You are using an older version of Internet Explorer.

In order to get the most out of our website, you can get a free update of Internet Explorer.
If you're using a work computer, please contact your IT administrator.

[CLOSE]
  email E-mail this to a friend email Printable version

Supplementary Question

mp Komba, Capt. John Damiano[CCM]

Mbinga Magharibi Constituency
Session No Question Number To the Ministry of Sector Date Asked
8 106 ENERGY AND MINERALS Energy 29 June 2012
Mheshimiwa Spika,
pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu
Waziri, nina maswali mawili ya nyongeza.

(a) Jambo hili la kupeleka umeme kutoka
Makambako kuelekea Songea na Mbinga sasa hivi ni
miaka karibu nane na ilikuwa kwenye Ilani ya Uchaguzi
ya miaka mitano iliyopita. Sasa kwa kuwa Halmashauri
ya Wilaya ya Mbinga imetoa jenereta na liko tayari na
imetoa kuanzia mwaka 2008, kuna ugumu gani wa REA
kwenda pale na kufanya network ya umeme ili mji
ule upate umeme?

(b) Mheshimiwa Naibu Waziri anajibu tu hivi
inaingia akilini au ama haiingii akilini kwamba makaa
ya mawe yanachumwa pale Ngaka, yanapelekwa
Malawi kuimarisha umeme wa Malawi na sisi pale
hatuna umeme hivi inaingia akilini, ama haiingii akilini?
ANSWERS TO SUPPLEMENTARY QUESTION #  106  SESSION #  8
mp Answer From Hon.Muhongo, Prof. Sospeter M.
ENERGY AND MINERALS
WAZIRI WA NISHATI NA MADINI:

Mheshimiwa Spika,
kwanza nimpongeze Mheshimiwa Mbunge na
niwapongeze Madiwani wote wa Halmashauri ya
Mbinga kwa kukubali na kuridhia kuachia jenereta
moja ambayo ilikuwa ikitumika kwenye Kiwanda cha
Kahawa itumike kupeleka umeme eneo la Mbamba
Bay.

Mheshimiwa Mbunge atakumbuka kuwa
Mheshimiwa Rais ameweza kutoa jenereta mbili katika
Wilaya ya Mbinga ili kutatua tatizo la umeme Wilaya ya
Mbinga na ni kweli kabisa kuwa Halmashauri ya Wilaya
ya Mbinga imeweza kutoa jenereta iliyokuwepo
kuipeleka Mbamba Bay, tayari tunafanya
mazungumzo na nimekwisha iagiza TANESCO pamoja
na REA watafute fedha kwa ajili ya kujenga miundo
mbinu ya kusambaza umeme kwa wateja, kazi
ambayo ingefanyika baadaye baada ya mradi wa
kutoa umeme kutoka Makambako- Songea kwenda
Mbinga Mbamba Bay ingekamilika. Kwa hiyo,
Mheshimiwa Mbunge kupitia Halmashauri ya Mbinga
wamekwenda hatua mbele zaidi ya kupata jenereta.
Kwa hiyo, kazi yetu sisi ni kuhakikisha kwamba
tunajenga miundombinu haraka ya kuwasambazia
wananchi umeme.

Mheshimiwa Spika, Katika swali lake la pili, jibu ni
haiingii akilini.

Mheshimiwa Spika,
nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali
inatambua hilo na tunafanya kazi sasa hivi ya
kuhakikisha kwamba rasilimali za makaa ya mawe
zinatumika kwanza kutosheleza mahitaji ya umeme wa
ndani kabla hatujafikia kuuza nje.

Kwa hiyo, kwa hiyo nimhakikishie Mheshimiwa
Mbunge makaa ya mawe yale hayapelekwi tu Malawi
lakini pia viwanda vyetu vya Sementi vya Twiga,
Mbeya pamoja na kiwanda cha Chai kinatumia
makaa ya mawe haya yanayotoka Mbinga. Lakini pia
tukijitosheleza kiu-meme, siyo vibaya pia kuuza kwa wenzetu.