| E-mail this to a friend | Printable version |
|
||||||
| Session No | Question Number | To the Ministry of | Sector | Date Asked | ||
|---|---|---|---|---|---|---|
| 4 | 362 | HEALTH AND SOCIAL WELFARE | Health | 3 August 2011 | ||
| Ahsante Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kunipa nafasi niweze kuuliza maswali ya nyongeza. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri, ninapenda kuuliza maswali madogo mawili kama ifuatavyo:- (i) Kwa kuwa asilimia tatu ya mshahara wanaokatwa wafanyakazi pamoja na ile inayotolewa na waajiri wao ni chanzo kimojawapo katika Mfuko huu wa Bima ya Afya; Serikali haioni kwamba ipo haja ya kuangalia upya marupurupu na mishahara wanayopata Wafanyakazi wa Mfuko kwa kuwa imelalamikiwa kuwa ni mikubwa inatokana na mishahara ya wafanyakazi wetu wa nchi hii? (ii) Kwa kuwa wataalam wameonesha kwamba kitendo cha kutahiri kinapunguza maambukizo ya UKIMWI kwa asilimia 30; je, kwa nini Mfuko huu usiweke circumcision kama gonjwa mojawapo ambalo linalipiwa na Mfuko kuliko ilivyo sasa kwa kuwataka wanaofanyiwa kitendo cha utahiri kutokulipiwa na Mfuko huu? |
||||||
| ANSWERS TO SUPPLEMENTARY QUESTION # 362 SESSION # 4 | ||||||
|
||||||
| WAZIRI WA AFYA NA USTAWI WA JAMII: Mheshimiwa Mwenyekiti, la kwanza, ninakubaliana naye kwamba, kuna haja ya kuangalia upya marupurupu ya Wafanyakazi wa Mfuko huu, lakini vilevile tukilenga kuboresha huduma zaidi ambazo wanazitoa. Hiyo ninakubaliana na Mheshimiwa Hokororo, tutaifanyia kazi. Swali la pili kuhusu tohara kwa wanaume; ni kweli tafiti za kisayansi zimeonesha kwamba, wale ambao wanapata tohara wanapunguza uwezo mkubwa zaidi wa maambukizi ya Virusi vya UKIMWI, ukifananisha na wale ambao hawakupata tohara. Ninaomba nilitaarifu Bunge lako Tukufu kwamba, Wizara ya Afya tuna mpango kwa Mikoa ambayo ina viwango vya chini vya wanaume waliotahiriwa na vilevile wana viwango vya juu vya maambukizi ya Virusi vya UKIMWI, tunafanya tohara hiyo bure. Vilevile Mfuko huu nao umeliangalia hili suala na ninaomba nimpe taarifa Mheshimiwa Hokororo kwamba, ni mojawapo ya vitita vilivyoongezwa katika huduma ambazo Mfuko wanatoa pamoja na tohara kwa wanaume. |
||||||