| E-mail this to a friend | Printable version |
|
||||||
| Session No | Question Number | To the Ministry of | Sector | Date Asked | ||
|---|---|---|---|---|---|---|
| 7 | 113 | WORKS | Communication/Infrastructure | 20 April 2012 | ||
| Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Pamoja na majibu ya Mheshimiwa Waziri ambayo yana masikitiko makubwa ameainisha barabara ambazo hazipo katika Jimbo langu, lakini majibu haya ya upembuzi yakinifu tumechoka nayo sasa. Tunahitaji utekelezaji wa barabara hii ya Makofia –Mzenga ni barabara ambayo inategemewa na wananchi wa Jimbo la Kibaha Vijijini katika kunyanyua uchumi wa Jimbo lao. Ni lini sasa barabara hii itajengwa kwa kiwango cha lami? |
||||||
| ANSWERS TO SUPPLEMENTARY QUESTION # 113 SESSION # 7 | ||||||
|
||||||
| NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Abuu, kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Spika, nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba hatutaweza kuijenga hiyo barabara bila kufanya upembuzi yakinifu na pia usanifu wa kina. Tuko kwenye kipindi cha sayansi na teknolojia, hatuwezi kurudi tena enzi zile za kuweka kamba na kuanza kulima barabara bila hata kufanya upembuzi yakinifu. Tumepanga kuanza upembuzi yakinifu na usanifu wa kina na pesa tutakuwa tunayo katika kipindi cha mwaka 2013/2014. |
||||||