You are using an older version of Internet Explorer.

In order to get the most out of our website, you can get a free update of Internet Explorer.
If you're using a work computer, please contact your IT administrator.

[CLOSE]
  email E-mail this to a friend email Printable version

Supplementary Question

mp Saleh, Ramadhan Haji[CCM]

Bumbwini Constituency
Session No Question Number To the Ministry of Sector Date Asked
10 113 FINANCE AND ECONOMIC AFFAIRS Tax 8 February 2013
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba niulize swali moja tu la nyongeza kama ifuatavyo:-

Kwa kuwa kumekuwa na sintafahamu katika ukusanyaji wa mapato katika nchi yetu, hali inayopelekea Watanzania kutoamini kuwa mapato haya yanayopatikana siyo sawa. Je, Serikali inawaambiaje Watanzania kuhusu hali hiyo?
ANSWERS TO SUPPLEMENTARY QUESTION #  113  SESSION #  10
mp Answer From Hon.Mbene, Janet Zebedayo
FINANCE AND ECONOMIC AFFAIRS
NAIBU WAZIRI WA FEDHA:

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba nijibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Ramadhani Haji Saleh, Mbunge wa Bumbwini, kama ifuatavyo:-

Ningependa kumhakikishia Mheshimiwa Mbunge pamoja na Watanzania wote kwa ujumla kuwa, takwimu tunazozitoa kwa ajili ya kulipa kodi zipo wazi na mahali popote pale ambapo kodi inapokelewa kuna taratibu zake na takwimu zinawekwa. Kwa hiyo, labda kitakachotakiwa ni kuwa zioneshwe kwa uwazi zaidi, sehemu nyingi zaidi, ili Wananchi waamini kama kweli tunapokea hizo kodi kama tunavyotamka na kuwa kodi hizo zinatumika katika maeneo ambayo Serikali imepanga kwa ajili ya maendeleo ya Wananchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama kuna mengine zaidi tutajitahidi kadiri iwezekanavyo, kutoa taarifa zaidi mpaka kufikia walengwa wote hadi Wananchi wa Vijijini kujua kama kweli tunakusanya, lakini takwimu hizo ni sahihi na ni rahisi kuzithibitisha.