You are using an older version of Internet Explorer.

In order to get the most out of our website, you can get a free update of Internet Explorer.
If you're using a work computer, please contact your IT administrator.

[CLOSE]
  email E-mail this to a friend email Printable version

Supplementary Question

mp Lwanji, John Paul[CCM]

Manyoni Magharibi Constituency
Session No Question Number To the Ministry of Sector Date Asked
8 102 COMMUNICATION, SCIENCE AND TECHNOLOGY Communication 29 June 2012
Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri nina maswali mawili ya nyongeza. Kwanza katika Wilaya hii ya Manyoni na hasa hizo tarafa zilizotajwa za Kintinku na Nkonko tuliwasilisha kwa pomoja kwa upande mwingine wa Wilaya upande wa Magharibi tuliwasilisha maombi kwa Kata ya Mamaghembe
Ipandye na Idondyandole.

Sasa napenda kujua hali ya hizi Kata katika huo
mchakato unaozungumza ikoje maana utafiti
ulifanywa na imeonekana kabisa hawa watu kiuchumi
wanaweza kupatiwa huduma hiyo?

Swali la pili, ni kweli kwamba mwaka jana au
mwaka juzi tulijaza fomu. Wakuu hawa wa Makampuni
walikuwa kwenye Ukumbi wa Msekwa tukajaza fomu
hizo lakini hali halisi inavyoonekana kwa kweli utoaji wa huduma hii ya minara unasuasua sana. Sasa napenda nieleweshwe ni nini hasa mahusiano haya?

Ni ushawishi tu mahusiano kati ya Serikali na haya
makampuni, uhusiano wake hasa ni upi katika
kushawishi haya makampuni? Maana inaonekana
kwa upande mwingine Serikali kama vile haina control kabisa katika eneo hili?
ANSWERS TO SUPPLEMENTARY QUESTION #  102  SESSION #  8
mp Answer From Hon.Makamba, January Yusuf
COMMUNICATION, SCIENCE AND TECHNOLOGY
NAIBU WAZIRI WA MAWASILIANO, SAYANSI NA TEKNOLOJIA:

Mheshimiwa Spika, kwanza nitakapoleta ile orodha tutatazama kama maeneo ya Jimbo lako yamo na kama hayamo basi utaongeza na tutayafanyia kazi.

Kuhusu hili la pili, msingi wa biashara ya
mawasiliano ni biashara ya faida na makampuni haya
hayalazimishwi kupeleka mawasiliano katika maeneo
ambayo wanaona hayana mvuto wa kibiashara.
Ndiyo maana Serikali ilianzisha mfuko wa UCAF, Mfuko wa Mawasiliano kwa wote msingi wake ni kutoa ruzuku kwa makampuni ya simu kupeleka mawasiliano katika maeneo ambayo hayana mvuto wa kibiashara.

Sasa mwanzo tulikuwa hatuna hakika kwamba moja, gharama halisi za kupeleka mawasiliano kwenye
eneo mahususi ni kiasi gani. Kwa hiyo, ruzuku
inayohitajika ni kiasi gani. Hizo taarifa hazikuwepo.

Tulichofanya sasa hivi ni kufanya tathimini ya kila kijiji na kujua gharama halisi za kupeleka mawasiliano kwenye kila kijiji na kutangaza tender kwa kila kijiji mahususi na ambacho tunajaribu kufanya ni kwamba katika yale
maeneo ambayo makampuni ya simu yana minara
inayozunguka katika maeneo haya inawezekana
kampuni ya Vodacom tayari imewekeza katika
maeneo ambayo ni jirani na Manyoni magharibi na
kampuni ya Airtel imewekeza katika maeneo jirani na Wilaya ya Liwale kwa hiyo tunajaribu kutoa ruzuku kulingana na uwepo wa Makampuni katika maeneo mahususi.

Mheshimiwa Spika, tunaamini njia hii na utafiti
tulioufanya upya na model hii mpya ambayo
tumeitengeneza itasaidia kuharakisha zoezi hili na
tayari tumepata fedha shilingi bilioni 45 kutoka Benki ya Dunia kwa ajili ya kugharamia awamu ya kwanza ya kazi hii.

Kwa hiyo, nataka niwahakikishie Waheshimiwa
Wabunge kwamba baada ya kutengeneza utaratibu
huu mpya zoezi hili litaenda haraka. Pale mwanzo
tulikuwa tunachelewa kwa sababu tulikuwa hatuna
hakika na kiwango cha ruzuku na utaratibu tuliouweka.

Kwa hiyo, sasa hii sio ahadi tu. Hii sasa ni utekelezaji.