio maana wanakijiji Wakikulyungu waligoma. Sasa Mheshimiwa Waziri ninachotaka kujua je, Mheshimiwa Waziri upo tayari kufuatana na Mheshimiwa Waziri wa Ardhi muende mkatafsiri GN ambayo inaitambua Pori la Akiba la Selous ukiachana na hii tangazo la mwaka 1974?
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi na mimi niulize swali langu la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye jibu la msingi Mheshimiwa Waziri amesema kwamba Bodi ya Mazao Mchanganyiko iko imara na haijatetereka. Naomba kuuliza kwa nini wakati tunaingiza zao la ufuta kwenye stakabadhi ghalani wasimamizi wakapewa Bodi ya Maghala badala ya Bodi ya Mazao Mchanganyiko?
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Halmashauri ya Wilaya ya Liwale ina umri wa miaka 43 sasa, licha ya kukosa nyumba za Askari walioko kule hata kituo cha Polisi hatuna, umri wa miaka 43. Ni lini Serikali itatujengea Kituo cha Polisi cha Wilaya ya Liwale, kuondokana na adha ya kupanga kwenye nyumba ambayo wamepanga, nyumba yenyewe nayo ni mbovu? (Makofi)
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kabla sijauliza swali la nyongeza kwanza napenda kutoa shukrani zangu za dhati kwa Mawaziri wote wanaohusika kuona wahudumu kwenye wizara hii kwa kunipunguzia tatizo la wafanyakazi, baada ya kunipatia wafanyakazi sita kwenye kada hii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sababu ya shida iliyopo wale wafanyakazi sita imekuwa kama tone la damu kwenye bahari. Kwa hiyo, shida iliyopo katika hospitali yetu ya Wilaya ya Liwale ni kubwa sana kiasi kwamba wauguzi wawili wanahudumia wodi tano kwa wakati mmoja, jambo hili ni baya sana vilevile linapunguza ufanisi wa kazi.
Je, Mheshimiwa Waziri yuko tayari kuniongezea wafanyakazi kwenye kada hii ya wauguzi ili kuongeza ufanisi kwenye hospitali ile ya wilaya?
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali moja la nyongeza. Baada ya tasnia ya korosho mwaka 2017 kufanya vizuri sana msimu uliopita, mwaka huu kumekuwa na matatizo ya mgogoro katika Mkoa wa Lindi kati ya Chama cha Ushirika cha Runali na Bodi ya Korosho. Jambo hili limefanya mpaka sasa hivi sulphur iwe bado haijafika katika Mkoa wa Lindi jambo ambapo limefanya sasa hivi mfuko mmoja wa sulphur kufika shilingi 70,000.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunaomba Serikali itoe tamko, ni lini mtatuletea sulphur ili kupunguza bei ya sulphur ambayo imepanda baada ya kuwa na mgogoro kati ya Runali na Bodi ya Korosho?
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri kutokana na swali hili. Kwa sababu sasa Harvesting Plan imekamilika ina maana sasa Serikali inaenda kuanza kupata mapato kutokana na msitu huo. Hata hivyo, kama ilivyo watu wa baharini au ziwani, uchumi wao mwingi unategemea mali ya bahari na mali ya ziwa. Vilevile sisi tulio kwenye misitu uchumi wetu mkubwa unategemea mazao ya misitu. Sasa kwa nini Serikali mpaka leo hii ile cess haijapata kuongezwa kutoka asilimia tano tunayoipata kutokana na uvunaji huu wa misitu, angalau ifike asilimia 10 ili kuweza kuinua kipato cha Halmashauri tunazozunguka?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, TFS wamekuwa na tabia ya kutotoa ile responsibility kwa vijiji vyetu yaani ile incentive. Sio hivyo tu kuna mazao ambayo yamevunwa na wavunaji haramu ambayo yapo kwenye Halmashauri zetu kwa muda mrefu yanaendelea kuharibika. Je, Serikali haioni sasa inaweza kutoa kwenye Halmashauri husika yale mazao ambayo yamevunwa kwa haramu ili yaweze kunufaisha kwenye vijiji vyetu, kwa mfano mazao ya mbao, yanaweza kutusaidia kutengeneza furniture au viti, meza na madawati kwa ajili ya shule zetu na hospitali zetu?
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kuniona na kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Mji wa Liwale ni Mji unaokua kwa haraka sana na una chanzo kimoja tu cha maji; na kutokana na mabadiliko ya tabianchi, chanzo kile hakitoshelezi tena. Je, ule mradi wa kutafuta chanzo mbadala cha maji kwa Mji wa Liwale, umefikia wapi?
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, barabara ya Nangurukuru-Liwale ni muhimu sana kwa wakazi wa Liwale, lakini siyo hivyo tu ni barabara iliyoahidiwa kwenye Ilani ya Chama cha Mapinduzi 2015-2020. Je, Serikali inawaambia nini wana Liwale juu ya ujenzi wa barabara hii kwa kiwango cha lami?
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante wa majibu ya Serikali athari kubwa ya mgogoro huo ni kijiji cha Kikulyungu kuondolewa kwenye WMA ya Jumuiya ya Magingo na kwa majibu haya inaonekana mgogoro huu umefika mwisho.

(i) Sasa ni lini Serikali itakuja Kikulyungu kuwapa wananchi matokeo ya maamuzi haya na kuwapa kibali au kuwapa kibali au kuwapa hati ili waweze kurudishwa kwenye Jumuiya ya Magingo?

(ii) Na kwa sababu sisi tunaoishi kwenye maeneo ya hifadhi kumekuwa na uharibufu mkubwa sana wa mazao unaotokana na wananyama waharibifu kama tembo, nguruwe, na wananyama wengine waharibu. Na Serikali imekuwa ikitoa kitu kinachoitwa kifuta machozi sasa ni lini Serikali itakuja na marekebisho ya sheria ili badala ya kutoa kifuta machozi iwe wananchi wao wanapata fidia inayotokana na uharibifu wa mazoa ya mashambani?
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Katika mradi wa kutafuta chanzo cha pili cha mbadala cha maji ya Wilaya ya Liwale palitolewa shilingi milioni 300 na DDCIA walishaanza kufanya kazi hiyo lakini wamechimba visima viwili ambavyo vina uwezo wa kutoa maji lita 5,000 lakini visima vile vimetelekezwa mpaka leo.

Je, Serikali iko tayari kutoa fedha kwa ajili ya kwenda kufanya uendelezaji wa visima vile ambavyo viko katika Kijiji cha Makata na kijiji na Mikunya?
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Baada ya Mtwara kupatikana kwa gesi Mheshimiwa Waziri akatangaza kwamba Liwale nao tutapata umeme wa gesi kutoka Mtwara. Wakati ambapo Mheshimiwa Waziri anatangaza nikamwomba nikamwambia kwa umeme ule wa Mtwara nafuu Liwale wakatuachia umeme wetu wa mafuta, lakini jambo hilo halikutekelezwa, matokeo yake sasa Liwale umeme unapatikana kwa shida sana.

Je, Mheshimiwa Waziri anatuahidi nini sisi watu wa Liwale shida hii tunayoipata mwisho lini? Maana sasa hivi umeme haupatikani kabisa, unawaka masaa mawili au matano.
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Awali ya yote, niishukuru Serikali kwa kuliona hili na kupandisha hadhi Hifadhi ya Selous, lakini baada ya kupandisha hadhi au baada ya Serikali kuimarisha uhifadhi katika hifadhi zetu suala la wanyamapori limekuwa ni shida sasa hivi, hasa wanyama kama tembo. Wanyama hawa sasa hivi wanasumbua kwenye maeneo yetu na niliuliza swali hapa kuhusiana na Serikali kuleta Muswada pengine kupata fidia wakasema haiwezekani, lakini bado suala la kifuta machozi hakipatikani. Je, Serikali ipo tayari kutupatia fedha hizi mapema iwezekanavyo?

Mheshimiwa Naibu Spika, Wizara ya Maliasili inapozungumzia utalii Kanda ya Kusini, bado napata changamoto. Mwaka jana tumepata fedha kuendeleza utalii Kanda ya Kusini, lakini Wizara hii inapozungumzia Kanda Kusini wanazungumzia Morogoro, Mbeya na Iringa, lakini Mkoa wa Lindi, Mtwara na Songea hautajwi. Je, Serikali kwa upande wake inapozungumzia kukuza utalii ukanda wa kusini unaamanisha mikoa ipi? Ahsante sana.
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ili niulize swali la nyongeza. Awali ya yote nitoe pole kwa wananchi wa nchi nzima hii ambao wamepata adha ya mafuriko hasa wa Wilaya yangu ya Liwale na Mkoa wa Lindi. Nawapa pole sana Mwenyezi Mungu aendelee kuwapa nafuu wakati huu wanahangaika na makazi yao.

Mheshimiwa Spika, suala la kilimo hakuna mtu ambaye hajui kwamba nchi yetu asilimia 75 ni wakulima lakini naona Serikali usimamizi wa kilimo wameachia Vyama vya Ushirika ambavyo havina uwezo wa kulisimamia. Mfano kwa suala la kuagiza vifaa au pembejeo wameachiwa Vyama vya Ushirika ambapo wao ndiyo wanaoingia mikataba na suppliers wa pembejeo hata kwenye mauzo. Kama Serikali mtaamua kuviachia Vyama vya Ushirika kusimamia kilimo basi tutendelea kusuasua kwenye kilimo.

Mheshimiwa Spika, mfano mzuri mwaka huu kwenye zao la korosho tumechelewa msimu tumekuja kuanza msimu mwezi wa kumi na moja wakati korosho wakulima wameshaanza kuzivuna tangu mwezi wa nane. Jambo hili mliliachia kwenye Vyama vya Ushirika matokeo yake tumechelewa kuanza msimu toka mwezi wa Novemba mpaka leo wakulima bado wana korosho.

SPIKA: Sasa swali.

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Je, Serikali ipo tayari kusimamia mazao haya badala ya kuviachia Vyama vya Ushirika?
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Wilaya ya Liwale ni wilaya ambayo ilianzishwa mwaka 75 leo ina umri wa miaka 45. Wilaya ile ina kata 20 lakini Mahakama mbili tu Mwanzo, na Mahakama ya Mwanzo ya Liwale Mijini ndio inayochangiwa na Mahakama ya Wilaya kwa maana kwamba Mahakama ya Wilaya hawana jengo. Lakini nilipouliza swali hili mwaka 2017 Mheshimiwa Kabudi akiwa hapo kwenye hicho kiti alisema mwaka 2018 inajengwa hospitali ya Wilaya. Je, Serikali kwenye majibu yale mlikuwa mnanidanganya?
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara ya Nangurukuru - Liwale ni ya vumbi na kokoto lakini naishukuru Serikali mwaka huu tumetengewa fedha shilingi milioni 300 kuanza usanifu wa kina. Hata hivyo, mvua zilizonyesha mwezi uliopita zimelaza watu siku tatu barabarani. Ni nini mkakati wa Serikali kuifanya barabara hii ipitike majira yote? (Makofi)
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi nami niulize swali la nyongeza. Wilaya ya Liwale ni Wilaya kongwe yenye umri zaidi ya miaka 44 sasa; pamoja na kwamba Halmashauri wametenga eneo kubwa kwa ajili ya ujenzi wa Kituo cha Polisi, lakini hadi leo Wilaya ya Liwale haina Kituo cha Polisi. Nini kauli ya Serikali namna ya kuwapatia wananchi wa Liwale ujenzi wa Kituo cha Polisi?
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Vilevile napenda kutoa shukrani kwa Mheshimiwa Waziri kwa majibu mazuri, lakini nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sababu ya msingi niliyosema shule hii ni shule pekee katika Halmashauri ya Wilaya ya Liwale, shule pekee yenye inawachukuwa watu wenye mahitaji maalum, kwa takwimu hiyo utaona kabisa kwamba bado kuna tatizo la miundombinu, shule hii inahitaji mabweni na ndiyo maana inakuwa na takwimu ndogo ya walemavu kwa sababu walemavu wengi kutoka vijijini wanashindwa kumudu kuandikishwa kwenye shule hii kwa sababu ya ukosefu wa mabweni, lakini siyo hivyo hata wale walimu hao anaowataja...

MWENYEKITI: Uliza swali basi Mheshimiwa.

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, najenga hoja; je, Mheshimiwa Waziri haoni umuhimu wa kujenga mabweni kwenye shule hii ili watoto wanaotoka nje ya Halmashauri hii waweze kumudu kuingia shuleni?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili kwa sababu ya mahitaji ya wanafunzi hawa wanatakiwa wafuatiliwe kule wanapokaa manyumbani kwa sababu hawakai bweni kwahiyo panahitajika usafiri wa walimu hao kuwafuatilia kule wanapoishi kuona maendeleo yao namna gani wanavyo catch yale masomo. Je, Serikali haioni umuhimu wa kuwanunulia vifaa kama vile mapikipiki hawa walimu watatu waliobaki ili waweze kumudu kuwafuatilia hawa watoto manjumbani kwao?
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi niulize swali la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, kama ambavyo Mheshimiwa Waziri amejibu mimi kwanza nimpongeze kwa majibu yake mazuri, lakini bado kuna tatizo la hawa watendaji wetu yaani kwa maana kwamba Wenyeviti wa Vijiji na Madiwani ni kwamba hawajapata semina, pamoja na kwamba sheria/sera bado haijaletwa ya ugatuzi wa madaraka lakini bado uko umuhimu wa kuwapa semina mara kwa mara ili waweze kujua mipaka yao ili waweze kuboresha utendaji wao wa kazi.

Je, Serikali haioni umuhimu wa kuwapa semina hawa watu, Wenyeviti wa Vijiji, Vitongoji ili waweze kufanya kazi vizuri? (Makofi)
MHE.ZUBERI M.KUCHAUKA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi na mimi niulize swali la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, pamoja na kwamba Serikali imewekeza fedha nyingi kwenye Bandari ya Mtwara, lakini commitment ya Serikali katika matumizi ya bandari ile bado haijaonekana. Mfano leo hii kule kuna kitengo cha mafuta (kuna pump ya mafuta ambayo inatakiwa wananchi wa Kanda ya Kusini wote wachukulie mafuta kwenye bandari ya Mtwara lakini ukienda kwa wafanyabiashara bado wanalalamika kwamba mafuta ya Mtwara yako bei juu kuliko Dar es Salaam, matokeo yake watu wanatoka Songea, wanatoka Lindi, wanatoka Tunduru wanafuata mafuta Dar es Salaam.

Mheshimiwa Spika, nini kauli ya Serikali namna bandari hii inaweza kutumika efficiently na sisi watu wa Kanda ya Kusini tukanufaika kwa kuwepo kwa bandari hii?
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kunipa nafasi niulize swali dogo la nyongeza, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, sambamba na barabara ya Masasi – Nachingwea, barabara hii vilevile ina jina la Lukuledi
– Liwale yenye jumla ya kilometa 175 kwa maana kutoka Masasi mpaka Liwale kilometa 175. Barabara hii tayari imeshafanyiwa upembuzi yakinifu na usanifu wa kina.

Wanaliwale wanataka kusikia barabara Nachingwea – Liwale lini itajengwa kwa kiwango cha lami? (Makofi)
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kuniona.

Mheshimiwa Naibu Spika, changamoto ya zao la kokoa iliyoko kule Mbeya ni sawasawa kabisa na changamoto ambayo zao la korosho kwenye Wilaya ya Liwale inakumbana nayo. Kwenye msimu uliopita 2018/2019 mikorosho yenyewe ilikuwa inakauka bila kujua sababu ni nini. Kwenye msimu huu uliopita kwa nje zinaonekana korosho ni nzima lakini ukizipasua kwa ndani zimeoza.

Je, Mheshimiwa Waziri yuko tayari kutuletea wataalam kwenye Wilaya ya Liwale waje kufanya tathmini au utafiti kujua ni nini changamoto za korosho Wilaya ya Liwale zinazosababisha wananchi wale wapate bei isiyoridhisha?
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi na mimi niulize swali la nyongeza. Tatizo kubwa la masoko ya tumbaku linafanana kabisa na tatizo la soko la korosho, lakini mimi nimegundua tatizo hili linasababishwa zaidi na kuwepo kwa mdudu mmoja anaitwa Vyama vya Ushirika. Vyama vya Ushirika vimekuwa vikiyumbisha sana masoko kwa wakulima wetu.

Je, Serikali iko tayari kuleta sheria ya Vyama vya Ushirika ili kuvifanyia marekebisho kuondoa matatizo yaliyoko kwenye vyama hivi? (Makofi)
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, Mji wa Liwale unakua kwa haraka sana na mahitaji ya maji yamekuwa ni makubwa na uhaba wa maji ni mkubwa sana. Bajeti iliyopita tuliletewa fedha shilingi milioni 100 kwa ajili ya kutafuta chanzo cha pili cha maji cha Mji wa Liwale lakini mpaka leo tunaambiwa DDCA hawana nafasi ya kuja Liwale. Ni lini Serikali watakuja sasa kutafuta chanzo cha pili cha maji kwa ajili ya Mji wa Liwale?
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi na mimi niweze kuuliza swali la nyongeza. Ni kwamba, Serikali yetu sasa hivi imeingia kwenye mfumo wa Serikali ya viwanda na uhamasishaji huu umekuwa mkubwa sana. Katika Wilaya ya Liwale viko viwanda vidogo vidogo kazi yake ni kusindika korosho, lakini wananchi wale wanashindwa kupata mali ghafi kwa sababu ya kuwa na mitaji midogo. Tunafahamu kwamba korosho, zinazalishwa, zinauzwa kwenye minada; na kwa sababu wale wawekezaji ni wadogo wadogo hawawezi kuingia kwenye mnada matokeo yake anapoingia kwa wananchi kwenda kununua korosho anaoneka wananunua kangomba.

Mheshimiwa Spika, je, sasa Serikali ina mpango gani wa kuwasaidia wananchi wale wadogo wadogo kupata mali ghafi hii ya korosho ili vile vikundi vyao vya kubangua korosho viweze kubangua kwa msimu mzima au kwa mwaka mzima?
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi na mimi kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, hii barabara siyo kwamba fedha Serikali hawana ya kujenga, ninachokiona hapa ni kwamba Serikali bado haijaamua kujenga hii barabara, kwa sababu zipo barabara zimefanyiwa upembuzi yakinifu tangu mwaka 2018, mwaka 2017, mwaka 2016 zimeshajengwa na zingine zinajengwa. Lakini hii tangu mwaka 2014, ninaiomba Serikali iamue kwa maksudi kabisa kuikomboa Wilaya ya Liwale na Wilaya ya Nachingwea ili iweze kufunguka nasi kiuchumi tuweze kuwa miongoni mwa watu waliopo duniani.

Mheshimiwa Spika, ahsante sana. (Makofi)
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi nami niulize swali la nyongeza. Halmashauri ya Wilaya ya Liwale ina vijiji 76, vijiji 34 bado havijapatiwa umeme. Naona uzalishaji wa vijiji vifuatavyo mahitaji ya umeme ni makubwa sana; Kijiji cha Mlembwe, Lilombe, Kikulyungu, Mkutano, Mpigamiti, Ngorongopa, Ngongowele, Kimambi, Nahoro na Ndapata, vijiji hivi kwa sababu ya uzalishaji wake mahitaji ya umeme ni makubwa sana. Je, Serikali ni lini mtatupelekea umeme kwenye vijiji hivi ili kuwatia wananchi hamasa zaidi waweze kuzalisha zaidi mazao ya chakula na biashara?
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Spika, ahsante kunipa nafasi kuuliza swali la nyongeza. Wilaya ya Liwale ni Wilaya ambayo iko mbali sana na makao makuu ya Mkoa ambako ni Lindi. Na pale Liwale hakuna kituo cha polisi kwa maana ya jengo hawana kabisaa, wanaishi kwenye nyumba ambayo ilipangwa na benki mpaka leo hii. Lakini, mwenyewe ni muhanga katika hili, mwaka huu mimi nimechomewa nyumba mbili na magari matatu wakati wa uchaguzi. Kimechangiwa sana na uhaba wa askari polisi na hatuna msaada wa karibu kutoka Liwale mpaka Nachingwea ni zaidi ya kilomita 120 mpaka Lindi zaidi ya kilomita 300. Sasa, je, Serikali ina mkakati gani kwanza, kutuongezea polisi Wilaya ya Liwale ikiwepo pamoja na majengo? (Makofi)
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Wilaya ya Liwale ina Kata 20 na vijiji 76, lakini bado upatikanaji wa maji ni wa shida sana hasa hasa kwenye vijiji vya Kihangara, Makata, Kikulyungu, Nahoro, Lilombe, Ngorongopa, Mkutano, Mtawatawa, Kimambi na Nanjegeja.

Mheshimiwa Waziri, ni lini vijiji hivi vinaweza kupatiwa maji safi na salama?
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa majibu ya Serikali ambayo naweza kusema kwamba hayaridhishi. Kwanza ni-declare interest kwamba na mimi ni miongoni mwa waathirika, nimepoteza mali yenye thamani ya zaidi ya shilingi 301,516,000. Pia kuna nyumba zaidi ya sita zenye thamani ya shilingi 417,300,000; magari nane yenye thamani ya shilingi 299,700,000; pikipiki nane zenye thamani ya shilingi 22,100,000 na vifaa vya ndani vyenye thamani ya zaidi ya shilingi 145,169,000. Jumla uharibifu huu umeigharimu halmashauri yetu zaidi ya shilingi milioni 886.

Mheshimiwa Naibu Spika, waathirika, kama nilivyosema, mimi mwenyewe ni mmoja wao, lakini yuko Musa Mkoyage, Hassan Liwango…

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Kuchauka, hilo ni swali, uliza swali lako.

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Naibu Spika, sawa. Sasa swali langu; hivi ni kweli Serikali pamoja na uharibifu huu mkubwa haioni umuhimu wa wananchi hawa waathirika zaidi ya 15 angalau kuwashika mkono? Ni kweli nchi yetu inaongozwa kwa sheria pamoja na kanuni, lakini kuna mila na desturi ya kufikiria kwamba hawa watu wameathirika, hawana mahali pa kuishi, hawana namna nyingine yoyote ya kushiriki maendeleo ya nchi hii; kweli Serikali haioni umuhimu wa kuwashika mkono watu hawa? (Makofi)
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Hali ya madhara yanayotokana na wanyamapori yamekuwa ni makubwa sana. Leo hii kwenye Vijiji vya Ngumbu, Kibutuka, Kiangala na Ngatapa, wananchi wameshahama wamerudi majumbani kwao kutoka mashambani, baada ya tembo kumaliza mazao yote. Sasa naomba Serikali ituambie, je, ina mkakati gani wa kuhakikisha usumbufu huu wa wanyamapori unapungua hasa kwenye hivi vijiji vichache nilivyovitaja? (Makofi)
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Spika, ahsante kunipa na mimi nafasi kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, ni kweli kama alivyojibu kwenye jibu la msingi kwamba barabara hii inaharibika sana kutokana na malori hasa ya Dangote na malori ya gypsum. Lakini usafirishaji kama anavyosema ni kweli Bandari ya Mtwara imeboreshwa kwa kiwango kikubwa, lakini gharama ya usafirishaji wa mzigo kutoka kwenye Bandari ya Mtwara na Bandari ya Dar es Salaam ni sawa sawa na ndiyo maana wafanyabiasha wana option kusafirisha mzigo kwa barabara kuja kusafirisha kwa Bandari ya Mtwara na ndiyo maana hata mafuta watu wa mafuta wameambiwa wachukulie Mtwara, lakini bado malori ya mafuta yanatoka Tunduru, yanatoka Liwale, yanatoka Nachingwea yana option kuja Dar es Salaam badala ya kuchukulia Mtwara.

Kwa hiyo, mimi naiomba Serikali sasa Serikali wataangalia namna yaku-adjust hizi bei ili iwe kivutio kwa Bandari ya Mtwara? (Makofi)
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Spika, ahsante kunipa na mimi nafasi kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, ni kweli kama alivyojibu kwenye jibu la msingi kwamba barabara hii inaharibika sana kutokana na malori hasa ya Dangote na malori ya gypsum. Lakini usafirishaji kama anavyosema ni kweli Bandari ya Mtwara imeboreshwa kwa kiwango kikubwa, lakini gharama ya usafirishaji wa mzigo kutoka kwenye Bandari ya Mtwara na Bandari ya Dar es Salaam ni sawa sawa na ndiyo maana wafanyabiasha wana option kusafirisha mzigo kwa barabara kuja kusafirisha kwa Bandari ya Mtwara na ndiyo maana hata mafuta watu wa mafuta wameambiwa wachukulie Mtwara, lakini bado malori ya mafuta yanatoka Tunduru, yanatoka Liwale, yanatoka Nachingwea yana option kuja Dar es Salaam badala ya kuchukulia Mtwara.

Kwa hiyo, mimi naiomba Serikali sasa Serikali wataangalia namna yaku-adjust hizi bei ili iwe kivutio kwa Bandari ya Mtwara? (Makofi)
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Spika, ahsante kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza:-

Mheshimiwa Spika, Wilaya ya Liwale inazungukwa na Pori la Selous, lakini sasahivi mkakati wa Serikali ni kuimarisha utalii wa picha badala ya utalii wa uwindaji na sisi kwenye Kanda ya Kusini kuanzia ukanda wa Kilwa mpaka Tunduru hakuna lango la utalii wa picha.

Je, Serikali haioni umuhimu wa kutuwekea sisi lango la utalii wa picha na sisi tuweze kunufaika na uwepo wa Selous?

SPIKA: Mheshimiwa kule Liwale unadhani lango lingeweza kukaa wapi kwa mfano?

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Spika, palepale Liwale Mjini ndio panafaa kwa sababu, Kambi ya Selou iko palepale Liwale.
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi na mimi niulize swali la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kumekuwa na tofauti kubwa kati ya miradi ya upembuzi yakinifu wa barabara zetu ukilinganisha na ujenzi, kwa sababu zipo barabara ambazo zimefanyiwa upembuzi yakinifu tangu mwaka 2012 na bado hazijajengwa.

Je, Serikali haioni kwamba ipunguze miradi ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina ili barabara ambazo zimeshafanyiwa upembuzi yakinifu kwanza zijengwe, kwa sababu haiwezekani mwaka 2012 ifanyiwe upembuzi halafu uje kuijenga 2025 useme kwamba utaijengwa kwa data zile zile, ni lazima itabidi ujenge kwa data zingine.

Je, huoni kama Serikali inapoteza fedha nyingi? (Makofi)
MHE: ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ili na mimi nipate kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naishukuru Serikali kwa kutupatia fedha kwa ajili ya maji ya Mji wa Liwale. Hata hivyo mpaka leo DDCA wametutia changa la macho, ni mwezi wa sita huu hawajaja; na Mheshimiwa Waziri ameniambia kwamba kuna uwezekano tukachukua watu binafsi wakaanza kuchimba pale. Lakini nimewasiliana na Mhandisi anasema asilimia 30 ya fedha hizo tayari DDCA walishachukua na walishaingia mitini.

Je, ni lini DDCA watakuja kutuchimbia maji Wilaya ya Liwale?
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Spika, na mimi kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Iko barabara ya kiuchumi barabara ya ukombozi kwa Wilaya ya Liwale, barabara ya Nangurukuru - Liwale. Barabara hii bajeti ya mwaka jana ilitengewa fedha kwa ajili ya kufanyiwa upembuzi yakini na usanifu wa kina, na mwaka huu pia imetengwa kwenye kufanyiwa upembuzi yakinifu na usanifu wa kina. Wana Liwale wangetaka kusikia, ni lini barabara hii itakwisha kufanyiwa upembuzi yakinifu na usanifu wa kina, na hatimaye kujengwa kwa kiwango cha lami? Ahsante sana. (Makofi)
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kwanza mimi ni Mjumbe wa Kamati ya Miundombinu. Barabara ya Nangurukuru - Niwale ni mwaka wa tano inatengwa fedha kwa ajili upembuzi yakinifu na usanifu wa kina…

NAIBU SPIKA: Uliza swali. Taja barabara unayotaka ijibiwe.

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Naibu Spika, Nangurukuru - Liwale, fedha hazijawahi kuletwa tangu zinatengwa miaka yote mitano.

NAIBU SPIKA: Swali lako ni nini?

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni lini Serikali italeta fedha kwa ajili ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina kwa barabara ya Nangurukuru - Liwale? (Makofi)
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nishukuru Serikali kwa majibu mazuri, na nimpongeze Naibu Waziri kwamba naye ameshafika Liwale kwa hiyo ninachokizungumza anakifahamu. Lakini hii sehemu ya pili anayosema kwamba Madiwani na Wabunge wanahusika, kwamba wanapata hizi taarifa, mimi nimekaa Liwale miaka sita, sijawahi kupata hii taarifa zikiletwa kwenye Baraza letu la Madiwani. Kwa hiyo jambo hili labda leo aagize hili jambo lifanyike lakini hili jambo halifanyiki kabisa.

Mheshimiwa Naibu Spika, sehemu ya pili, kwamba Kamati hii ya Uvunaji anayeingia mwanakijiji ni Mwenyekiti wa Kijiji peke yake, sasa wanaovuna hesabu zinakuja pale wanaambiwa cubic meters yule mwanakijiji cubic meters hajui, magogo mangapi yanaondoka hajui, matokeo yake kuna magogo yale makubwa ambayo yana mashimoshimo wanayaacha, kwa hiyo uharibifu ni mkubwa sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa naomba kufahamu, ni lini Serikali italeta fedha za upandaji miti kwenye vile vijiji ambavyo vina uvunaji huo ambao mimi nausema kwamba ni uvunaji wa holela?
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi nami niulize swali dogo la nyongeza. Wilaya ya Liwale ni miongoni mwa wilaya kongwe lakini haina Kituo cha Polisi mpaka leo sambamba na nyumba za watumishi. Nami kutoka kwenye Mfuko wa Jimbo kutokana na shida hiyo, nimetoa shilingi milioni 10 kusaidia ujenzi wa Kituo cha Polisi. Nini kauli ya Serikali kuwasaidia wananchi wale wapate Kituo cha Polisi? (Makofi)
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Kwanza nitoe shukrani kwa majibu mazuri ya Serikali juu ya swali langu, lakini nina maswali mawili ya nyongeza: -

Mheshimiwa Spika, kwani upo udanganyifu uliofanywa katika Kijiji cha Kibutuka na aliyekuwa mfanyakazi wa Tigo, alienda pale akadanganya wanakijiji kwamba, anahitaji eneo la kujenga mnara, baadaye wanakijiji walimpa bure wakitumia mukhtasari ule yule sasa hivi anekuwa ndio mnufaika wa kodi ya mnara ule badala ya kuwa wanakijiji waliopo katika kijiji kile.

Je, Serikali ina mkakati gani au ina kauli gani juu ya utapeli wa huyu mtumishi wa tiGO ambaye yeye anajifanya kwamba, ndio mmiliki wa lile eneo wakati aliliomba apewe bure?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; pamoja na kwamba, Vijiji vya Ndapata, Ndunyungu, Makata, Mtawatawa, Kipelele, Makinda na Nambinda havina mawasiliano ya kutosha. Nini mkakati wa Serikali wa kutuwashia ile minara ambayo tayari imeshawashwa kwenye baadhi ya vijiji hapa nchini?
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Wilaya ya Liwale ina umri wa miaka 47 sasa, haijawahi kuwa na jengo la Kituo cha Polisi ukiacha lile jengo ambao wamepanga lililokuwa la benki. Nini, kauli ya Serikali kuipatia Wilaya ya Liwale jengo la Polisi? (Makofi)
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali ya nyongeza. Kwa kweli vijiji hivi kama majibu ya msingi yanavyosema; ni kweli upimaji huu ulifanywa lakini walio wengi wanaolalamika ni kwamba upimaji haukuwa shirikishi. Kwa mfano, kuna mgogoro wa Mkutano na Kikunyungu, Kipelele, Nangumbu au Ngongowele na Ngunja. Wanachozungumza pale ni kwamba yale mawe wakati wanabeba kuna mahali walichoka wakayatunza mahali. Matokeo yake hawakurudi pale, kwa hiyo, yule aliyekuja kuchukua a-coordinate majira ya nukta akachukulia pale. Kwa hiyo, hicho ndiyo chanzo cha migogo mingi kwenye hivi vijiji ambavyo nimevitaja.

Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile kuna mgogoro kati ya Wilaya ya Kilwa na Wilaya ya Liwale kwenye Vijiji vya Nanjilinji na Milui. Mgogoro wake scenario yake inafanana na hiyo hiyo, kwamba wakati wanapima wakazi wa wilaya hizi mbili zote hawakushirikishwa. Sasa Je, Mheshimiwa Waziri yupo tayari kufuatana nami baada ya Bunge hili twende Liwale akatatue migogoro hii?
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Barabara inayotoka Mangaka Wilaya ya Nanyumbu - Nachingwea Tarafa ya Kilinalondo - Liwale katika Kata ya Ilombe, tumeshaiombea iingie TANROADS, lakini mpaka leo tunapigwa danadana.

Je, ni lini barabara hii itaweza kupandishwa hadhi kuwa barabara ya TANROADS kwa sababu barabara hiyo imepita katika wilaya tatu?
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa na mimi nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, Wilaya ya Liwale ilikuwa na gari moja tu ambalo kwenye Uchaguzi uliopita gari lile lilichomwa moto mpaka sasa hivi Wilaya nzima ile haina gari hata moja. Ni nini mpango wa Serikali kutupatia miongoni mwa hayo magari 78?
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, asante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wilaya ya Liwale ilikuwa na mradi wa kimkakati wa stendi lakini fedha zililetwa zikarejeshwa baada kukwama kwenye manunuzi.

Je, fedha zile zitarejeshwa lini ili mradi ule uendelee?
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Wilaya ya Liwale haina Kituo cha Polisi na kwa kuliona tatizo hilo nimetoa fedha shilingi 10,000,000 kutoka kwenye Mfuko wa Jimbo kwa ajili ya kuanza ujenzi. Je, Serikali inatusaidiaje ili kuimarisha kituo cha Polisi cha Wilaya ya Liwale? (Makofi)
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, Wilaya ya Liwale inazo barabara moja muhimu sana, barabara ya uchumi, barabara ya Mkombozi. Barabara hii nimeizungumza mara nyingi mno, barabara ya Nangurukuru Liwale. Wananchi wa Liwale wanataka kusikia barabara hii itajengwa lini kwa kiwango cha lami?
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Kwanza naishukuru Serikali kwa majibu mazuri yanayotia moyo. Hata hivyo majibu haya hajatoa takwimu; yaani hizi takwimu hazijaja na percent ili tuone ukubwa wa tatizo sisi kama wawakilishi wa wananchi.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mfano, mimi hapa nina takwimu ya chuo kimoja tu hiki cha MUHAS hapo Muhimbili. Mwaka 2022/2023 udahili, wanafunzi walioomba pale walikuwa 27,540; waliokidhi vigezo 19,287, lakini chuo kile kina uwezo wa kudahili wanafunzi 866 tu, ambayo ni 4% tu ya mahitaji: Je, hatuoni kwa trend hii kwamba tunakatisha tamaa vijana wetu kuendelea kusoma masomo ya Sayansi? (Makofi)
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kwenye Mji wa Liwale upo mradi wa kuupatia maji mji ule na tumechimba visima vitatu Kijiji cha Turuki, lakini mradi ule sasa umesimama kwa muda mrefu. Je, lini hatima ya mradi ule ili Mji wa Liwale upate maji safi na salama?
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi na mimi kuuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, wakati tunatangaza Hifadhi ya Nyerere, National Park tayari kuna maeneo ya WMA, mfano kama Wma ya Magingo katika vijiji vya Mpigamiti, Barikiwa na Mlembwe tayari vimechukuliwa na TANAPA.

Je, ni lini Serikali itakuja kuhakiki hiyo mipaka ili yale maeneo yaliyokuwa yamehifadhiwa na vijiji yaendelee kuwa yanahifadhiwa na vijiji?
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kutokana na ripoti ya GST, Wilaya ya Liwale imeonekana kuwa na madini mengi sana ya dhahabu, kito na sapphire. Tayari wawekezaji wako kule na wachimbaji wadogo wameshaanza kazi, lakini Wilaya ya Liwale haina Ofisi ya Madini pale, matokeo yake wale wachimbaji wadogo na wawekezaji wengine wanakwenda Tunduru kuuzia madini. Je, Serikali haioni umuhimu wa kuweka ofisi pale Liwale ili kuwarahisishia wachimbaji wadogo kupeleka madini yao Tunduru badala ya kuuzia Liwale?
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi kuuliza maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, kwanza nishukuru Serikali kwa kuonesha commitment ya kutaka kujenga stendi hii ya kisasa, lakini nimewasiliana na watu wa Halmashauri, wanasema kwamba kwa upande wa Halmashauri mchakato umeshakamilika kutoka kwenye ngazi ya Wilaya mpaka kwenye ngazi ya Mkoa. Sasa hivi Je, Mheshimiwa Waziri upo tayari kuwasiliana na watu wa TAMISEMI kwa kuona kwamba mradi huu umekwama kwenye ngazi hiyo? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili kwa sababu kumebakizwa miezi miwili bajeti aliyoitaja hapo inakwenda kukamilika. Je, Mheshimiwa Waziri upo tayari kututengea tena fedha kwenye bajeti hii iwapo kama fedha zile za mwanzo zitakuwa bado hazijatumika? (Makofi)
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali. Lakini kutokana na umuhimu wa shule hii, kama ilivyoelezwa hapa; kwamba ni ya muda mrefu sana; na naona hapa majibu yote yaliyotoka ni ya jumla jumla.

Mheshimiwa Spika, nachotaka kuomba ni commitment ya Serikali; je, Shule hii ya Kingurungundwa ni lini italetewa fedha kufanyiwa ukarabati? Kwa sababu hali ya shule hii ni mbaya zaidi kuliko hizo shule nyingine ambazo umezijumuisha kwenye majibu yao. Naomba kupata commitment ya Serikali, hii Shule ya Kingurungundwa ni lini italetewa fedha ili ifanyiwe ukarabati mkubwa?
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Katika Mji wetu wa Dar es Salaam kumejengwa barabara ya njia nane, lakini madereva wengi hawajui matumizi ya barabara ile.

Je, ni lini Serikali itaendesha mafunzo ya kutumia ile barabara kwa sababu unakuta guta limekaa kwenye highway badala ya kukaa kwenye barabara ya upande wa kushoto. Je, Serikali ni lini itatoa mafunzo rasmi?
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwanza napenda kutoa shukrani za dhati kwa majibu mazuri ya Serikali yanayotia matumaini, lakini hata hivyo namshukuru sana Mheshimiwa Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanznaia, Mama yetu Mama Samia Suluhu Hassan, tumepata fedha zile za UVIKO, tumejenga chujio na sasa hivi tunapata maji safi ka Mji wetu wa Liwale. Nina swali moja tu la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, vipo Vijiji vya Ngongowele, Makata, Mtatawa, Kihangala, Kipelele, Nguta, Mpengele, Ndapaka, Mlembwe na Nangano. Vijiji hivi bado havijapata maji safi na salama. Naomba kupata comfort kutoka Serikalini, ni lini wananchi wa vijiji hivi wataweza kufikiwa na mradi wa maji ili kutimiza ile azma ya kumtua Mama ndoo kichwani iweze kukamilika? Ahsante sana. (Makofi)
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Wilaya ya Liwale iliahidiwa kujengewa Chuo cha VETA kwenye bajeti hii inayotekelezwa sasa. Mpaka leo hii imebakia miezi miwili bajeti inakwenda kwisha: Je, lini tutapewa fedha hizi tuweze kujenga chuo hicho?
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, viko Vijiji vya Mtawatawa, Ndapata, Ndunyungu na Ndinda, ambavyo havina mawasiliano kabisa. Ni lini Serikali itaona umuhimu wa kupeleka mawasiliano kwenye vijiji hivyo?
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi kuuliza swali la nyongeza. Sera ya Taifa letu ni kuunganisha barabara za mikoa kwa lami, lakini sisi Mkoa wa Lindi haujaunganishwa na Mkoa wa Morogoro kwa barabara hata ya vumbi.

Je, Serikali inasema nini juu ya kuunganisha sisi Mkoa wa Morogoro na Lindi kwa barabara angalau ya changarawe pale Liwale na Mahenge?
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Wilaya ya Liwale pamoja na kwamba ni ya mwaka 1975 haijawahi kuwa na jengo la Kituo cha Polisi, lakini Serikali walituahidi kutujengea Vituo vya Polisi katika Kata za Kimambi, Lilombe na Kibutuka. Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi hii?
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Gereza la Liwale pamoja na kwamba lina uzio wa miti, Mkuu wa Gereza amejenga nyumba tano za two in One na bado nyumba zile zimeishia kwenye linta. Je, Serikali haioni umuhimu wa kumwongezea fedha Askari yule ili wamalizie nyumba zile za maaskari?
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wilaya ya Liwale kwenye bajeti ya 2018-2020 tulitengewa fedha kwa ajili ya kujenga stendi ya kisasa kama mradi wa kimkakati, lakini fedha zile zilirudishwa kutokana na sababu zisizojulikana. Je, ni lini Serikali itatuletea fedha hizo tena ili mradi ule wa kimkakati uweze kukamilika kwa wakati?
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kabla sijaja na swali la nyongeza kwanza nisikitike kwa majibu ambayo hayajaridhisha. Hayajaniridhisha mimi wala wananchi wa Liwale. Nina sababu zifuatazo; kwanza Wizara haikuzingatia umbali uliopo kutoka Liwale kwenda Nachingwea lakini vile vile haikuzingatia miundombinu ya usafiri uliopo kutoka Liwale kwenda maeneo iliyotajwa. Hata Mkoa wenyewe wa Lindi ukiuangalia ukubwa wake Wilaya ya Liwale ndiyo yenye eneo kubwa Mkoa wa Lindi. Takriban theluthi moja ya Mkoa wa Lindi iko Liwale. Sasa kuniambia kwamba Wilaya ya Liwale ina shughuli pungufu ya uchimbaji wa madini napata shida kukubaliana na jambo hilo. Hii ni kwa sababu kuna eneo kubwa sana ambalo linazungumzwa Wilayani Nachingwea, eneo la Kitowelo. Eneo hili la Kitowelo liko mpakani na Liwale...

MWENYEKITI: Mheshimiwa uliza swali la nyongeza.

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Swali langu: -

(a) Je, Wizara hii ya Madini haiko katika mfumo ule wa kusogeza huduma kwa wananchi?

Mheshimiwa Mwenyekiti, maana kama ingekuwa kwenye hiyo mpango wa kusogeza huduma kwa wananchi kwa karibu basi na sisi tungepatiwa Ofisi. Ile taasisi ya GST ilikuja Liwale ikakaa mwezi mzima ikakaa pale Liwale waliweka kambi Mpigamiti pale, mwezi mzima. Wamefanya utafiti wa madini lakini mpaka leo hatujapata sisi kama Wilaya, kupata hata kile kitabu cha matokeo yale ya uchimbaji wa madini. Matokeo yake sasa watu kutoka Kanda ya Ziwa ndio wanachukua vitalu kule kwa wingi sana kwa sababu matokeo yote yako hapa GST Makao Makuu.

(b) Je, Wizara ya madini iko tayari sisi kama Halmashauri kutupatia vile vitabu vya matokeo ya utafiti ule?
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Wilaya ya Liwale ina WMA ya Magingo, lakini uanzishwaji wa TANAPA, ile Hifadhi ya Mwalimu Nyerere imeingia kwenye maeneo ya WMA ya Magingo katika Kitalu cha Nachengo, Kijiji cha Mpigamiti na Ndapata na Kimambi: Je, Serikali inachukua hatua gani kwenda kutatua migogoro hii iliyoletwa na uanzishwaji wa Hifadhi ya Mwalimu Nyerere?
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kituo cha Afya cha Ngongowele kilipata fedha za Matokeo Makubwa Sasa, tulipata shilingi milioni 250, mradi ambao umeshaisha; je, Serikali haioni imefika wakati kutupatia shilingi milioni 250 nyingine kumalizia kituo kile?
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kumekuwa na wimbi kubwa la kuhama watumishi kwenye Idara ya Afya kwenye Halmashauri hasa zile za pembezoni. Mfano Liwale tulipata watumishi 80 lakini watumishi wale leo ukienda kuwahesabu hata 15 hawafiki, wanahama 36 wanahamia wawili; je, Serikali ina mpango gani kudhibiti huo uhamaji wa watumishi holela?
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Wilaya ya Liwale ndiyo wilaya pekee yenye kilometa chache sana za barabara za changarawe na tuna chini ya kilometa nne tu za lami. Je, Serikali haioni umuhimu wa kuiongezea wilaya hii fedha za TARURA ili kuongeza ufanisi wa ujenzi wa barabara hizo? (Makofi)
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa majibu mazuri ya Serikali yanayotia moyo, lakini nina maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza; Mji wa Nachingwea ni mji unaokua haraka sana. Upo Mradi wa Maji pale Nachingwea ambao tayari sasa hivi imeonekana mradi ule hautoshelezi. Je, Serikali iko tayari kutupatia fedha Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea ili kupanua Mradi ule wa Maji wa Mji wa Nachingwea?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; kama ilivyo kwa Mji wa Nachingwea unakua haraka, Mji wa Liwale nao una mradi sasa una miaka zaidi ya miwili kwa ajili ya maji katika Mji wa Liwale. Je, Serikali ipo tayari kutupatia fedha ili tuondokane na adha ya maji pale Mjini Liwale? (Makofi)
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Spika, kwanza ninashukuru kwa majibu mazuri yanayotia tumaini kutoka Serikalini. Vilevile ninashukuru kwenye ile barabara yangu ya Nachingwea – Liwale, tarehe 12 yule mkandarasi anaenda kukagua. Nashukuru sana. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, baada ya hivyo, nina maswali mawili; barabara hii niliyoitaja inayounganisha Morogoro, tayari TANAPA wameshaanza kuichonga. Sasa tunachotaka kujua; je, sisi tunaweza kuanza kupita hata kabla ya huo upembuzi yakinifu na usanifu wa kina uliotajwa?

Swali la pili, tayari kwenye bajeti iliyopita tunayo barabara yetu ya Nangurukuru – Liwale kilometa 230. Tulishapewa kilometa 72 wananchi wa Liwale wanataka kujua ujenzi unaanza lini? (Makofi)
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Ninaishukuru Serikali kwa majibu mazuri yenye kutia matumaini, nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, kwa sababu Serikali imekiri kwamba upatikanaji wa pembejeo ndiyo shida mojawapo inayofanya zao hili lisilete tija iliyokusudiwa. Je, Serikali haioni pamoja na kwamba mwakani itatusambazia hizo mbegu bure, je na pembejeo zingine kama mbolea tutazipata?

Swali la pili, kwa kuwa tunayo Bodi ya Pareto, je, Serikali haioni umuhimu wa kuiwezesha hiyo Bodi ya Pareto kwa kuwaongeza bajeti na kuwaongezea watumishi?
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi na mimi kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mji wa Liwale unaoundwa na Kata tatu, Kata ya Likongole, Liwale Mjini na Nangando vipo vijiji zaidi ya kumi lakini vijiji vile vimegawanya, kuna vijiji vinalipa shilingi 27000 na kuna vinavyotakiwa kulipa shilingi 350,000. Je, Serikali haioni kwamba kwa sababu vyote hivi ni vijiji viingizwe kwenye kulipa shilingi 27000 ili kuweka usawa?
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Spika, kwanza nishukuru kwa mara ya kwanza swali langu hili limepata majibu mazuri ya Serikali, imenitia tumaini, lakini bado ina maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza; kwa sababu ya kituo hiki kuitwa kituo cha karibu cha usaidizi Mheshimiwa Waziri Mkuu alipokuja Liwale alituahidi kutujengea kituo kwenye Tarafa ya Kibutuka na Kata ya Lilombe. Je, ahadi hiyo itatekelezwa lini?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; kwa sababu jiografia ya Liwale kuwa ngumu hali ya usafiri ni mbaya sana, sasa je, Serikali iko tayari kutupatia gari kwa ajili ya maaskari wa kituo hiki?
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Mheshimiwa Waziri amesema kwamba mwajiri wa Walimu hawa ni Mkurugenzi wa Halmashauri, lakini Mkurugenzi huyo wa Halmshauri amemnyima nafasi ya kukataa uhamisho wa mtumishi, jambo linalofanya watumishi wengi kuchukua namba tu kwenye hizi wilaya ambazo zipo pembezoni na kuondoka. Je, Serikali ina mkakati gani kuhakikisha Wakurugenzi wanakuwa na Mamlaka ya kuhamisha kulingana na wanavyoona nafasi inayopatikana?
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Wilaya ya Liwale ndiyo Wilaya katika Mkoa wa Lindi imepokea wafugaji wengi sana lakini hakuna miundombinu ya majosho wala malambo. Je Serikali iko tayari kutujengea majosho na malambo kwenye Kata ya Lilombe na Kata ya Ndapata, Kata ambazo ndizo zimetengwa kwa ajili ya kupokea wafugaji? (Makofi)
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, kwanza nishukuru Wizara kwa majibu mazuri yanayotia matumaini. Jambo hili linaenda kutatua tatizo kubwa la ununuzi, na hasa katika taasisi zetu za umma ambazo zinaingia kwenye ushindani ambazo zinashindwa kufanya manunuzi kwa sababu ya ushindani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini nina maswali mawili ya nyongeza. Kwa kuwa miradi mingi kwenye halmsahuri zetu sasa hivi inatekelezwa kwa force account na watu wanaoingia kwenye manunuzi ni watu ambao hawana taalum; Je, Serikali iko tayari kutoa mwongozo mahsusi ili kuongoza kuona namna gani hayo manunuzi yanayokwenda kufanya kusiwe na mgongano ambao sasa hivi nani ambaye anatakiwa kujibu maswali hayo ya ununuzi?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, ili kupunguza safari nyingi za maafisa ununuzi kwenda na kurudi kwa ajili ya kwenda kufanya manunuzi, Je, Serikali haioni umuhimu wa kuongeza yale masurufi (imprest) kutoka milioni tatu ili kufika milioni kumi, kwa sababu sasa hivi hakuna bidhaa inayoweza kununuliwa kwa shilingi milioni tatu? Kwa hiyo matokeo yake wale maafisa manunuzi wanakwenda na kurudi zaidi ya mara tatu kwa bidhaa moja.
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa jambo la kuita watu wengi kwenye nafasi chache chache za usaili limekuwa ni jambo sugu na Serikali hamuwezi kulifanyia kazi; je, hamuoni sasa umefika wakati kuwapa posho angalau wale mnaowaita, ili waweze kujikimu wanapokuwa Dodoma?
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, Mji wa Wilaya ya Liwale kijiografia imekaa vibaya sana hasa kwa ulinzi tunayoahadi ya kujengewa vituo vya polisi kwenye Tarafa ya Kibutuka, Kata ya Lilombe na Kata ya Kimambi. Nini kauli ya Serikali juu ya kutekeleza ahadi hiyo ili kuimarisha ulinzi kwenye Wilaya yetu ya Liwale? (Makofi)
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kunipa nafasi kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, kumekuwa na uhaba mkubwa wa watumishi katika Wilaya ya Liwale, lakini hata hivyo mgao tunapata watumishi, lakini idadi ya watumishi wanaohama na wanaohamia kubwa ni ile ambayo wanahama bila kufanyiwa replacement. Je, nini kauli ya Serikali juu ya kuhamisha watumishi bila kutupatia replacement kuziba nafasi hizo? Ahsante.
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kuniona kunipa nafasi niulize swali la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, Mji wa Liwale ni mji unaokua kwa kasi sana na ni miaka 42 sasa umri wa mji ule, lakini una kilometa 1.8 tu za lami pale mjini. Je, Serikali iko tayari kutuongezea mtandao wa barabara ya lami kwenye mwaka huu wa bajeti?
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kata ya Miluwi iko umbali wa kilomita 80 kutoka Liwale Mjini ambako kuna hospitali ya wilaya na uhitaji wa kituo cha afya pale ni mkubwa sana na wananchi wameshaanza ujenzi wa kituo cha afya pale. Je, Serikali iko tayari kusaidia kwenye bajeti hii kuunga mkono juhudi zile za wananchi?
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa majibu ya kuridhisha.

Kwa kuwa barabara nyingi hapa nchini zimeshafanyiwa upembuzi yakinifu kwa muda mrefu sasa na hizo barabara zimeshakuwa ni nyingi sana; na bado ukiuliza unaambiwa tunatafuta fedha kwa ajili ujenzi.

Je, Serikali haioni kwamba imefika wakati sasa tusitishe kwanza kuendelea kufanyia upembuzi yakinifu tumalize hizi barabara ambazo tayari zimeshajengwa ili resource tulizonazo tumalizie hizi zilizojengwa ndipo tuendee kufanya upembuzi yakinifu?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, iko barabara inayotoka Masasi kwenda Nachingwea mpaka Liwale zaidi ya kilometa 158, barabara hii imeshafanyiwa upembuzi yakinifu zaidi ya miaka minane sasa.

Je, ni lini Serikali wataijenga barabara hii kwa kiwango cha lami?
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa nafasi. Pamoja na kwamba Serikali imekuwa ikipeleka vifaa tiba kwenye baadhi ya zahanati zetu na vituo vya afya lakini bado kuna tatizo la vifaa tiba hivyo kukosa watumiaji (wataalamu). Nini kauli ya Serikali kupeleka watumishi kwenye hizi zahanati na vituo vya afya ambavyo vina vifaa tiba?
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa nafasi. Pamoja na kwamba Mheshimiwa Rais alipokuja Liwale ametuahidi kutujengea barabara ya Nangurukuru - Liwale, vilevile alituahidi kutujengea barabara kilometa mbili kwa ajili ya Liwale Mjini. Je, ahadi hiyo itatekelezwa lini?

Hon. Dr. Tulia Ackson

Speaker

Legislative Role

Profile

Ask the Speaker / Comments

Ms. Nenelwa J. Mwihambi

Clerk of the National Assembly

Legislative Role

Profile

Ask the Clerk / Comments

View All MP's