You are using an older version of Internet Explorer.

In order to get the most out of our website, you can get a free update of Internet Explorer.
If you're using a work computer, please contact your IT administrator.

[CLOSE]
  email E-mail this to a friend email Printable version

Supplementary Question

mp Murji, Hasnain Mohamed[CCM]

Mtwara Mjini Constituency
Session No Question Number To the Ministry of Sector Date Asked
4 183 WORKS Works 5 July 2011
Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kuniona. Kwa kuwa, ahadi ya kivuko cha mto Pangani inafanana na ahadi ya kupewa kivuko cha kutoka Mtwara kwenda Msanga Mkuu.

Je, ni lini pia ahadi hii itatekelezwa?
ANSWERS TO SUPPLEMENTARY QUESTION #  183  SESSION #  4
mp Answer From Hon.Mwakyembe, Dr. Harrison George
WORKS
NAIBU WAZIRI WA UJENZI:

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Hasnain, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, sio tu kivuko cha Msanga Mkuu, lakini vile vile tuna kivuko cha Rusumo, kivuko cha Kilambo, vyote hivi mikataba ya kuleta vivuko hivyo tulisaini mwezi Juni, mwaka 2010 na ujenzi umeendelea vizuri na unakamilika wakati wowote katika kipindi cha mwaka huu na miradi hii yote iko kwenye Ilani ya Uchaguzi. Kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge ajjue kwamba tunaijali sana.