You are using an older version of Internet Explorer.

In order to get the most out of our website, you can get a free update of Internet Explorer.
If you're using a work computer, please contact your IT administrator.

[CLOSE]
  email E-mail this to a friend email Printable version

Contributions

Ali, Juma Othman[CCM]

Tumbatu Constituency
Session No Seating No Contribution Date Contribution To
4 29 20 July 2011 Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka 2011/2012 Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi
Mheshimiwa Spika, kumekuwa na
malalamiko mengi sana ya walimu wapya wanaoajiriwa kwa mara ya kwanza kukosa
mishahara yao kwa wakati, hivyo husababisha usumbufu mkubwa sana. Je, Serikali
itawasaidia vipi au itaweka mikakati gani ili kusaidia walimu hao kupata haki yao haraka
wanapoajiriwa? Ninaiomba Wizara ilifikirie sana suala hili ili kuepusha migogoro na pia
kuwarahisishia na kuwapunguzia ukali wa maisha walimu wapya.

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa wanafunzi muda mrefu wanakuwa shuleni kuliko
muda wanaokuwa nyumbani, ninaiomba Wizara ipange Mpango Maalum wa
kuwafundisha watoto wetu elimu ya nadharia kama hatari za madawa ya kulevya, mimba
za utotoni na madhara yake. Pia wapwewe elimu ya afya ya jamii.

Mheshimiwa Spika, ninaunga mkono hoja.