You are using an older version of Internet Explorer.

In order to get the most out of our website, you can get a free update of Internet Explorer.
If you're using a work computer, please contact your IT administrator.

[CLOSE]
  email E-mail this to a friend email Printable version

Supplementary Question

Session No Question Number To the Ministry of Sector Date Asked
8 328 INFORMATION, CULTURE AND SPORTS Youth 6 August 2012
Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali moja la nyongeza. Kwa kuwa, fursa nyingi wamekuwa wakizipata vijana wengi walioko mijini, je, Serikali, ina mkakati gani wa kuwafikia vijana walioko vijijini katika uundwaji wa Baraza hili?
ANSWERS TO SUPPLEMENTARY QUESTION #  328  SESSION #  8
mp Answer From Hon.Makalla, Amos Gabriel
INFORMATION, CULTURE AND SPORTS
NAIBU WAZIRI WA HABARI, VIJANA, UTAMADUNI NA
MICHEZO:

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba, inawezekana kuwe na hofu kwamba, vijana wa Vijijini wasipate uelewa juu ya suala hili. Wizara yangu imejipanga kuwaelimisha vijana, kutakuwa na vipindi kuelekea katika kuunda Baraza la Vijana kuanzia katika
Television na Redio, ili kupata uelewa. Pia Baraza hili, litakuwa na muundo kuanzia Vijijini hadi Taifa.