You are using an older version of Internet Explorer.

In order to get the most out of our website, you can get a free update of Internet Explorer.
If you're using a work computer, please contact your IT administrator.

[CLOSE]
  email E-mail this to a friend email Printable version

Supplementary Question

mp Bulaya, Ester Amos[CCM]

Special Seat
Session No Question Number To the Ministry of Sector Date Asked
7 102 COMMUNITY DEVELOPMENT, GENDER AND CHILDREN Projects/Fund 19 April 2012
Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Asasi
nyingi zisizokuwa za Kiserikali, zimekuwa zikisaidiana na Serikali katika
kutoa elimu katika jamii na kusaidia shughuli za kimaendeleo. Lakini
baadhi ya asasi zisizo za Kierikali zimekuwa zikishindwa kufanya hivyo na
matokeo yake kujihusisha kwenye masuala ya kisiasa na kujenga chuki
kati Serikali na wananchi kwa ajili ya kutimiza azma za kisiasa kwa baadhi
ya vyama fulani fulani:-

(a) Mheshimiwa Spika, huku tunakoelekea, tunaenda katika
mchakato wa Katiba mpya na tuna habari kwamba kuna baadhi ya
vyama vimejipanga kuhakikisha kuleta asasi zisizo za Kiserikali kwa ajili ya
kushinikiza wananchi kutimiza malengo yao ya kisiasa na agenda zingine
katika Katiba mpya.

Je, Serikali wanalijua hilo na wamejipanga vipi?
(b) Mheshimiwa Spika, kuna malalamiko katika ada ya usajili na
kama tunavyojua vijana wengi ambao wanamaliza elimu ya juu mbali ya
kwamba kuna tatizo ya ajira, lakini wengi wamekuwa wakipenda
kuanzisha NGO zao, lakini wanakwama kwenye ada ya usajili.

Je, Serikali haioni kwamba kuna haja ya kupunguza ada hiyo ili
vijana wengi waweze kuanzisha NGOs zao?

Mheshimiwa Spika, ada yenyewe ni
shilingi laki mbili.
ANSWERS TO SUPPLEMENTARY QUESTION #  102  SESSION #  7
mp Answer From Hon.Simba, Sophia Mattayo
COMMUNITY DEVELOPMENT, GENDER AND CHILDREN
WAZIRI WA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA NA WATOTO:

Mheshimiwa
Spika, naomba kumjibu Mheshimiwa Ester Bulaya, maswali yake mawili ya
nyongeza:-

Kwanza ningependa niwafahamishe wananchi kwamba kila NGO
imeanzishwa ikiwa na majukumu ambayo yamo katika Katiba yake. Kwa
hiyo NGO ambazo zinaacha majukumu yake na kufanya majukumu
mengine ni uvunjaji wa sheria ambayo imeunda ile NGO.
Wizara yangu kwa kushirikiana na Baraza la Taifa la NGO iliandaa
Kanuni za madili za NGO ambayo ilipitishwa 2008. Kwa hiyo, hizo NGOs
zikiwemo pia na NGO za briefcase zinatakiwa kuchukuliwa hatua:-

(a)Mheshimiwa Spika, tuna Maafisa Maendeleo ya Jamii ambao ni
wasajili wa NGOs katika kila Wilaya. Kwa hiyo, kwa kupitia Bunge hili nawahamasisha na kuwaagiza wale Maafisa wa Maendeleo ya Jamii
katika Wilaya waangalie kwamba NGOs ambazo zinafika katika maeneo
yao na kufanya majukumu mbali na yale ambayo yameandikwa
watufahamishe ili hatua stahiki zichukuliwe.

(b)Swali la pili linazungumzia kuhusu ada ya usajili kuwa ni ya juu.
Naona hili pengine tulichukue na tulifanyie kazi. Lakini nadhani ada
iliyopo si kubwa kiasi hicho, lakini bado mimi nalichukua tuliangalie
pengine inawezekana ni kweli kwa vijana ambao wanaanzisha asasi zao
wanashindwa kufanya hivyo. Ahsante sana.

ANSWERS TO SUPPLEMENTARY QUESTION #  102  SESSION #  7
mp Answer From Hon.Malima, Adam Kighoma Ali
COMMUNITY DEVELOPMENT, GENDER AND CHILDREN
test