| E-mail this to a friend | Printable version |
|
|||||
| Session No | Seating No | Contribution Date | Contribution To | ||
|---|---|---|---|---|---|
| 4 | 29 | 20 July 2011 | Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka 2011/2012 Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi | ||
Mheshimiwa Spika, katika kuchangia kwa maandishi hotuba ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, naomba kuchangia mambo matatu. Mambo hayo ni Elimu ya Awali, Elimu ya Msingi na Walimu. Mheshimiwa Spika, nikianza na Elimu ya Awali, kwanza kabisa kama tunataka elimu yetu iwe bora, ni lazima mtoto aandaliwe kwa Elimu ya Awali na hivyo basi, mtoto asomeshwe kwa vitendo ili atakapoingia katika Elimu ya Msingi asiwe mgeni na masomo atakayoyakuta huko. Maana katika Elimu ya Awali, mtoto anakuwa au shule nyingi za awali, watoto huwa wanasomeshwa masomo kwa Kiingereza hasa zile za kulipia. Kwa hiyo, ni ushauri wangu kwamba hata hizo za Serikali ambazo ziko kwenye Halmashauri, basi nazo ziboreshwe angalau mwanafunzi akitoka hapo akiingia Shule ya Msingi, anaendelea na siyo kuanza Alifu. Mheshimiwa Spika, kwanini tusiboreshe mitaala yetu ya Elimu ya Msingi ili mtoto anapotoka katika Elimu ya Awali asiyaone masomo mageni? Kwani Elimu ya Awali huwa wanasoma Kiingereza zaidi. Baadhi ya shule cha kusikitisha anapoingia elimu ya msingi ni Kiswahili kitupu, kwa hiyo, hapo unamrudisha nyumba na ndiyo maana elimu yetu inakuwa bora elimu tu na siyo elimu bora. Mheshimiwa Spika, nikija katika elimu ya msingi, wakati sasa umefika kurejesha elimu hii ya msingi ya kusoma kwa vitendo. Nakumbuka niliposoma mimi kipindi cha Sayansi huwa tunapelekwa laboratory kusoma kwa vitendo, tunafundishwa jinsi ya kuchuguza kitu kwa Microscope, tunajifunza kwa makundi. Hali kadhalika katika siku za project tunapelekwa shamba kulima, kupanda na kuvuna. Pia wakati wa mavuno au kazi za mikono hapo inakuwa tunafundishwa ubunifu wa kutengeneza vitu kwa mikono. Mheshimiwa Spika, naomba haya yote yarejeshwe, kwani mtoto akitoka hapo siyo lazima apate ajira Serikalini, yeye atakuwa na uwezo wa kujiajiri mwenyewe kwa sababu hiyo VETA siyo wananchi wengi wanaoweza kulipia watoto wao kwenda pale kusoma, jamani lazima tuwafikirie walio wengi siyo matajiri, ni masikini hasa. Mheshimiwa Spika, nikiwa kwa walimu ni watu waliosahaulika kabisa hata mishahara yao basi haikidhi haja. Kwa wanavyolitumikia Taifa hili karibia toka Rais hadi Mwenyekiti wa Kata anatokana na Mwalimu. Imefika wakati sasa tuwape motisha walimu wetu ili bado waendelee kusomesha kwa bidii ili Taifa lipate wataalam. Tunakoendea, tuwatunze walimu wetu. Katika bajeti hii shilingi bilioni 525.941 ni kwa ajili ya matumizi ya kawaida. Kwanini pesa hizi zisitiwe kwenye kwenye mishahara ya walimu ili basi wapate kufanya kazi kwa ufanisi zaidi? Mheshimiwa Spika, katika pesa za maendeleo, shilingi bilioni 139.632 ni pesa kidogo sana. Kwa kipindi hiki cha sayansi na teknolojia, maendeleo gani utayafanya? Naomba hapa nifahamishwe. Mheshimiwa Spika, kwanini hatubuni njia mbadala ya haya yote ili tuwe na elimu bora ili nayo iweze kutoa walimu bora pia tupate wanafunzi bora tuondokane na bora elimu? Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha. |
|||||