Home » Members »Supplementary Question
Supplementary Question
 |
Daftari, Dr. Maua Abeid[CCM]
Special Seat |
|
|
|
|
|
|
| 10 |
10 |
WORKS |
Transport/Road |
29 January 2013 |
Mheshimiwa Spika, namshukuru Waziri, kwa majibu yake, lakini nina swali dogo tu la nyongeza. Kwa kuwa hivi sasa mvua zimeanza Dodoma na baadhi ya nyumba zetu nyingi zinavuja. Ni ile ile kusema kwamba, TBA inapaswa kuwajali wateja wake, lakini hilo bado halijafanywa. Majumba yetu yote yanavuja, mapanya yapo ndani na board zote zinaloa zina mipaka na mito mbalimbali juu. Hata kule Kisasa kwa Waheshimiwa Wabunge wanakokaa, fancing haijatiwa.
Mheshimiwa Spika, je, Mheshimiwa Waziri ananiambiaje? Ni lini shughuli hii itashughulikiwa ipasavyo?
|
| ANSWERS TO SUPPLEMENTARY QUESTION # 10
SESSION # 10 |
 |
Answer From Hon.Lwenge, Eng. Gerson Hosea Malangalila
WORKS |
|
NAIBU WAZIRI WA UJENZI:
Mheshimiwa Spika, kwanza nakiri kwamba, kama nyumba zinavuja ni jukumu la TBA kuzifanyia matengenezo, kwa hiyo, kazi hiyo, tutakwenda kuishughulikia.
Mheshimiwa Spika, sehemu ya pili kuhusu uzio katika nyumba za Kisasa, hiyo, tumeiweka kwenye mpango; tutafanyia kazi na tutajenga uzio kwenye nyumba zile za kisasa.
|
|
|
|