| E-mail this to a friend | Printable version |
| Session No | Question Number | To the Ministry of | Sector | Date Asked | ||
|---|---|---|---|---|---|---|
| 7 | 116 | AGRICULTURE, FOOD SECURITY AND CO-OPERATIVES | Food/Agriculture | 20 April 2012 | ||
| Nashukuru Mheshimiwa Spika, kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Kwa kuwa yapo malalamiko mengi juu ya suala hili kwa nini isiundwe Tume Maalum kwa ajili ya kwenda kuchunguza suala hili badala ya kumtuma mtu mmoja ambaye ni Rais kudanganywa? Swali la pili, kwa kuwa taarifa hiyo iliyotolewa imeandaliwa na Halmashauri ya Wilaya ambao ni watuhumiwa wakuu katika suala hili. Je, Mheshimiwa Waziri yuko tayari kuongozana na mimi mpaka kwa wananchi hao kwenda kusikiliza kero zinazohusiana na Wizara yake? |
||||||
| ANSWERS TO SUPPLEMENTARY QUESTION # 116 SESSION # 7 | ||||||
|
||||||
| WAZIRI WA KILIMO, CHAKULA NA USHIRIKA: Mheshimiwa Spika, sioni kama kuna sababu ya kuunda Tume Maalum wakati ambapo Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Serikali ameshaandaa ukaguzi maalum katika jambo hili. Hatua ya kwanza ya ukaguzi huo yaani ile preliminary audit imeshakamilika na wanajiandaa sasa kwenda kufanya ukaguzi wa pili. Kwa hiyo, tungoje taarifa yake ili tuweze kuchukua hatua stahiki. Pili, nitafuatana na Mheshimiwa Mbunge kwa furaha kabisa ili kusikiliza malalamiko ya wananchi. |
||||||