| E-mail this to a friend | Printable version |
|
|||||
| Session No | Seating No | Contribution Date | Contribution To | ||
|---|---|---|---|---|---|
| 8 | 13 | 29 June 2012 | Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka 2012/2013 – Ofisi ya Waziri Mkuu na Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa | ||
Mheshimiwa Spika, kwa kuwa Ofisi ya Waziri Mkuu ni ofisi muhimu sana katika kuratibu utaratibu wote katika Halmashauri zetu ili kusimamia maendeleo ya Mikoa na Halmashauri zote nchini Tanzania, naomba kutoa ushauri kwa Serikali kama ifuatavyo:- (i) Katika Halmashauri kuna mali nyingi sana za Serikali lakini usimamizi wake bado duni kwa mfano Kitengo cha Manunuzi bado hakijaimarishwa. Fedha nyingi sana zinapotea kupitia kitengo hiki. Kwa hiyo, Serikali iimarishe usimamizi madhubuti katika kitengo hiki kwa kufuata Sheria ya Manunuzi. (ii) Naomba Halmashauri zetu kuwa na miradi ili kupata mapato ya ndani siyo kutegemea ruzuku kutoka Serikali kuu. (iii) Halmashauri zina wawekezaji ambao wana miradi mikubwa kwa mfano viwanda vya chai, viwanda vya mbao na viwanda vya karatasi ambavyo vipo katika Jimbo la Mufindi Kusini, Wilaya ya Mufindi. Kwa hiyo, Halmashauri inaweza kufaidikia kupitia viwanda hivi kwa kupewa mrahaba kutoka katika viwanda hivi. Mheshimiwa Spika, suala la maji, katika vijiji vingi hapa Tanzania wana tatizo la maji, ndiyo maana Wabunge wengi sana wanauliza maswali ya maji hasa miradi wa World Bank bado haitekelezeki. Naomba Serikali itafute njia nyingine ili kutatua tatizo hili la maji. Katika Jimbo la Mufindi Kusini, kuna Vijiji vya Sawala, Kibao, Rufuna na Kipande. Wananchi wanapata shida ya maji, wananchi wameshachangia fedha mpaka sasa fedha zao zipo benki lakini Serikali bado haijapeleka maji kwa mradi huu wa World Bank. Mheshimiwa Spika, maji ni tatizo kubwa sana katika Jimbo la Mufindi. Serikali kwa kushirikiana na wananchi wa Jimbo la Mufindi Kusini walijenga matanki ya maji katika vijiji vya Sawala, Kibao, Igowole, Nyololo, Maduma na Nyigo lakini miundombinu yake imechakaa sana mpaka sasa hivi matanki hayo hayatumiki sababu miundombinu yake imechakaa. Naiomba Serikali kuchukua hatua za haraka ili kukarabati miundombinu ya maji katika Jimbo la Mufindi Kusini. Mheshimiwa Spika, naiomba Serikali kujenga barabara kwa kiwango cha lami, barabara ya Nyololo – Igowole – Kibao – Mtwango – Mgololo. Ni barabara muhimu sana katika uchumi wa Taifa kwa ujumla sababu imepita katika viwanda vikubwa vya chai, mbao, karatasi na viwanda vidogovidogo vya wajasiriamali. Pia kuna idadi ya watu wengi wanaoishi katika barabara hiyo. Naiomba sana Serikali kulichukulia hili kuwa ni tatizo kubwa katia Jimbo la Mufindi Kusini. |
|||||