You are using an older version of Internet Explorer.

In order to get the most out of our website, you can get a free update of Internet Explorer.
If you're using a work computer, please contact your IT administrator.

[CLOSE]
  email E-mail this to a friend email Printable version

Supplementary Question

mp Maige, Ezekiel Magolyo[CCM]

Msalala Constituency
Session No Question Number To the Ministry of Sector Date Asked
8 146 WATER Water 6 July 2012
Mheshimiwa Spika, naomba nimshukuru sana Naibu Waziri kwa majibu yake mazuri, naomba kuuliza swali moja dogo la nyongeza.

Mheshimiwa Spika mpango wa kuongeza vijiji au
miji inayonufaika na maji ya ziwa Viktoria umekuwepo kwa muda mrefu na kwa miji midogo inayozunguka Mji wa Kahama, miji inayoguswa na mpango huo ni pamoja na Mji mdogo wa Kagongwa na Isaka na mpango huu umekuwepo tangu mwaka 2008 na
mipango imekuwa ikiendelea. Nilitaka kufahamu. Je,
Serikali imefikia hatua gani sasa katika mpango wa
kuwapatia maji wananchi wa Isaka na Kagongwa
Wilayani Kahama ambao wapo kwenye mpango wa
maji ya Ziwa Victoria?
ANSWERS TO SUPPLEMENTARY QUESTION #  146  SESSION #  8
mp Answer From Hon.Mahenge, Dr. Binilith Satano
WATER
NAIBU WAZIRI WA MAJI:

Mheshimiwa Spika, ni kweli kumekuwa na mpango wa kupeleka maji kwenye vijiji vilivyokuwa kandokando ya bomba linalotoa maji kutoka ziwa Victoria kwenda Kahama na Shinyanga na mpango huu umekuwa ukitekelezwa kwa awamu.

Awamu ya kwanza ilikuwa ni kupeleka kwenye vijiji
vilivyo kilomita tano kutoka umbali wa bomba
ambavyo vilipatikana vijiji 54 na 39 vikaanza kupata maji.

Awamu ya pili ikaongezwa vifikie vijiji 96 na
uongezeke umbali wa kilomita 12 kutoka katikati ya
bomba kila upande. Sasa hivi kinachofanywa ni
kwamba tayari Serikali imeshatenga fedha katika
awamu hii tunayokwenda kwenye Bajeti bilioni moja
kwa ajili ya kufanya usanifu kwenye vile vijiji ambavyo vipo umbali wa kilomita 12, lakini vile vile kama utazingatia juzi tarehe 4 Julai, 2012 Wizara imeshatoa tangazo kwenye magazeti kuhusu zabuni ya kuepeleka maji Magu na Miji ya Ngudu na vile vile kutoka Victoria kwenda miji ya Meatu.

Kwa hiyo, mipango inaendelea na tutaendelea kukamilisha awamu kwa awamu.