You are using an older version of Internet Explorer.

In order to get the most out of our website, you can get a free update of Internet Explorer.
If you're using a work computer, please contact your IT administrator.

[CLOSE]
  email E-mail this to a friend email Printable version

Supplementary Question

mp Abwao, Chiku Aflah[CHADEMA]

Special Seat
Session No Question Number To the Ministry of Sector Date Asked
8 226 REGIONAL ADMINISTRATION AND LOCAL GOVERNMENT Local Government 20 July 2012
Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa Mheshimiwa Waziri ameona umuhimu wa Kamati ya Fedha kushiriki katika Mipango ya Maendeleo na kwa kuwa Wabunge wa Viti Maalum ni Madiwani.

Je, Serikali itaangalia lini utaratibu wa Wabunge
wa Viti Maalum kushiriki katika Kamati ya Mipango na Fedha katika maeneo yao kwa kuwa suala hili
limekuwa likizungumzwa mara kwa mara na
Mheshimiwa Waziri Mkuu alilitolea maelezo kwamba
hakuna tatizo. Mheshimiwa Waziri mwenyewe
alishawahi kuzungumzia umuhimu huo, lakini
utekelezaji wake unasuasua. Ni lini sasa utakamilisha kanuni ili tuweze kushiriki Wabunge wa Viti Maalum katika Kamati ya Mipango na Fedha?
ANSWERS TO SUPPLEMENTARY QUESTION #  226  SESSION #  8
mp Answer From Hon.Mwanri, Aggrey Deaisile Joshua
REGIONAL ADMINISTRATION AND LOCAL GOVERNMENT
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA
MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (TAMISEMI):

Mheshimiwa Naibu Spika, namshukuru sana Mheshimiwa Chiku Abwao kwa kutambua kwamba tuliwahi kulisemea jambo hili. Mimi niliwahi kusimama hapa nikasema nimezaliwa na mama na mke wangu ni mama. Kwa hiyo najua umuhimu na wala hapa sitaki kuzua mgogoro hapa tukaanza kushindana hapa umuhumi wa hawa. Mimi natambua akinamama wana umuhimu mkubwa sana katika taifa.

Jana ameondoka Mheshimiwa Rais wa Liberia mwanamama, amekuja hapa tumemwona wote mizinga 21 amepigiwa pale.

Kwa hiyo natambua umuhimu wao na Chama changu
cha Mapinduzi kinawatambua akinamama.
Tulipokuwa tunajibu jambo hili tulisema kabisa
kwamba Mbunge huyu wa namna hii kwa sababu ni
wa Mkoa walau achague Halmashauri moja ambayo
angetaka ashiriki. Kwa sababu hawezi akawa anatoka
Rombo, anakwenda Siha anakwenda kule, anakwenda Same pamoja na kwamba anawahudumia wananchi. Ikasemwa kwa uzito mkubwa sana baadaye Mheshimiwa Waziri Mkuu kwa sababu limekuwa linajitokeza akalibeba yeye mwenyewe.

Sasa hebu jiulize Waziri Mkuu na mimi nani
mkubwa? Yaani mimi nianze kukataa hapa, Waziri
Mkuu alishasema analibeba na mimi nikisema nikujibu kwamba sasa tayari imekuwa, ataniambia bwana mdogo hii habari umeipata wapi.

Nataka nithibitishe kwako hapa kwamba jambo
hili Mheshimiwa Waziri Mkuu amelichukua kwa uzito
mkubwa. Kwa hiyo anaendelea kulifanyiwa kazi,
tunaiona hiyo concern na haya mabadiliko ambayo
yanatokea na nadhani kwamba tutafika mahali
tutalitatua. Kwa hiyo tunakaribisha wazo hili na
tunawatambua akinamama.