| E-mail this to a friend | Printable version |
|
||||||
| Session No | Question Number | To the Ministry of | Sector | Date Asked | ||
|---|---|---|---|---|---|---|
| 4 | 387 | HOME AFFAIRS | Security | 9 August 2011 | ||
| Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Kwa kuwa kanda hii maalum ya kipolisi ya Rorya na Tarime inao upungufu mkubwa sana wa vitendea kazi kama magari na pikipiki, na kwa kuwa kanda hii ya kipolisi imeonyesha upungufu mkubwa sana wa utendaji wa kazi kutokana na upungufu wa vifaa hivyo: Je, Wizara ina mpango gani wa kuipatia kanda hii ya Tarime na Rorya vifaa kama magari na pikipiki ili waweze kutekeleza majukumu yao vizuri? |
||||||
| ANSWERS TO SUPPLEMENTARY QUESTION # 387 SESSION # 4 | ||||||
|
||||||
| NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli tumekiri hata katika bajeti ambayo tumeitoa majuzi ni kwamba upo upungufu wa vitendea kazi na hii siyo katika maeneo ambayo ameyataja yeye, lakini pia yako maeneo mengi nchini ambayo Waheshimiwa Wabunge hapa wamekuwa wakiyazungumzia. Namhakikishia kwamba kadri tutakavyokuwa tunapata fedha na uwezo utakavyokuwa unaruhusu, ndivyo tutakavyokuwa tunatoa vitendea kazi. Lakini kuhusu hali halisi ya Mkoa maalum huu wa Tarime - Rorya ni kwa sababu ya matatizo yao. Tutajitahidi kadri tuwezavyo kuupa kipaumbele. |
||||||