You are using an older version of Internet Explorer.

In order to get the most out of our website, you can get a free update of Internet Explorer.
If you're using a work computer, please contact your IT administrator.

[CLOSE]
  email E-mail this to a friend email Printable version

Supplementary Question

Session No Question Number To the Ministry of Sector Date Asked
8 326 ENERGY AND MINERALS Energy 6 August 2012
Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa majibu ya Mheshimiwa Waziri, lakini nina maswali ya nyongeza. Mheshimiwa Waziri amezungumzia la umeme wa gesi pamoja na makaa ya mawe. Lakini makaa ya mawe ya Ngaka ambayo yameshaanza kuvunwa bado Serikali haijaweka msisitizo wa kujenga transmission line kutoka Ngaka mpaka Songea, Njombe hadi kufika Mufindi. Je, nini majibu ya Serikali kuhusiana na mradi huo wa ujenzi wa
Transmission line?

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Waziri amesema
kwamba hawawezi kulipa fidia lakini kwa kuwa watu
wengi ambao wamechukua mikopo katika mabenki
wanashindwa kufanya marejesho kutokana na
kutokuwa na uzalishaji wa kutosha kulingana na miradi yao ilivyokuwa. Kwa nini Serikali isitoe dhamana yaani wa bailout kwa kipindi fulani ili watu waweze kujenga uwezo wa kulipa madeni hayo kwa uhakika?
ANSWERS TO SUPPLEMENTARY QUESTION #  326  SESSION #  8
mp Answer From Hon.Simbachawene, George Boniface Taguluvala
ENERGY AND MINERALS
NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI:

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba maendeleo ya mipango ya uzalishaji wa umeme kupitia makaa ya mawe ya Mchuchuma, Ngaka na Kiwira yanaendelea vizuri. Tuna matarajio kwamba ifikapo mwaka 2015 tunaweza tukawa tumeshaanza kuzalisha takribani MW 200 kutoka Mgodi wa Kiwira na takribani MW 300 kwa Mchuchuma na Ngaka 120. Hayo ndio matarajio yetu.

Mheshimiwa Spika, napenda kuchukua nafasi hii
kumhakikishia kwamba mipango ya ujenzi wa
miundombinu itakayokwenda sambamba na uzalishaji
huu mpya wa umeme iko mbioni na tuna mradi
ambao unaendelea sasa na uko kwenye hatua nzuri
ambao tunaanza kujenga line kubwa kutoka
Makambako kwenda mpaka Songea.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, sambamba na hiyo
mipango inaendelea ili kuhakikisha kwamba kabla ya
uzalishaji huo haujafikiwa basi tumeshajenga line ya kutosha kuweza kusafirisha umeme huo ambao
utazalishwa.

Lakini jibu la kipengele cha (b) kwamba mikopo
iweze kutolewa, kuna watu wamekopa na wanahitaji
kurejesha hapa nafikiri swali la msingi lilikuwa limejikita kwenye suala zima la watu waliopoteza ajira. Sasa kama kuna watu ambao wamekopa mikopo na wanahitaji kufanya marejesho kupitia tatizo hili la umeme kwamba wanapata shida, basi hili ni jambo ambalo nafikiri kimsingi ni lazima sisi kama Serikali tuliangalie. Lakini lina namna nyingi ya kuweza kuliangalia, si namna peke yake tu ya kuangalia katika Wizara ya Nishati na Madini kwa maana ya kulipa fidia kupitia kwenye Wizara yetu.

Mheshimiwa Spika, lakini niseme tu kwamba, tatizo
hili ni la Kitaifa na wote tunafahamu sababu
zilizotupelekea kufikia kwenye hatua hii ni kuamini kwamba vyanzo vya maji vingeendelea kuwepo. Lakini sasa Serikali imejikita katika suala zima la kuhakikisha tunaanzisha vyanzo vingine vya kuzalisha umeme kwa njia nyingine kama jua, makaa ya mawe, gesi ambayo inatusaidia sana na hivi tunashukuru Mungu kwamba, tunaendelea kugundua gesi kwa kiasi kikubwa katika
exploration zinazoendelea.