You are using an older version of Internet Explorer.

In order to get the most out of our website, you can get a free update of Internet Explorer.
If you're using a work computer, please contact your IT administrator.

[CLOSE]
  email E-mail this to a friend email Printable version

Supplementary Question

mp Lwanji, John Paul[CCM]

Manyoni Magharibi Constituency
Session No Question Number To the Ministry of Sector Date Asked
8 14 ENERGY AND MINERALS Energy 13 June 2012
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa hali ya Shule ya Sekondari ya Puma inafanana kabisa na ile ya Sekondari ya Sanjaranda, Wilaya ya Manyoni. Je, Wizara itakuwa tayari kuiingiza shule hii katika mpango wake ili iweze kupata umeme?
ANSWERS TO SUPPLEMENTARY QUESTION #  14  SESSION #  8
mp Answer From Hon.Simbachawene, George Boniface Taguluvala
ENERGY AND MINERALS
NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI:

Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la
Mheshimiwa John Lwanji, ambalo ameliuliza kuhusiana na sekondari iliyopo Wilaya ya Manyoni.

Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyosema, REA wameonesha jitihada kubwa ya kufikia maeneo mengi, basi katika mipango inayofuata ya REA ni suala la mawasiliano ili tuweze kuona kama kweli na utafiti utakaofanywa na wataalam wetu ukithibitisha kwamba kweli kuna umuhimu huo, basi tunaweza tukajitahidi. Kama nilivyosema, njia ya solar pia inaweza ikatusaidia sana katika kupunguza matatizo ya maeneo ambayo hayajafikiwa na grid.