You are using an older version of Internet Explorer.

In order to get the most out of our website, you can get a free update of Internet Explorer.
If you're using a work computer, please contact your IT administrator.

[CLOSE]
  email E-mail this to a friend email Printable version

Supplementary Question

mp Mbassa, Antony Gervase[CHADEMA]

Biharamulo Magharibi Constituency
Session No Question Number To the Ministry of Sector Date Asked
8 109 REGIONAL ADMINISTRATION AND LOCAL GOVERNMENT Local Government 2 July 2012
Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza
swali la nyongeza. Nianze kwa ku-declare interest
kwamba mimi ni Mjumbe wa Kamati ya Huduma za
Jamii, sasa swali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika shule nyingi
ambazo tumepita kuna uhaba mkubwa sana wa
walimu wa taaluma hususani kuhudumia watu wenye
ulemavu. Serikali ina mpango gani wa kuongeza
idadi ya walimu hawa?
ANSWERS TO SUPPLEMENTARY QUESTION #  109  SESSION #  8
mp Answer From Hon.Mwanri, Aggrey Deaisile Joshua
REGIONAL ADMINISTRATION AND LOCAL GOVERNMENT
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA
MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (TAMISEMI):

Mheshimiwa
Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Dkt. Mbassa kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, tumezungumza na watu
wa kitengo hiki mara tu baada ya kupata hili swali.

Tumshukuru sana Mheshimiwa Kwegyir ambaye
anafuatilia sana masuala ya walemavu. Kila wakati
tumekuwa na utaratibu wa kuhakikisha kwamba
walimu hawa wanaongezeka na idadi yao
inaongezeka. Sina takwimu hapa kwamba ni kiasi gani
tumefanya katika hilo eneo na niombe tu kumthibitishia
kwamba kila wakati idadi hii imekuwa inaongezeka,
wengine wako katika shule wanafundisha, lakini
anaamua kwenda Chuo Kikuu ili kwenda kujifunza
mafunzo maalum kwa ajili ya walemavu. Mimi
mwenyewe nimejifunza habari hii, mwalimu wangu
pale Chuo Kikuu Dkt. Gichoi ndiyo alikuwa
anafundisha, nafikiri siku hizi wanamwita Dkt. Mboya.

Ametufundisha eneo hili kwa hiyo, nalifahamu jambo
analolizungumza hapa. Lakini idadi yao imekuwa
inaongezeka kutokana na mahitaji haya ya nchi kwa
ujumla. Baadaye nitamtafutia takwimu ili kuweza
kuona jinsi ambavyo imekuwa inapanuka.