| E-mail this to a friend | Printable version |
|
||||||
| Session No | Question Number | To the Ministry of | Sector | Date Asked | ||
|---|---|---|---|---|---|---|
| 8 | 297 | EDUCATION AND VOCATIONAL TRAINING | Education | 31 July 2012 | ||
| Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Nina maswali madogo ya nyongeza. (a) Kwa kuwa inajulikana kabisa kwamba kuna shule nyingi sana za watoto wenye ulemavu na Waziri anashuhudia kwa sababu tumezitembelea hizo shule na tumewakuta watoto hawa wanahangaika, ninaomba kujua hivi ni kweli Serikali inayo takwimu ya wanataaluma ambao wamemaliza? (b) Je, Serikali sasa inawaambia nini hawa watoto ambao wamekuwa wanahangaika wanashinda mchana kutwa bila kufundishwa wakati walimu wapo ambao hawana kazi? |
||||||
| ANSWERS TO SUPPLEMENTARY QUESTION # 297 SESSION # 8 | ||||||
|
||||||
| NAIBU WAZIRI WA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI: Mheshimiwa Spika, kama nilivyosema kwenye jibu langu la msingi, takwimu za walimu waliomaliza Vyuo vye Elimu Maalum ambavyo kwa Tanzania nzima tunavyo Vyuo viwili tu vinavyotoa mafunzo ya Elimu Maalum. Kwa Chuo cha Serikali ni chuo cha Arusha chuo cha Patandi na Shirika la dini wametusaidia kuanzisha chuo pale SECUCO. Hivyo ndiyo vyuo pekee vinavyotoa mafunzo kwa walimu elimu maalum kwa Msingi, Sekondari na hata Shahada. Mheshimiwa Spika, kuhusu takwimu kwa sababu amehitaji ninazo ofisini nitajaribu kumpatia Mbunge. Lakini hapa ninayo takwimu tu ya Walimu waliomaliza ambao ni 539 kwa mwaka 2010/2011. Mheshimiwa Spika, swali la pili juu ya watoto wanaohangaika hawana walimu. Ni kweli tumejaribu kulihangaikia hili na ndiyo maana tukalifanyia uharaka wa hali ya juu sana. Wapo Walimu ambao hawajaajiriwa, Walimu wa Kawaida lakini kwa wale wa Elimu Maalum tumewajumuisha pamoja kwa miaka yote miwili 2010/11 tumeweza kuwaajiri mwezi huu wa saba na Wabunge mkienda kwenye tovuti ya Ofisi ya Waziri Mkuu TAMISEMI inayoshughulikia Elimu Maalum kwa kushirikiana na Wizara ya Elimu tumeweka tayari Walimu ambao watasambazwa kwenda kufundisha kwenye hizo shule za Elimu Maalum. |
||||||