Parliament of Tanzania

Questions By: Hon. Eng. Atashasta Justus Nditiye

Primary Questions
MHE. ENG. ATASHASTA J. NDITIYE aliuliza:-
Je, Serikali ina mkakati gani wa makusudi wa kuwadhibiti wakimbizi hasa maaskari ambao hutoroka kambini Nduta na kwenda kujumuika na wananchi, hivyo kuhatarisha usalama wa wananchi?
MHE. VENANCE M. MWAMOTO (K.n.y. MHE. ENG. ATASHASTA J. NDITIYE) aliuliza:-
Katika Jimbo la Muhambwe kuna Chuo cha Wauguzi (MCH) ambacho ni muhimu sana katika sekta ya afya, lakini hakiko katika hali nzuri.
Je, Serikali ina mpango gani wa kukiboresha chuo hicho na vingine vya aina hiyo ili viweze kujiendesha na kulipa wazabuni wengi ambao wanawadai?
MHE. ENG. ATASHASTA J. NDITIYE aliuliza:-
Je, Shirika la UNHCR lina mpango wowote kwa usimamizi wa Serikali wa kujenga angalau wodi tatu za kulaza wagonjwa katika Hospitali ya Wilaya ya Kibondo?
MHE. ENG. ATASHASTA J. NDITIYE aliuliza:-
Mwezi Septemba, 2015 Mheshimiwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli, aliwaahidi wananchi wa Kata za Busonzu, Busagara na Murungu ambao wamepakana na Hifadhi ya Taifa ya Muyowosi kwamba mpaka kati ya wananchi hao na hifadhi hiyo, utarekebishwa ili wananchi wapate eneo kwa ajili ya kilimo.
Je, utekelezaji wa ahadi hiyo utaanza lini?
MHE. ENG.ATASHASTA J.NDITIYE aliuliza:-
Nchi yetu bado ina upungufu mkubwa sana wa sukari na kwa kuwa Wilayani Kibondo kuna ardhi oevu kwenye Bonde la Mto Malagarasi na Lupungu ipatayo ekari 52,000 na wananchi wako tayari kutoa ushirikiano kwa matumizi ya ardhi hiyo.
Je, Serikali haioni umuhimu wa kutafuta mwekezaji wa kiwanda cha sukari katika eneo hilo?
MHE. ENG. ATASHASTA J. NDITIYE aliuliza:-
Kwa muda wa zaidi ya miaka miwili, Hospitali ya Wilaya ya Kibondo haina mganga wa meno licha ya hospitali hiyo kuhudumia wagonjwa wengi kwa sasa ikiwemo wakimbizi kutoka nchini jirani ya Burundi:-
Je, ni lini Serikali itapeleka mtaalam wa meno katika hospitali hiyo?
MHE. MHANDISI ATASHASTA J. NDITIYE aliuliza:-
Gereza la Wilaya ya Kibondo – Nyamisati limekuwa na ongezeko kubwa sana la wafungwa na mahabusu kwa sababu ya uwepo wa wakimbizi.
Je, Serikali haioni sasa ni wakati unaofaa kupeleka mradi mkubwa wa maji kwenye gereza hilo ili kulinda afya za raia na askari walioko kwenye gereza hilo?
MHE. ENG. ATASHASTA J. NDITIYE aliuza:-
Kwa muda mrefu sasa Mji wa Kibondo hauna maji baada ya chanzo cha maji kuharibiwa na shughuli za kibinadamu:-
Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga mradi mwingine wa maji toka chanzo kingine (hasa Mto Malagarasi) ili Kata za Busunzu, Busagara, Lusohoko, Kitahana, Kumwambu, Kibondo Mjini na Miserezo zipate maji safi na salama?

Hon. Dr. Tulia Ackson

Speaker

Legislative Role

Profile

Ask the Speaker / Comments

Ms. Nenelwa J. Mwihambi

Clerk of the National Assembly

Legislative Role

Profile

Ask the Clerk / Comments

View All MP's