| E-mail this to a friend | Printable version |
|
|||||
| Session No | Seating No | Contribution Date | Contribution To | ||
|---|---|---|---|---|---|
| 4 | 19 | 5 July 2011 | Makadirio ya Matumizi ya Ofisi ya Rais (Menejimenti ya Utumishi wa Umma), (Utawala Bora), na Ofisi ya Rais (Uhusiano na Uratibu) kwa mwaka wa Fedha 2011/2012 | ||
Mheshimiwa Spika, kumekuwepo malalamiko toka kwa wananchi juu ya ajira na hususan taratibu iliyoanzishwa ya kuwa na Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma, kwa matarajio ingeweza kuleta ufanisi na kupunguza kero, matokeo yake yamekuwa tofauti na kuwa kero badala ya ufanisi na faraja. Mheshimiwa Spika, hofu yangu hayakufanyika maandalizi ya kutosha na kuiwezesha Sekretarieti hiyo kwa rasilimali fedha na watu kwa kuzingatia ukubwa wa nchi hii na mahitaji yake ya ajira pia uamuzi huo unakinzana na mpango wa kugatua madaraka na kuipunguzia mzigo Serikali Kuu ya maamuzi na kuwepo kwa Sekretarieti ya Ajira ni kinyume chake. Mheshimiwa Spika, ili kupunguza kero na malalamiko ipo haja Wizara kuangalia upya uwepo wa Sekretarieti hii na kama ni lazima basi wawezeshwe vya kutosha kukabili changamoto zilizopo na kupunguza malalamiko mengi. |
|||||