| E-mail this to a friend | Printable version |
|
||||||
| Session No | Question Number | To the Ministry of | Sector | Date Asked | ||
|---|---|---|---|---|---|---|
| 7 | 115 | EDUCATION AND VOCATIONAL TRAINING | Education | 20 April 2012 | ||
| Mheshimiwa Spika, ahsante. Pamoja na majibu mazuri kabisa ya Mheshimiwa Naibu Waziri, naomba kumwuliza swali moja la nyongeza kama ifuatavyo:- Kwa kuwa katika Mkoa wa Kanda ya Ziwa hususani Mkoa mpya wa Geita tatizo la ukosefu wa mabweni ni kubwa na ni kubwa kweli kweli. Watoto wetu na hasa watoto wa kike wamekuwa wakipata elimu yao katika mazingira magumu na hatarishi kweli kweli. Mheshimiwa Spika, watoto hawa wamekuwa wakilazimika kupanga kwenye nyumba za watu binafsi na kibaya zaidi wamekuwa wakipata mimba na magonjwa mbali mbali mabaya kama UKIMWI na kadhalika. Je, Serikali haioni kuna haja ya kunusuru maisha ya watoto hawa kwa kutumia hata Mashirika ya Umma kama vile National Housing Corporation (NHC) kuweza kujenga mabweni katika shule zetu za Sekondari? |
||||||
| ANSWERS TO SUPPLEMENTARY QUESTION # 115 SESSION # 7 | ||||||
|
||||||
| NAIBU WAZIRI WA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI: Mheshimiwa Spika, kama tulivyosema katika awamu ya kwanza, Serikali inayo nia ya kuendeleza elimu nchini, lakini kikubwa hapa ni ufinyu wa bajeti. Kama tulivyosema pia kwamba, tumetenga fedha kwenye mpango wa MMES wa kujenga hosteli 20 at least kwa kila mwaka. Naomba labda nimweleweshe Mheshimiwa Mbunge jambo moja, tunaposema shule za bweni na tunaposema kujenga hosteli ni kitu tofauti kabisa. Shule za bweni maana yake wanafunzi wote kutoka Form One ama mpaka Form Six maana yake wanakaa shuleni hapo hapo, wavulana au wasichana, wanakula hapo, wanalala hapo na wanachaguliwa kutoka sehemu mbalimbali za Tanzania Bara. Mheshimiwa Spika, hosteli ni nyumba tunazojenga kwa kushirikiana na Halmashauri ama Baraza la Madiwani kule kwenye Kata, zile Ward C’s, wanakaa pamoja wanakubaliana kwamba tujenge hosteli kwa ajili ya watoto wanaokaa mbali na kituo cha shule kilipo, maana wanatoka kwenye vijiji mbali kidogo. Kwa hiyo, hosteli ni nyumba tu ambayo tunakuwa tumeweka pale kwa ajili ya wanafunzi wanaotoka mbali lakini inakuwa ni mchanganyiko, wanafunzi wanaokaa hosteli na wengine wanatoka mbali. Tunazo shule za mfano huo kama vile Lugalo, Mbeya Day, hata pale Azania na Tambaza. Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, kunakuwa na wanafunzi wanatoka day na wengine wanakaa pale hosteli, lakini shule za bweni ni kwa ajili ya bweni tu na watoto wanatoka katika different dejects kama vile Songea Boys, Tabora Boys na shule zingine za mfumo huo. Kwa hiyo, kwa upande wa Geita, ukosefu wa hosteli, namwomba Mheshimiwa Mbunge kwa sababu na yeye ni Mjumbe kwenye Halmashauri ya Wilaya, wakae, wapange, waone ni namna gani wataweza kusaidia. Lakini bado Serikali sisi tutachangia mfumo mwingine kama nilivyosema kwamba tutajenga hosteli 20 na kila mwaka tunaweka bajeti hiyo. |
||||||